Advertise Here

Showing posts with label Waimbaji. Show all posts
Showing posts with label Waimbaji. Show all posts

Friday, May 31, 2013

Mfahamu kiundani Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Sam Batenzi.

SAM 1
Samwel Batenzi maarufu sana kwa jina la Sam Batenzi, ni Mwimbaji Chipukizi wa Nyimbo za Injili anayekuja kwa kasi ya Ajabu katika tasnia ya Muziki wa Injili Tanzania, kutokana na Uimbaji wake un avyowabariki watu wa Mungu. Kwa mara ya Kwanza, nilikutana na Sam Jijini Mwanza katika kituo cha Kazi yaani HHC ALIVE FM (91.9Mhz), na ndipo hapo nilipopata shauku ya Kumfahamu zaidi.

HISTORIA YAKE KIMAISHA
Sam alizaliwa miaka 25 iliyopita katika Mkoa wa Mwanza, katika familia ya kikuhani ya Bishop David Batenzi na Mama Batenzi. Sam ni mtoto wa 3 kati ya watoto 4 wa Askofu Batenzi, na kabila lake ni Mnyamwezi kwa Upande wa Baba, na Msukuma kwa Upande wa Mama.
 

                            HISTORIA YAKE KIMUZIKI
Sam alianza kujishughulisha na Maswala ya Kimuziki Mwaka 2000, lakini katika kujifunza vyombo vya Muziki huko Mkoani Mwanza. Na alianza rasmi uimbaji Mwaka 2004 huko Tabora katika shule moja iliyojulikana kama Umoja Secondary School.

Nilipotaka kufahamu ni Kwanini aliamua kuimba Muziki wa Injili na Si aina Nyingine ya Muziki, Sam alisema; “Nimeamua kumtumikia Mungu katika Uimbaji wa Muziki wa Injili kwa sababu Muziki wa Injili ndio muziki ambao umekuwa ukigusa maisha yangu kwa aina moja au nyingine, lakini naweza sema pia nilizaliwa katika familia ya kikristo na kukulia katika Malezi ya Kikristo.Na pia nilipompokea kristo kama mwokozi wa maisha yangu, ndipo nilipogundua nini Mungu amenizawadia, nami nikatumia zawadi hiyo kufanya kazi yake.”
 

Vipi kuhusu vikundi/kwaya ambazo Sam ameimbia?
Hapa Sam anasema; “Nilipokuwa shule niliimbia kikundi kimoja kilijulikana kama LPP (Long Pray Praise) ambacho naweza sema ndo waliendeleza kile Mungu ameweka ndani yangu, lakina pia nimewahi imbia Dar es Salaam Gospel Choir DGC ya Dar, na nimewahi kuwa member kwa muda katika kundi moja la kusifu na kuabudu linajulikana kama New Wine la Dar.
 


Nini ambacho Sam anafanya kwa Sasa?
“Kwasasa nimekuwa nafanya kazi za Uimbaji na vikundi ambavyo vimekuwa vinatengenezwa kwa muda kwa ajili ya kazi fulani tu baadae kinaisha baada ya hiyo kazi.
Kuhusu aina ya Muziki ambao Sam anaupenda sana ni African Music kama Zouk,Rhumba,Qwato,Sebene,Tradition music, lakini pia napenda pia Black Gospel,Jazz,RnB,Soul, na Soft rock.

Ni Mwimbaji gani wa Gospel unaempenda zaidi kwa Hapa Nyumbani?
“Mwimbaji wa Gospel kwa hapa nyumbani naweza sema Jackson Benty, Minza na John Lisu zaidi ya hapo labda vikundi kama Next Level, Sowers, Holy of Holies, Calvary Band, UGM. Ila napenda zaidi makundi.

Vipi ulishawahi kurekodi Wimbo wowote?
“Nilipoanza muziki tulirekodi na hilo kundi ambalo nilijiunga nalo la LPP, mbali ya hapo nimekuwa nafanya na watu tu, ila ndo nimeanza taratibu za kuandaa album yangu ya kwanza maana sikupenda sana muziki wa kurekodi studio. Napenda sana muziki wa live, na hata kama ni kurekodi iwe live on stage maana naamini ndo unakuwa na mguso wa aina yake na kuwa karibu na Mungu at a particular time”

Mbali ya Uimbaji, ni Kazi gani Nyingine unayojishughulisha nayo?
“Mbali ya Uimbaji, nafanya kazi ya Video Shooting pamoja na Editing. Maana nda Taaluma yangu hiyo.”
 

Vipi umeshajiunga na Chama cha Waimbaji wa Nyimbo za Injili?
“Kiukweli bado sijajiunga na chama cha waimbaji, maana sikuwa asilimia zote kwa muziki maana nimekuwa na shughuli zingine hasa za kimasomo labda kwa sasa ndo naweza kuanza taratibu za kujiunga.”
 

Ni aina gani ya Muziki unaofanya?
“Mimi nafanya muziki wa asili ya kiafrika ambao nimeupa jina la African Christian Soul (Afrocso), na hii ni kutokana na kugundua sisi Tanzania tumebarikiwa na miziki mbalimbali ya asili ambayo ikifanyiwa kazi, inakuwa mizuri sana badala ya kuanza kucopy nchi za magharibi. Kkwahiyo huo ndo aina ya muziki ambao mimi naimba katika kumtukuza Mungu.”

Ni vyombo gani vya Muziki unavyoweza kupiga?
“Napiga vyombo mbali kama bass guitar, acoustic guitar, kinanda, solo guitar na drums kidogo, ila zaidi chombo changu ni Bass guitar.”
 

