Advertise Here

Friday, February 14, 2014

Alichokiandika Mwimbaji John Lisu kuhusu watoto wake Mapacha watatu.

Wednesday, February 12, 2014

PCT walalamikia kukosa uwakilishi Bunge la Katiba.

Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Askofu David Butenzi, akizungumza na waandishi wa habari (hawako pichani), wakati Baraza la Maaskofu wa kanisa hilo lilipotoa tamko lao kuhusu kutopata nafasi
Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania (PCT), limesema limefedheheshwa na kusikitishwa kwa kunyimwa uwakilishi wa  kushiriki katika Bunge maalum la Katiba licha ya kuwasilisha  majina ya wajumbe wake.

Limesema kitendo cha kushindwa  kupewa fursa ya kushiriki katika Bunge hilo,  ni kuwanyima haki za msingi Watanzania wengi wanaowakilishwa na Baraza hilo, kama ilivyo kwa Watanzania wengine.


Akisoma tamko la baraza hilo mbele ya waandishi wa habari jana, baada ya kufikiwa katika mkutano ulioshirikisha Maaskofu wakuu wa Madhehebu ya Kipentekoste jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa PCT,  David Mwasota,  alisema wameamua kutoa tamko hilo ili kuonyesha namna ambavyo wamesikitishwa na kitendo hicho.


“Tumewaita leo (jana) ili mtusaidie kufikisha masikitiko yetu kwa viongozi, Watanzania  na waamini wa Kipentekoste kutokana na kitendo cha serikali yetu tunayoiheshimu, kuipenda na kuiombea, kwa kutubagua na kututenga katika bunge maalum la Katiba, huku  tukiwa ni  miongoni mwa taasisi kubwa za kidini na makundi mengine ya kijamii,” alisema na kuongeza:


“Ikumbukwe kuwa hivi karibuni Rais aliagiza makundi mbalimbali ya kijamii na taasisi za kidini kupendekeza majina ya watu wanaoona wanafaa kuchaguliwa kushiriki katika bunge maalum la Katiba na kwa kuzingatia wingi wa wanachama wetu tulipendekeza majina  tisa ya watu tulioona wanafaa kutuwakilisha, lakini cha kushangaza hakuna hata mmoja aliyeteuliwa.”


Aidha, aliongeza kuwa ikiwa serikali itaendelea kunga`ng`ania msimamo wake wa kutaka wajumbe wa baraza la PCT wasihusike katika Bunge hilo, Baraza litaitisha mkutano mkuu wa dharura wa kitaifa utakaojumuisha maaskofu wote wa kitaifa, Kanda na jimbo, mitume na manabii na  wachungaji zaidi ya 30,000 ili kutafakari kwa pamoja na kuamua hatua za kuchukua.


Mjumbe wa TCP ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Kanisa la  Full Gospel  Bible Fellowship,  Zacharia Kakobe,  alisema Katiba ni haki ya Watanzania wote hivyo haoni sababu ya wengine kubaguliwa.

- Nipashe -

Monday, February 10, 2014

Friends' Barbecue - Special Valentine Day, Ijumaa hii Mwanza.

Safu ya James Kalekwa; Mwisho tangu Mwanzo: Usuri wa njozi kwenye maisha binafsi. - Part 1

James Kalekwa
Mithali 29:18, “Pasipo maono, watu huacha kujizuia; Bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.”

Bwana Yesu asifiwe! Ndugu msomaji, ni neema kubwa sana ya Bwana Yesu kwamba tumepata kibali cha kuwa hai lakini zaidi kutumia uhuru wetu wa habari na utashi wetu kukutana hapa kwaajili ya kuanza mfululizo mpya juu ya “Usuri wa njozi kwenye maisha binafsi”.

Neno la utangulizi:
Je, unafanya mambo yaleyale kwa namna ileile huku ukitaraji matokeo tofauti?

Hagai 1: 5-7
“BWANA wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu. Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakinihapana aonaye moto; na yeye apataye mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka. BWANA wa majeshi asema hivi zitafakarini njia zenu.”

Mungu anawasemesha kitu cha tofauti na kigumu sana taifa la Israeli kupitia kinywa cha mtumishi wake Hagai. Wanaisha maisha yasiyo na tija – pesa ya mshahara haikai wala kuwazalia matunda yoyote, chakula hakiwashibishi tena na wala nguo haziwapi joto.

Wao wakijitazama wanaona hakuna tija lakini wanaendelea na mzunguko uleule wa maisha wakitegemea kupokea mabadiliko. Binafsi ninaamini kabisa, ni upumbavu kurudia mambo yaleyale huku ukitarajia matokeo ya kiutofauti kwenye maisha – ni upumbavu wa ngazi ya juu sana!

Ni kama Mungu anawaambia hakuna “njozi” ndani ya nguo, hakuna “njozi” ndani ya mshahara na hakuna “njozi” ndani ya chakula! Ninapata wapi ujasiri wa kusema hayo? Ni kwenye habari ya tija na faida ya mfumo wa maisha!

