Itakumbukwa kwamba, Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili iliyopita majira ya jioni aliadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano, Makao Makuu ya Jimbo kuu la Roma na kuanza utume wake rasmi kama Askofu wa Jimbo la Roma. Ibada hii ilihudhuriwa na umati mkubwa wa watu waliokuwa wamefurika ndani na nje.
Kama inavyoonekana kuwa ni sehemu ya utaratibu wake, Baba Mtakatifu Francisko huanza kwa kusalimiana na waamini na watu wenye mapenzi mema, ambao wamekuwa wakifurika katika matukio kama hawa tangu alipochaguliwa kuliongoza Kanisa. Huu ni upepo mpya wa imani na matumaini ndani ya Kanisa.