Nini Malengo yako ya Baadae?
“Malengo yangu ni kumtukuza Mungu katika anga za kimataifa, na kundi ambalo nililianzisha mwaka jana kwa jina la “The Psalmists” ambalo hadi sasa tumeshafanya matamsaha mawili moja lilifanyika Dar 9 – 1 – 2011 katika kanisa la FPCT Kurasini, na la pili Mwanza 8 – 1- 2012 katika kanisa la FPCT kitangiri pia naanda matamasha mengi zaidi ambayo sasa hivi yatakuwa na muziki wa asili zaidi ili ku’promote such kind of music which is much blesses much”

Sasa sikiliza Mahojiano aliyoyafanya Sam Batenzi na Radio France International, April 13, 2013 akiwa na Mwimbaji wa Nyimbo za Injili toka Congo, Nyumba ya Mungu.

Wednesday, May 15, 2013

Album mpya ya Goodluck Gozbert kuingia Sokoni Mwezi Huu.

Goodluck Gozbert
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili toka Jijini Mwanza, ambaye pia ni Mtayarishaji wa Muziki, Goodluck Gozbert anategemea kuingiza sokoni album yake mwezi huu, Album hiyo itakuwa na jumla ya Nyimbo 8, ambazo ni 1.Nimeuona,2.Uko Sawa, 3.Wa Moyo 4.Nimwabudu nani, 5.Shika sana 6.Mpaka Lini 7.Umetamalaki 8.Atoshekaye.

 Kaa Mkao wa kupokea kitu kipyaaa toka kwa Mwimbaji huyu. Sikiliza wimbo wake huu

Mawasiliano ya Goodluck Gozbert
0762486168

Tuesday, May 7, 2013

Hongera Boniphace Magupa na Jessica Honore kwa kufunga ndoa.

Juzi ilikuwa ni Siku ya Furaha kwa Wanandoa hawa wapya Boniphace Magupa ambaye ni Mtangazaji wa kituo cha luninga cha Chanel 10 na Jessica Honore ambaye ni Mwimbaji wa Nyimbo za Injili.

Harusi hii ilifungwa katika Kanisa la Anglikani mkoani Shinyanga, na kufuatiwa na tafrija fupi nyumbani kwa akina Boniphace Magupa maeneo ya Ndala, Shinyanga kabla ya kuelekea Ukumbi wa NSSF kwa ajili ya kuwapongeza Maharusi hawa.

Shughuli hiyo ilihudhuriwa na watu mbalimbali kutoka mikoa mbalimbali Tanzania.
 Mtandao huu, unawatakia Maharusi hawa Maisha mema na yenye Furaha tele.

Thursday, April 25, 2013

Christina Shusho, Upendo Nkone kushiriki International Gospel Music Festival 2013.

Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Tanzania Christina Shusho anatarajia kushiriki Tamasha la The International Gospel Music festival kwa Mwaka 2013, lililoandaliwa na Kanisa la All Nation Break Through lililoko lililoko Columbus, Ohio, USA chini ya Watumishi wa Mungu Pastor Donnis & Nnunu Nkone.

Waimbaji wengine watakaoshiriki ni pamoja na Upendo Nkone, Pastor Daniel Kiza na Wengine wengi watakaoendelea kutangazwa siku chache zijazo. Taarifa zaidi kuhusu Muda na Sehemu zitatolewa hivi karibuni.

Tuesday, April 23, 2013

Historia ya Mwimbaji Sifa John.

Jina langu ni Sifa John. Nilizaliwa katika familia ya kiislamu na ni mtoto wa tano kuzaliwa ila kwa upande wa mama mimi ni mtoto wa pili, na wa kwanza alifariki ambaye alikua anaitwa Mwamvita. Nikiwa muislam nilikua naitwa Tiba Hamadi na baada ya kuokoka siku ambayo nilibatizwa ndipo nikapewa jina la Sifa, na baada ya kuolewa nikawa naitwa Sifa John(John ni Jina la Mume wangu). Baba yangu alitengana na mama yangu baada ya mama kurudi kwenye dini yake awali ya kikristo alikotokea kabla ya kuslim na kuolewa na baba. Baada ya mama kuondoka, baba yangu alioa mke mwengine na ambaye ndiye aliendelea kunilea baada ya kuachwa na mama.

Nilikaa kwa baba yangu mda mrefu bila kumjua mamaangu kwa sababu aliniacha nikiwa mdogo sana mana nilikua na miaka miwili tu, na baada ya kufikisha miaka kumi na nne nilikutana na mkutano wa injili hivyo nikaokoka kupitia mkutano huo. Ugomvi wangu na babaangu mzazi ulianzia hapo. Baba alikasirika sana na akanitenga kabisa na akakataa kuniendeleza kimasomo, na aliniambia hata akifa nisifike na mimi nikifa hatofika kwenye Mazishi. Lakini pamoja na yote baba yangu ananipenda sanaaaaana. na niliwahi kupata ajali ya mguu, mfupa ukakatika mara mbili na kupishana ikawa kwamba nikatwe mguu. Baba yangu alikua analia sanaaa kila akija hospitali.

Madaktari walikua wakimtoa nje mara kwa mara kwajili ya kulia, lakini alipambana kiume na kukwangua acount yake yote ili mimi nisikatwe mguu, mana aliambiwa kwamba ili nipone dawa inatakiwa iagizwe Ufaransa. Baba hakusita juu ya hilo kwani dawa iliagizwa hivyo nikatibiwa mpaka sasa nina miguu yote miwili. Hii yote ni kwaajili ya upendo wa baba yangu, hata mimi nampenda sanaaa baba yangu, lakini ninachomshukuru Mungu baba yangu amerejeza Moyo na sasa tunaishi nae kwa upendo sanaaa.