Soma maandiko hayo kwa jicho la kujifunza, utagundua ya kwamba ndugu hawa wameamua kuwekeza muda na nafasi zao kutafuta tija ya maisha kwa njia tatu:
Mshahara (pesa/mali)
Chakula na vinywaji
Mavazi

Lakini ukutazama kwa kina zaidi utagundua ya kwamba ndani ya hayo mambo mitatu, hawa ndugu hawakupata ridhiko la nafsi wala maisha yao. Ni kweli walikuwa wanapata mshahara, wanapata chakula na vinywaji na wanapata mavazi…

Lakini kulikuwa hakuna utoshelevu katika hayo! Kitu cha ajabu na cha kushangazwa ni kwamba, pamoja na hayo yote hawa ndugu waliendelea kufanya mambo yale yale wakitegemea vitu vya tofauti mpaka pale Mungu alipowasemesha jambo na kisha kuwaita kwenye maisha ya kiwango kikubwa “Zitafakarini njia zenu”.

Huu ni mwito wa moyo wangu na kilio cha moyo wangu kwa Mungu kwa muda mrefu kwaajili ya taifa la Tanzania na vijana wa taifa hili kwenye maisha yao binafsi na maisha ya kijumuiya. Unapoendelea kujifunza katika mfululizo huu, zitafakari njia zako!

Hazina ya kukumbuka kutoka kwenye mfululizo uliopita:
“Lengo”  si kuwa na malengo bali kuwa na matokeo

Kabla hujachukua hatua ya kuanza sasa kuweka mafundisho haya kwenye matendo, ninapenda nisisitize jambo moja kwako ambalo linaweza kuwa mtego kwako.

Watu wengi baada ya kuwa wamejifunza huelekeza akili na mawazo yao kwenye shughuli nzima ya kuweka malengo na kujisahau kabisa kuhusu usuri (essence) ya mchakato wa uwekaji malengo.

Kwahiyo utakutana na watu ambao wanazungumza na kujivunia kabisa malengo! Kwa mfano, mtu anaweza kusema “nimeweza kuhubiri kwenye wilaya 4 za Tanzania.” Au utakuta mwingine anajaivunia kabisa “oooh, mwaka huu nimeandika na kuchapisha kitabu kimoja.”

Ni sawa, ni mambo mazuri lakini hayo yote si “malengo” ya malengo yako! Sidhani kama unaoujasiri wa kuweka lengo ili ulifikie tu; sidhani kama ni furaha yako kukamilisha ratiba na kukamilisha shughuli fulani iliyo ndani ya malengo – sidhani!

Najua nyuma ya kila lengo kuna matokeo ambayo yamekusudiwa. Ndiyo kusema lengo la kuweka malengo au usuri wa malengo ni kuzalisha matokeo yaliyokusidiwa, kwa mantiki hiyo basi malengo ni nyenzo kukupeleka kwenye matokeo hayo. Kama una lengo lakini halikufikishi kwenye matokeo yako…. Ni heri kabisa ukachagua kufanya jambo jingine!

Ni heri kutokuwa na malengo kuliko kuwa na malengo yasiyokufikisha kwenye mwisho wowote yatakapokuwa yamekamilishwa! Mungu akupe hekima ya kunia kuwa na matokeo, kuzaa matunda, kuona mabadiliko na kisha malengo yakusaidie kuelekea huko!
 
 Somo hili litaendelea Jumatatu Ijayo
  
Mafundisho haya yameandaliwa na James Kalekwa
Mwanataaluma, Mwandishi wa vitabu na Mwalimu wa Neno la Mungu
+255 714 762 669
+255 754 917 764

Mwimbaji Jimmy Gait akana shutma dhidi yake juu ya Video yake mpya.

544714_334676729923469_868042671_n
Jimmy Gait
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili kutoka Nchini Kenya jimmy Gait amekataa kuomba radhi kwa kutoa Video yake Mpya ijulikanayo kama "Makekes" aliyomshirikisha Papaa Dennis. Hatua hiyo imekuja baada ya baadhi ya Watangazaji na Madj kukataa kucheza wimbo wake kwenye Vituo mbalimbali kwa Madai kuwa hawajapendezwa na Mavazi ya Wadada kwenye video hiyo na pia Wimbo huo una ujumbe mdogo sana.

Akijibu Madai hayo Jimmy Gait amesema kuwa haoni umuhimu wa kuomba radhi kwani anaamini hakuna jambo baya katika Video hiyo na kuwa hayo ni mapinduzi katika Muziki wa Injili, kwahiyo hakuna alichokosea.

Video hiyo iliyotengenezwa Nchini Afrika Kusini chini ya kampuni kubwa ya Godfather Production, imegharimu Ksh. Million 1.

Tazama Video hiyo