Advertise Here

Sunday, February 16, 2014

Tazama wimbo wa Joepraize - Mighty God.

Namna Uzinduzi wa FRIENDS' BARBECUE(FB) ulivyofana Jijini Mwanza.

Ijumaa ya February 14, 2014 ilikuwa ni siku ya Uzinduzi wa Event ya FRIENDS' BARBECUE(FB) Mkoani Mwanza ambapo shughuli hiyo ilifanyika Royal Sunset Beach Resort maeneo ya Malimbe, Jijini Mwanza.

Akizungumza kwa niaba ya Kamati ya Maandalizi, Noel Mlabwa a.k.a Papaa alisema kuwa |Lengo hasa la kuanzisha FRIENDS' BARBECUE(FB) ni baada ya kuona Vijana wengi wa Kikristo hasa wa Jijini Mwanza hawana sehemu ya kwenda kufurahi kwa pamoja kama Vijana wa kipendwa, hivyo ujio wa Event hii utakuwa unawakutanisha Vijana na kupata Nyama Choma, Vinywaji, Mafundisho mbalimbali ya Kikristo hasa ya vijana na Live Music.

Siku ya tukio watu wengi walionekana kufurahia tukio huku wengine wakiomba tukio hilo liwe ni la Mara kwa Mara.

Sasa Tazama namna mambo yalivyokuwa
Noel Mlabwa akielezea Maana ya FRIENDS' BARBECUE na Umuhimu wake
Ma Mc wa Event hiyo Sowane Emmanuel na Kabula Siza
Ma Mc wakipata picha ya pamoja na Best Couple
Ufunguzi wa Shampein
Raha ya Shampein tuone mapovu
Shampein
Mc Kabula(Kushoto) akiwa na Muimbaji Ester Nyanda
Happy People
Ni zaidi ya Furaha
Best Couple ikipokea Zawadi yao
Bw. James Kalekwa akiwa eneo la tukio
Victoria Napiya(Kushoto) akiwa na Deborah Shija(Kulia) wakiwa na Furaha ya kutosha
Ester Nyanda akiimba
Papaa Noel Mlabwa akienda sawa wakati Ester Nyanda akiimba
Mazungumzo na Majadiliano
Papaa Noel akijibu baadhi ya Maswali kutoka kwa Mc
Baadhi ya waliohudhuria event hiyo wakiwa makini kufuatilia kilichokuwa kikiendelea
Bw. James Kalekwa akijibu Maswali kutoka kwa Mc
Deborah Shija akijibu Maswali kutoka kwa Mc
Kamati iliyoandaa Friends' Barbecue ikiimba wimbo Maalum
Mc Sowane Emmanuel akilonga Jambo
So Happy
Chakula kwa Tumbo, Tumbo kwa Chakula
Soft Music ikiendelea
Watu wakiendelea kula
Supu pia ilikuwepo
Mc Sowane na Lilian Mhando
Baadhi wa waliohudhuria
Ilikuwa ni Valentine Day
Very funny! Vick akinywa Shampein kwenye chupa


Wapo pia waliokuwa wakilia Jikoni

Hapo kila mtu alikuwa busy kupiga picha
Kaa tayari kwa FRIENDS' BARBECUE(FB) nyingine baada ya uzinduzi rasmi wa Event hiyo jijini Mwanza.

Friday, February 14, 2014

Alichokiandika Mwimbaji John Lisu kuhusu watoto wake Mapacha watatu.

Wednesday, February 12, 2014

PCT walalamikia kukosa uwakilishi Bunge la Katiba.

Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Askofu David Butenzi, akizungumza na waandishi wa habari (hawako pichani), wakati Baraza la Maaskofu wa kanisa hilo lilipotoa tamko lao kuhusu kutopata nafasi
Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania (PCT), limesema limefedheheshwa na kusikitishwa kwa kunyimwa uwakilishi wa  kushiriki katika Bunge maalum la Katiba licha ya kuwasilisha  majina ya wajumbe wake.

Limesema kitendo cha kushindwa  kupewa fursa ya kushiriki katika Bunge hilo,  ni kuwanyima haki za msingi Watanzania wengi wanaowakilishwa na Baraza hilo, kama ilivyo kwa Watanzania wengine.


Akisoma tamko la baraza hilo mbele ya waandishi wa habari jana, baada ya kufikiwa katika mkutano ulioshirikisha Maaskofu wakuu wa Madhehebu ya Kipentekoste jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa PCT,  David Mwasota,  alisema wameamua kutoa tamko hilo ili kuonyesha namna ambavyo wamesikitishwa na kitendo hicho.


“Tumewaita leo (jana) ili mtusaidie kufikisha masikitiko yetu kwa viongozi, Watanzania  na waamini wa Kipentekoste kutokana na kitendo cha serikali yetu tunayoiheshimu, kuipenda na kuiombea, kwa kutubagua na kututenga katika bunge maalum la Katiba, huku  tukiwa ni  miongoni mwa taasisi kubwa za kidini na makundi mengine ya kijamii,” alisema na kuongeza:


“Ikumbukwe kuwa hivi karibuni Rais aliagiza makundi mbalimbali ya kijamii na taasisi za kidini kupendekeza majina ya watu wanaoona wanafaa kuchaguliwa kushiriki katika bunge maalum la Katiba na kwa kuzingatia wingi wa wanachama wetu tulipendekeza majina  tisa ya watu tulioona wanafaa kutuwakilisha, lakini cha kushangaza hakuna hata mmoja aliyeteuliwa.”


Aidha, aliongeza kuwa ikiwa serikali itaendelea kunga`ng`ania msimamo wake wa kutaka wajumbe wa baraza la PCT wasihusike katika Bunge hilo, Baraza litaitisha mkutano mkuu wa dharura wa kitaifa utakaojumuisha maaskofu wote wa kitaifa, Kanda na jimbo, mitume na manabii na  wachungaji zaidi ya 30,000 ili kutafakari kwa pamoja na kuamua hatua za kuchukua.


Mjumbe wa TCP ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la  Full Gospel  Bible Fellowship,  Zacharia Kakobe,  alisema Katiba ni haki ya Watanzania wote hivyo haoni sababu ya wengine kubaguliwa.

- Nipashe -