HISTORIA YAKE KIUIMBAJI
Nilianza huduma ya uimbaji Mwaka 1983 katika kwaya moja ya kanisa la Mchungaji Lukindo Kawe, na wakati huo nilikua nasoma Shule ya Msingi Kawe darasa la 4. Badae niliimba kwaya ya Yerusalem ya kanisa la Pentecoste Kawe-Mbezi kwa Mchungaji Kibingu Marandura ambae kwa sasa ni marehemu.Nipoolewa nilianza kuimba kwaya ya kanisa la EAGT Imani Choir ambayo ilikua chini ya kanisa la Mch. Ernesti Nyanda aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, na hapo nilikua Sololist niliyevuma sana na wimbo wa Kigeugeu. Hiyo ilikuwa ni katika mkoa wa Mwanza.

Badae nilichukuliwa na Kwaya ya Calvary EAGT Nyamanoro kwa Mch Kapera nikiwa Sololist na nilivuma sana kwa wimbo wa Malaika katika Kanisa la Efeso. Hapo sasa nilipata mtu mmoja anaitwa Gahutu akanidhamini nikatoa Album yangu ya kwanza ya Wateule Tutakwenda. Kwa sasa nimetoa album yangu ya pili ujulikanayo kama Usililie Moyoni Yupo Mungu.
Namshukuru sana Mungu ananipigania sana katika huduma hii mana nimekuwa nikisafiri huku na huko kwa ajili ya huduma na ananilinda sana. Pia kupitia huduma ya uimbaji nimefanikiwa kuanzisha huduma ya kusaidia watoto yatima na watoto waishio katika mazingira magumu. Pia ninao vijana ambao walikua wamekata tamaa tunaowapa mafunzo mbali mbali kama kushona, uigizaji, na computer.

Watoto hao nilionao wanapata misaada mbali mbali kama vile elimu mana kuna walimu wanawafundisha hapo kituoni mana walikua hawajawahi kusoma kwajili ya matatizo na shida walizonazo na kukosa msaada.
Pia namshukuru sana Mungu kwa sasa amenifanikisha nimefungua studio ya kushoot video pamoja na kupiga picha aina zote. Ofisi yetu iko Bunju B, hapahapa jirani na ofisi yangu ya Sifa Group Foundation, yote hii ili kupata pesa za kunisaidia katika uendeshaji wa kituo hiki. Soma Zaidi kuhusu Sifa Group Foundation Hapa.

Kwasasa vijana wangu wa upende wa maigizo wako location wanashoot movie iitwayo NO LOVE. Pia watoto hao wamepata mwalimu wa kuendeleza vipaji vyao. Kwa upande wa huduma yangu ya uimbaji tayari nimeanza kuandaa nyimbo mpya mbazo nitazitoa mwaka huu. Sitoacha kumtumikia Mungu kwa huduma hii mana alikonitoa ni mbali sanaaa.
Pia naomba mtu yeyote ambae ataguswa kuniwezesha katika huduma zangu hizi aniwezeshe mana nahitaji msaada sanaaa, hasa katika kituo cha watoto hao yatima na wale wa mazingira magumu.

Mungu akubariki sana wewe utakayewaza Kunisidia!

Mwalimu na Mwimbaji John Shabani atunukiwa Shahada.

Mwl. John Shabani akipokea Cheti chake
Mchungaji mtarajiwa John Shabani (kushoto) amekabidhiwa shahada yake na Askofu Kitonga (Kiongozi wa Makanisa ya Redeemed duniani), baada ya kuhitimu Mafunzo katika chuo cha kimataifa cha huduma (International School of Ministry - ISOM) chenye makao makuu New York Marekani.

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa Mwalimu huyo wa muziki wa injili Afrika mashariki bwana John Shabani, baada ya kuhitimu mafunzo yake hayo kwenye chuo hicho cha kimataifa. John ambaye amekuwa na ndoto za kujiendeleza sana katika elimu mbalimbali, amekuwa miongoni mwa wanafunzi waliofanya vizuri katika chuo hicho.
Mchungaji huyo mtarajiwa anategemea kujiunga na chuo kimoja huko marekani ili kuendelea zaidi na masomo yake, pia amewahasa waimbaji wenzake wa injili kuwa na mpango wa kujiendeleza ki-elimu.

Mahafali hayo yamefanyika jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ki-dini na serikali. Makao makuu ya chuo yaliwakilishwa na Dr. Lee kutoka Marekani.

CHANZO: Tanzania Daily Eye

Thursday, April 18, 2013

Historia ya Mwimbaji Ephraim Sekeleti.

Ephraim Sekeleti Mutalange ni muimbaji maarufu wa nyimbo za Injili nchini Zambia, alizaliwa Mwaka 1983 katika mji wa Kalulushi nchini Zambia. Alimaliza elimu yake ya sekondari katika shule ya Kalulushi mwaka 2001.Ephraim ni mtoto wa pili toka mwisho kati ya watoto sita, aliingia kwenye muziki wa injili tangu akiwa kinda huku alifundishwa kupiga kinanda na mmishonari alipokuwa bado mdogo. Mama yake anasema  “ Ephraim alikuwa ni mtoto aliyekuwa wa kelele nyingi”.

