Advertise Here

Sunday, December 8, 2013

Mkutano wa Ufufuo na Uzima sasa kuhamia Morogoro.

Mch. Josephat Gwajima
Baada ya mikutano iliyovunja rekodi kwa idadi ya watu yaani Arusha, Moshi na Tanga; sasa kanisa la Ufufuo na Uzima linahamishia mikutano yake mkoani Morogoro ambapo Mchungaji Gwajima ambaye pia ni mchungaji kiongozi wa kanisa hilo anatarajiwa kuhubiri kwa siku nane mfululizo.

Pamoja Mchungaji Gwajima atafuatana na timi ya watendakazi zaidi ya mia tatu na waimbaji maarufu wa injili kama Flora Mbasha, John Lisu, Jackson Benty na Mwanamapinduzi Band.

Mkutano huo wa kwanza kufanyika Morogoro kwa kanisa la Ufufuo na Uzima unatarajiwa kushuhudia misukule wakirudi, wagonjwa kupona, viwete kutembea na mambo mengine mengi ya ajabu.

Usikose kuhudhuria na wewe ili kupokea muujiza wako.

- Ufufuo na Uzima -