Yeye pamoja na dada zake waliimba kanisani wakitumia kinanda na huko alipata uzoefu katika uimbaji na upigaji wa kinanda. Baadaye alijiendeleza katika uimbaji kwenye kikundi kilichojulikana kwa jina la  “Virtue for Christ” na aliimba katika kikundi hicho kwa muda wa miaka miwili.
 
Mwaka 2002 akiwa na kiu ya kurekodi album yake, Aliamua kujitoa muhanga kwenda Afrika ya Kusini kwa kutumia kiasi kidogo tu cha pesa alichokuwa nacho, nia ilikua ni kurekodi album yake ya kwanza. Pamoja na jitihada hizo, baada ya kufika nchini Afrika ya Kusini alijikuta anaweza kurekodi nyimbo mbili tu kati ya album nzima. 

Hivyo akaamua kujiingiza katika Theater ya Pretoria na ndipo akapata fursa ya kuimba mbele ya Rais wa Afrika ya Kusini. Nafasi nyingi ziliendelea kujitokeza zilizomsababishia kutaka kuacha kuendelea na muziki wa injili ili aimbe miziki ya kidunia, lakini akawa muaminifu kuendelea na uimbaji wa injili. Mlango ulifunguka kumruhusu kurekodi album ya kwanza iitwayo Temba Baby“(Mtoto wa Miujiza)”.

Baada ya kurekodi, na kuuza nakala za kutosha za album hiyo ya Temba boy, kwa mafanikio ya hiyo kazi Ephraim aliamua kurudi nyumbani kuwekeza ile fedha. aliona awekeze zaidi kwenye ya album yake ya pili iliyopata mafanikio makubwa iliyoitwa Limo Ndanaka. Hi album imefanya vizuri kwenye chati mbalibali za muziki wa injili. Ephraim akiwa nje ya Zambia ameimba katika nchi mbali mbali zikiwemo Namibia, Afrika ya Kusini, Tanzania, Zimbawe na Australia.

Alisema anafurahi akiona watu wasiokuwa na tumaina la Kristo wakianza kuwa na matumain, Licha ya kufanya muziki wake nchini Zambia amewahi kuja nchini Tanzania na kurekodi album yake nzima kwa Lugha ya Kiswahili. Moja kati ya Nyimbo zake zinazotamba hapa nchini ni pamoja na;
                                             1. Uniongoze                                 
                                             2. Baraka Zako
                                             3. Huu Mwaka 
 
Ephraim hajui Kiswahili fasaha na nyimbo zake hizo alifundishwa kuziimba kwa lugha ya Kiswahili na Mchungaji ambaye pia ni muimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Tanzania Ency Mwalukasa. Ephraim amesema ataendelea kuhubiri kwa njia ya uimbaji kwa sababu imempa changamoto zilizomuinua. Licha ya uimbaji Ephraim amefunga ndoa na Faith Chelishe na wamejaliwa kupata mtoto mmoja wa kike.Imeandaliwa Na; Victor Nivox

Thursday, April 11, 2013

Spacio: Mwimbaji wa Nyimbo za Injili aliyeishi na Jini Mahaba kwa Miaka 17.

Kwa jina naitwa Spacio Abubakary Ngalla, nimezaliwa na kukulia Dar es salaam, Sinza. Na ni mtoto wa 3 katika familia ya kiislamu.

Kiukweli mimi nilikuwa mmoja wa watu ambao hawakutaka kusikia Jina la YESU na nilikuwa siamini miujiza yeyote na kuona ni mazingaombo tu wachungaji wanafanya kuwateka watu akili. Ila hadi siku ambayo mungu aliponionesha njia ya uzima na kuniponya tatizo lililonisumbua mda mrefu, ndipo nikaamini uwepo wa UKRISTO

NILIVYOKUTANA NA JINI MAHABA
Nakumbuka ilikuwa mwaka 1996, nikiwa na miaka 7, Mimi na marafiki zangu tulikuwa na tabia ya kwenda kuogelea coco beach siku za weekend, siku moja baada ya kumaliza kazi zangu za nyumbani majira ya saa 6 hivi nikaenda kuwapitia marafiki zangu (4) ili twende beach kuogelea ikifika jioni turudi nyumbani. Tulipofika beach watu walikuwa ni wengi sana kila mmoja alikuwa yupo busy na yake, sisi tulijigawa wengine walienda kuogelea sehemu nyingine, mimi na mwenzangu Ali tulibaki upande wa mwanzoni kwa kuwa hatukuwa tunajua kuogelea vizuri.

Majira ya saa 10, hivi nikiwa na Ali, nilisikia harufu nzuri kweli ikiwa inavuma kuja kwetu, ambayo siku wahi kuisikia kabla, ni nzuri kwa kweli, nikamuuliza Ali “unaisikia harufu hii?” yeye akajibu ndio ninaisikia ila sijui inatoka wapi!

Baada ya dakika kadhaa nilisikia sauti ya kike ikinisalimia “hujambo?” nikashtuka, kugeuka nyuma nikakutana na msichana sijui nimuelezeeje, ni mweupe kiasi, ana nywele ndefu, sura yake ipo serious na ukiiangalia tena ni kama anatabasamu, macho yake ni ang’avu, ni mzuri kiufupi akiwa amevaa nguo za kawaida tu ila kichwani amejitanda baibui. Aliniambia jina anaitwa MAIMUNA!

Mwili uninisisimka huku kidogo nikiwa na natetemeka japo sikutaka kumuonesha kwa kuwa hilo jina halikuwa geni kwangu, cha ajabu kadri alivyokuwa anaongea na mimi uoga ulizidi kunipungua hadi nikawa najiskia kawada na kucheka pamoja. Aliomba tuogelee wote nikamwambia, mimi siwezi kuogolea vizuri, akaniambia “Usiwe na wasi wasi nitakufundisha usijali” basi akaanza kunishika mikono na kuanza kunivuta ili niweze kujifunza kupiga mbizi taratibu. Siku hiyo ilikuwa ni tofauti sana kwani tulifurahi sana.

Saa 12 na nusu jioni ilipofika tukaanza kujiandaa kwa safari, siku hiyo tulichelewa kweli kuondoka! Ghafla Maimuna nikawa simuoni, nikaita sana “Maimunaaaaa uko wapi sisi tunataka kuondokaaaaa!” Kimyaa! Basi  sisi tukaanza kuondoka pale beach, kuna sehemu huwa ina miti mingi sana na ni shortcut kwenda kituoni, kwa mchana ni salama lakini kama ni giza giza si pazuri huwa kunakuwa na wahuni. Sisi tukiwa tunakaribia hiyo njia roho ilisita kupita pale, kumbe nyuma kulikua na wahuni wakitufatilia. Na sisi tupo watato tu, wao walikuwa watatu.

Heee mara tukashangaa kundi la watu zaidi ya 15 nao wakawa wanapita hiyo hiyo njia, basi sisi tukaongozana nao hadi kupita ile njia salama, kushtuka tunajiona tupo wa tano tu mbele tunakajiuliza “wale watu wameenda wapi?” Wahuni kumbe walikimbia katikati! sasa hatukujua ni kwa kwa sababu gani. Ila mimi nikahisi kundi la watu wale hawakuwa watu bali ni majini ndo waliotusindikiza, nikawaambia wenzangu “jamani tukimbie wale ni majini” kwa sauti kubwa ya uoga”.


URAFIKI NA JINI MAIMUNA
Tukafika nyumbani kila mmoja hoi, mimi bado nilikuwa na mawazo ya yule msichana niliyekutana nae baharini. Usiku nikiwa ndotoni nilimuota akija kunitembelea nyumbani na kufurahi pamoja.

Hali ile iliendelea hadi nafika form 1, ambapo nilikuwa nasoma Azania Sec School, haipiti siku moja lazima niote tuko pamoja tunafurahi pamoja hadi nikazoea,

Mwaka 2004, Maimuna alijitokeza tena kwa mara ya pili nikiwa niko chumbani, niliogopa sana nilipiga kelele mama akaja Maimuna akaondoka. Mama alishushwa sana na hali hiyo akaniuliza tatizo ni nini lakini nikamwambia nilikuwa naota tu, niliogopa kusema kwa kuwa Maimuna aliniambia nisiseme chochote kuhusu yeye la sisivyo nitakiona cha moto.

Baada ya muda nikazoea, akija tunaongea tu vizuri na kazi zingine alikuwa ananisaidia kama kutengeneza computer za baba, alikuwa ananisaidia kama tatizo ni kubwa sana namwita kimoyo moyo anakuja ktk mwili wangu kisha naanza kutengeneza computer, watu wengi walinishangaa sana uwezo niliokuwa nao lakini kumbe walikuwa hawajui JINI ndie alikuwa mara nyingi ananifundisha usiku.

Alinipa hela nyingi tu kiasi kwamba nilikuwa naenda shule nikiwa elfu 50, laki, ILA ole wangu nitumie na mwanamke au nimnunulie mtu sigara, pombe, basi hela zote zinapotea na nitahangaika hata shilingi 100 sipati zaidi ya kupewa hela ya shule, na nitahangaika hadi basi.

KAMA kawaida ukisha fikia umri fulani lazima uanze utundu wa kufatilia wasichana, kuwapa hela au kuwanunulia zawadi hasa katika siku kuu vile au valentine day, mimi iliponza sana hiyo tabia, kwani niliteseka sana.Kwani maimuna alikuwa hapendi

Kitu kilichonifanya nitafute wasichana wengine ni kwamba Maimuna hakuwa anakuja kila wakati, ni mara moja tu kwa siku tena hasa usiku. Na pia ukiangalia hata nikija kukua yeye anabaki jini na mimi binadamu kwa hiyo si rahisi kuja kuishi pamoja.

ILA chochote kilichokuwa kibaya kwangu kilichotegeshwa kichawi hakikuweza kunipata na hata usiku wachawi hawakuweza kunifata fata, japo mwanzoni nilihangaika sana na wachawi kwani walikuwa wanatusumbua sana nyumbani, waganga walidai nyumba haikuwa na zindiko!

Kiukweli alinifundisha vitu vingi pamoja na uchoraji, utayarishaji muziki, computer ambavyo hadi sasa vinanisaidia ktk maisha yangu, baada ya kutoka darasani yeye hunifuata usiku na kunielekeza zaidi. MIAKA YOTE HIYO TULIISHI KAMA WACHUMBA.Mengine siwezi kuyataja lakini mtakuwa mshaelewa nini ninamaanisha.


UGOMVI NA JINI KUANZA
Mwaka 2009, nina miaka 20 nikiwa nafanya kazi Cellulant Tanzania, kuna dada mmoja alikosea namba na kupiga kwangu, alijitambulisha kwa jina anaiwa UPENDO, mara ndio ukawa mwanzo wa urafiki wetu ambae hadi sasa tunaishi pamoja tukijipanga kwa ajili ya kufunga ndoa. Nilitokea kumpenda sana dada huyo japo hatukuwa tumeonana, na hata yeye pia alitokea kupenda kuongea na mimi mda wote. Maimuna alikuwa hapendi tabia ya mimi kuongea na huyo dada na mara nyingi alikuwa ananionya sana, ila mimi ilikuwa vigumu mno kukubali kwani nilikuwa nimshapenda tayari.

Siku moja nikasema hataa lazima nionane na huyu dada, hadi lini tutaishia kuongea kwa simu tu. Kwa mara ya kwanza kukutana na dada huyo, usiku wake sikulala! Nilipatwa na homa hadi asubuhi yake sikuweza kwenda kazini ikabidi nipumzike. Mara mwili unachoma, mara kifua kinanibana, mara kichwa kinaniuma, kikitulia nyama za mwili zinatikisika kama mtu anani vibrate vile.Niliteseka sana wiki nzima nilkuwa mgonjwa. Maimuna akaniambia hiyo ni bakora moja nimekupa, nataka uachane na UPENDO.

Baada ya kuseka sana kwa hali hiyo kwani mara kwa mara ilikuwa inanitokea, nikaanza kwenda kwa waganga kutafuta tiba ya kumuondoa jini huyo katika mwili wangu,kwani alikuwa kero kwangu, zaidi ya waganga 15 nilikwenda lakini bila mafanikio.


                                                    KUOKOKA KWANGU
Baada ya kuchoka kuvumilia nikamfuata rafiki yangu wa karibu Robert na kuanza kumueleza,  akaniambia kwanini usiende kuombewa, mbona wengi tu wanapona na hata mjomba wangu alikuwa anaumwa miguu alipoombea akapona. Nikamwambia sasa nikienda huko wazazi wangu waanifikiriaje? Akanijaza moyo na kunipa ujarisi kuwa “IMANI YAKO NA MUNGU SI YA WAZAZI WAKO BALI NI WEWE NA MUNGU WAKO NA HATA UKIFA UTAENDA NAO? SI WEWE NDIE UTAKAYE ENDA KUJIBU HUKO? FANYA MAAMUZI YALIYO SAHIHI”

Nikakubali! Basi nikasubiri jumapili ilipofika nikajiandaa na kwenda kanisani kuombewa, hakika nilipoombewa kila kitu kili badilika na kijisikia mwepesi kama vile nilikuwa nimebeba viroba vya michanga! Nilipoombewa nikadondoka chini na kupoteza fahamu. Baada ya dakika kadhaa nikaamka na kujikuta nikochini nimelala huku nikijishangaa nini kilichotokea.

Toka hapo nikaamini na nikaamua kuimba Nyimbo za Injili ili kueneza Neno la Mungu kwa wasiofahamu utamu wake.

Kwasasa nipo huru na ni kweli Yesu anatenda na Roho Mtakatifu yupo kwa ajili yako endapo utaamua kumpokea! Mungu ni mwema, Mungu anatenda. NAMSHUKURU KWA KUNIOKOA!

Saturday, March 23, 2013

Historia ya Mwimbaji Sipho Makhabane.

Sipho Makhabane
Sipho Makhabane, Mwimbaji mwenye jina kubwa barani Afrika, ambapo umaarufu wake umepatikana kutokana na uwezo wake wa kutunga nyimbo zenye ujumbe wa hali ya juu wa kumsifu na kumuabudu Mungu.

Kutokana na uwezo wake huo mashabiki wengi wa muziki wa Injili wamekuwa wakimfananisha na wanamuziki mahiri kama Joyous Celebration ama Sfiso Ncwane.
  Makhabane mwenye umri wa miaka 45 ni mmoja wa magwiji wa uimbaji nchini Afrika Kusini, na ameshiriki katika shughuli mbalimbali za kiroho na kijamii. 

Kutokana na kutingwa na shughuli zake mwaka 2010 alitangaza kuachana na kazi ya kuimba, hata hivyo mwaka 2012 aliushangaza ulimwengu kwa kuachia albamu yake mpya iliyokubalika na watu wengi.

Historia ya maisha yake inaonesha kuwa ni mtu aliyekulia katika muziki huo, na kutokana na ugumu wa maisha uliokuwa ukiikabili familia yake, Makhabane alilazimika kuacha shule akiwa darasa la tano na akiamua kufanya kazi katika shamba la miwa la Kaaruls huko Mpumalanga kama ilivyokuwa kwa mwimbaji mwingine nguli Rebecca Malope.
  Makhabane alifanya hivyo walau aweze kupata fedha ya kuwasaidia wazazi wake pamoja na ndugu zake ambao walikuwa wakimtegemea yeye.

 Alipotimiza  miaka 17, alihamia kwenye kazi za ujenzi kwenye Hifadhi ya Taifa ya Afrika Kusini ya Kruger.

Akiwa huko alifanya kazi ya kuwasaidia mafundi waliokuwa wakijenga nyumba kambini hapo na alipotimiza miaka 21 alikuwa tayari na ujuzi wa kutosha katika kazi ya ujenzi na akapata kazi katika eneo la Pienaar.

Mwaka 1986, Makhabane alipata ofa nzuri katika kampuni ya Telkom kama fundi, lakini katika kuhangaika kwake alijikuta akiishia kwenye muziki wa Injili.

Hata hivyo hakuwa akijua kuwa nyota ya mafanikio yake ilikuwa kwenye huduma hiyo ya uimbaji na badala yake alikuwa akifanya muziki wa kujifurahisha zaidi na si wa biashara.

Mwaka 1990, wakati huo akiwa na umri wa miaka 25, Makhabane alifunga ndoa na binti aliyekuwa na umri wa miaka 18.

Baada ya hapo ndipo alianza kazi ya kununua na kuuza kazi za muziki ndani na nje ya nchi ya Afrika Kusini.

Kutokana na kuona muziki umeanza kuingia kwa kasi kwenye akili yake, Makhabane aliamua kuachana na kazi ya ufundi mitambo ya simu na kujikita kwenye muziki.

Katika kuhakikisha anapunguza wizi wa kazi zake, mwanamuziki huyo aliamua kusambaza kazi zake mwenyewe, lakini kikwazo kwake kikawa ni namna ya kuwavutia wasambazaji waliokuwa tayari kununua kazi kutoka kwake.

Kazi yake iliyomfanya kukubalika ilianza kusikika kwenye redio ya Swazi ambayo inajulikana zaidi kwa jina la Ligwalagwala FM, ambapo kibao kilichomtambulisha ni kile cha Ngitinikela Kuwe.
Hatimaye mwaka 1996, Makhabane aliamua rasmi kuifanya kazi hiyo ya muziki wa Injili na kuacha kazi aliyokuwa akiifanya kwenye kampuni ya simu.

 Mwaka huo huo aliachia album yake iitwayo “Yek’intokozo” wimbo ambao mpaka leo unakumbukwa na mashabiki wake kwani ndio ulimtambulisha vema, ingawa tayari alishatoa album nyingine mbili miaka ya 1993 hadi 1999 za ‘Thum'umlolo” na “Jesu Uliqhawe”. 

Mwaka 1998, kupitia kampuni ya CCP Records aliachia album yake ya nne iitwayo “Uyigugu” iliyofanya vema kabla ya mwaka uliofuata kuachia nyingine iitwayo “Makadunyiswe,”. 

Mwaka 2001, alifyatua album ya Calvary ambayo iliuza kufikia kiwango cha juu na mwaka uliofuata (2002), aliachia albamu  nyingine ya ‘Akukhalwa’ ambayo ilitikisa kama album ya “Yek’intokozo,” akiuza zaidi ya nakala 70,000.

Mwaka 2003, Makhabane aliachia album ya ‘Moya wami’ ambayo pia iliuza zaidi ya nakala 70,000. 

Kutokana na umahiri wake, Makhabane ameweza kushirikishwa katika album na waimbaji wakongwe wa nchini kwake kama Jabu Hlongwane, Marehemu Vuyo Mokoena, Lundi, Hlengiwe Mhlaba na wengine wengi. 

Pia akiwa nyuma ya mafanikio ya waimbaji lukuki kama Hlengiwe Mhlaba, Ncandweni Christ Ambassadors, Shongwe na Khuphuka Saved Group. 

Nje ya uimbaji, Makhabane ni mtayarishaji wa kazi za muziki wa injili akiwa daraja la waimbaji wengine kutokana na kuwika vilivyo kupitia kazi zao zilizoandaliwa na gwiji huyo.
 
Sipho Makhabane ni mmoja kati ya Waimbaji watakaohudumu siku ya Tamasha la Pasaka la Mwaka huu litakalofanyika Uwanja wa Taifa.

Saturday, March 16, 2013

Mfahamu kiundani Jessica Honore na The Jessica's Music.

Jessica Honore
Jessica Honore ambaye ni Mtoto wa 6 na wa mwisho kuzaliwa katika familia ya kitumishi amerithi kipaji cha uimbaji toka kwa wazazi wake, kaka pamoja na dada zake. Watoto wa familia yao wengi wamekuwa ni waimbaj na wapiga vyombo vya Muziki.

Jessica alianza uimbaji akiwa na umri wa miaka 6. Alikua akiimba kwaya ya watoto Kijitonyama Pentecoste, na baadae Mwananyamala Pentecoste. Huko ndiko alikokukuzia huduma iliyokua ndani yake. Mnamo Mwaka 2005 akiwa darasa la 7 Jeesica akasikia habari za mashindano ya Uimbaji(Gospel Star Search).
Jessica akiwa na baadhi ya Washiriki wa Gosprl Star Search ya Mwaka 2005
Jessica anasema "Wakati huo sikuwa katika mazingira ya kuniruhusu kushiriki shindano hilo, ila kwa msukumo uliokuwa ndani yangu juu ya uimbaji na kwa ruhusa na ushirikiano wa Mama yangu, niliweza kwenda katika usahili na kushiriki shindano hilo. Baada ya mchakato mrefu sana, ulio jumusha washiriki toka mikoa mingine ya tanzania kama mitatu hivi, ndipo nikafanikiwa kuibuka mshindi."

"Hapo ndipo nilipoanza safari rasmi ya uimbaji. Nilifanikiwa kupata gari na kusomeshwa elimu ya sekondari mpaka kidato cha 4 kupitia Ushindi ule chini ja usimamizi wa Walezi Ruge Mutahaba na Michael Nkya. Pia Mwaka huo huo wa 2005 nikafanikiwa kutoa track yangu ya kwanza iliyojulikana kama "Mungu Yupo" na ikafanya vyema katika vyombo mbalimbali vya habari, ingawa bado sikuwa tayari kuingia deep kwenye maswala ya Muziki kwani nilikuwa bado ni Mwanafunzi na nilikua chini ya uongozi ambao haukuhitaji kunipeleka puta, maana waliona nahitaji kukua kiuimbaji, kielimu na kiakili." Aliongeza Jessica.
Jessica akiwa Studio
Baadaye akafanikiwa kutoa nyimbo nyingi sana akiwa bado anasoma, chini ya usimamizi wa Mlezi wake Rugemalila. Baadhi ya Nyimbo hizo ni kama Sitaogopa, Mtumikie, Sifuni, Sitahofu na nyingine nyingi ila hakutengeneza album. Mnamo Mwaka 2010 baada ya kumaliza shule Jessica alifanikiwa kutengeneza album ya Tenzi za Rohoni, ila kwa sababu mbalimbali haikuweza kutoka.

Baada ya kumaliza kidato cha 4, Jessica alitamani sana kwenda shule ya Uandishi wa Habari(School of Journalisim) ila haikuwezekana kwa kipindi hicho na ndipo akaanza rasmi kazi ya Muziki. Wakati huo alianza kwa kufanya Matangazo mbalimbali na Jingles pia hasa za Clouds Fm, na zikapendwa sana na watu. Pia alifanya Matangazo ya Kampuni za simu kama Vodacom na Zantel.
Jessica akiwa katika Utengenezaji wa Video yake ya Napokea
Jessica anasema " Pia nimekuwa nikiitwa kwenye hafla mbalimbali kuhudumu kama Harusi, Misiba na Sherehe mbalimbali huku nikitumia Keyboard pamoja na Mpigaj aitwae Isaya, na kwahiyo niliweza endesha Maisha yangu vyema. Nilipendelea pia maswala ya Modeling na Designing na Wakati mwingine nimekuwa nikichora designs za nguo kwa mitindo mbalimbali."

Jessica alianza jitegemea mwaka 2010, na Mwaka 2011 Emmanuel Mabisa alimfuata na kumshirikisha swala la Glorious Celebration. Jessica anasema, "Sikusita maana nilikuwa napenda sana kushirikiana na waimbaji wengine ila ilikuwa ni kwa makubaliano ya kua nitapotaka anza rasmi simamia maono yangu nitatoka Glorious Celebration na kuanza simamia kitu kilicho ndani yangu. Pia mwaka huo huo nikapata nafasi katika kanisa la Word Alive Center kwa kufundisha Praise Team na kuanza kusali pale baada ya kua Christ Embassy kwa miaka mitatu.
Jessica akiwa na Glorious Celebration
Mwaka jana(yaani 2012) Mwezi wa 5 au wa 6 alianza chukua hatua ya Maono yake huku akiendelea shughurikia album yake aliyokua ameitelekeza kwa muda mrefu. Jessica anasema ilikua ni changamoto maana alikuja gundua kuwa alikua akua kiuimbaji hivyo ikabidi aanze kuziimba upya Nyimbo za kwenye Album hiyo. Jessica anaendelea kusema kuwa amekuwa na maono ya muda mredu ya kua na team maalum ya kuhudumu nayo mahali mbalimbali kwa kufanya Live Music, kuwa na shule ya Muziki, pamoja na eneo ambalo watu wanaweza kuwa wakilitumia katika Kusifu na Kuabudu yaani Cathedral of Worship.
Jessica katika pozi
"Pia napenda kuwa na studio kubwa ya muziki na kwa kutambua hilo nikaanza kwa kujitoa kufundisha watu ambao wamekua wakihitaj msaada wangu. Mwaka jana mwishoni nilifanikiwa kuanzisha Team yangu kwa kupata mabinti walio kua na vipaji ila walihitaji uzoefu na mafunzo ya ziada ili kukua na kuimba vizuri. Hivyo nikawafundisha na pia nikawashirikisha baadhi ya wapigaji wa vyombo akiwemo kaka yangu wa kufuatana John na akakubali na kunisaidia kusimamisha maono yangu."

Mwaka jana mwishoni nikaanza kuhudumu na mabinti zangu na wakaka wawili niliowafundisha mwenyewe. Baada ya kuona tumefanya vizuri katika tamasha la Holy Bass Guitor lililofanyika pale DPC mwaka jana, nikaamua kuwa serious zaidi na kujikita kufanya huduma ikue. Kweli huduna ikaanza kukua, watu wa kufanya back up wakaanza ongezeka pamoja na wapiga vyombo maana wakati huo bado nilikua sijapata wapigaji maalum wa kuwa nao katika huduma. Ndipo nikawa na msukumo wa kufanya huduma hii kwa ukamilifu zaidi."
Jessica(aliyekaa) akiwa na baadhi ya waimbaji wake
"Baadaye nikapata msukumo wa kuandaa tamasha la uzinduzi wa album yangu ya kwanza ili kuelezea maono yangu na kutambulisha team yangu nitakayokuwa nikihudumu nayo kwa jina la THE JESSICA MUSIC. Na kwa mwaka huu nikaanza mikakati mingi kwa msaada wa Pastor mmoja toka Nchini Zambia Pastor John Mumba aliyeguswa na huduma yangu na kuamua kunisaidia kupanua ufahamu wangu kufikia ndoto zangu, na akawa bega kwa bega pamoja na Mume wangu mtarajiwa Boniphace Magupa mpaka kufikia hapa."
Jessica akiwa na Mume wake Mtarajiwa Boniphace Magupa
Kwa sasa The Jessica Music ina member wasiopungua 10 ikiwa ni waimbaji na wapiga vyombo. jessica anasema "Namshukuru Mungu kwa kuwa nao mana ni Baraka katika Maisha yangu na kwangu ni ushuhuda mkuu wa Mungu alikonitoa". Sasa The Jessica Music inaelekea katika tamasha la ZIMA UKIMYA NA JESSICA HONORE, Tamasha litakalofanyika pale City Christian Centre - Upanga Machi 24, Mwaka huu kuanzia Saa 9 Alasiri - Saa 1 Usiku. Kiingilio katika tamasha hilo kitakuwa ni Tshs. 15,000. USIKOSEEE!

Hii ni Video ya Wimbo wa Jessica Honore unaojulikana kama Napokea