Advertise Here

Thursday, February 28, 2013

Hatua za kwenda katika Hatua Nyingine, Kitabu kitakachobadili Mfumo wa Maisha yako.

WAKRISTO wengi wamekuwa hawaoni mabadiliko katika maisha yao, na mara nyingi wamekuwa wanataka kuombewa tu na watumishi wa Mungu lakini hawachukui hatua ya utendaji ili kufanya maombi hayo kuwa na majibu.
                
Kitabu hiki kimeeleza kiundani ngazi za kumuwezesha mtu yeyote kuweza kupata mabadiliko chanya katika maeneo yote kama kihuduma, kimasomo, mahusiano hadi ndoa, biashara, familia, kazi nk.
                
Lengo ni kufika HATUA NYINGINE, lakini mtu huwezi kufika juu kabla ya kuchukua hatua ndogo ndogo zitakazompeleka huko juu.
               
 Kuna hatua saba za kufika katika kusudi la Mungu katika maisha yako. Hatua ya kwanza ni Matarajio Mema na hatua ya mwisho ni Utendaji Bora. Pata nakala ya kitabu hiki ili uzifahamu hatua zote saba na ubadili maisha yako sasa.
            
           Kwa Dar es salaam kitabu kinapatikana maeneo yafuatayo: CCBC-Survey, Ubungo Bus Terminal, Efatha Bookshop (Mwenge), Tarakea Christian Bookshop(Mwenge), TPH bookshop(Samora Avenue), Sunlight Bookshop(DPC -Kinondoni), Canaaland Bookshop(Winners chapel G/Mboto), Mbogo Bookshop(Benjamini Mkapa High School, Kariakoo kwa Nyamoga ilipokuwa Ilala TAG, na Tegeta Kibaoni.

Kama uko nje ya Dar es salaam, piga simu namba zifuatazo: Dodoma - 0762 898546, Morogoro - 0653 358086, Mbeya - 0654779468, Arusha - Kimahama Bookshop, Moshi - 0712 849965, Mtwara - 0653 244848.

Kwa Mawasiliano zaidi, wasiliana na Mwandishi wa kitabu hiki Dr. Richard Z. Adam kwa namba zifuatazo: 0717 085810, 0758416940, 0782 085810.

Monday, February 25, 2013

Facebook na Watumishi wa Mungu leo.

Song Lyrics: Tshala - Joyous Celebration.

Song Name; Tshala
Song By; Siphumelele Mbambo
Album; Joyous 16
  
Tshala, tshala ngezinyembezi.
[Invest, invest with your tears]
Tshala, tshala ungakhathali.
[Invest, invest don't be tired]
Tshala, tshala Ngezinyembezi
INkos'iyezwa,iyabona.
[The Lord can hear and can see]

Uzovuna ngaphezu kokwazi
[You'll reap more than you know]
Uzothwala umqhele phakade
[You'll benefit for a lifetime]
Uzovuna ngaphezu kokwazi
Uzothwala umqhele phakade
Tshala Tshala Ngezinyembezi
INkos'iyezwa,iyabona.

Hlala hlala, hlal'eNkosini
[Dwell, Dwell in the Lord]
Hlala hlala ungakhathali
[Dwell, dwell and don't get tired]
Hlala hlala, hlal' ekholweni
[Stay, stay in faithfulness]
Nkos'iyezwa futhi iyabona

Uzovuna ngaphezu kokwazi
Uzothwala umqhele phakade
Hlala hlala, hlal' ekholweni
INkos' iyezwa iyabona

Hiki ndicho kilichotokea February 23, 1990.

Sunday, February 24, 2013

Joyce Meyer: How to study the Bible?


I've spent about 30 years studying God's Word, and it has totally changed my life. I thank God for what I know now, but it didn't come overnight. If you want to see areas of your life change, learn to truly study the Bible.

Why Should I Study the Bible?

The Bible is no ordinary book. The words within its pages are like medicine to your soul. It has the power to change your life because there is life in the Word! (See Hebrews 4:12.) And when you discover the power and truth of God’s Word, you will begin to see changes in your life that only this truth can bring. You will even learn how to recognize what the enemy tries to bring against you.

The good news is, it won’t take you 30 years to know what you need to know. Just begin where you are right now and determine to stick with it! Every time you study the Bible and pay attention to what you’re reading, you’re learning something.

Proverbs 4:20-22 says, “My son attend to my words…for they are life to those who find them…” The word “attend” means to pay attention to, give some time to something. To attend to the Word of God is a lot more than just reading; it’s meditating on it.

We need to get into agreement with what God wants us to do because, as the writer of Proverbs says, these words are life! When you need an encouraging word, or you’re in a negative environment, it’s good to know that you can find life (plus healing and health) in God’s Word.

What Do I Study?

There’s really no wrong place to start.  You can study anything that’s going to help you. If you’re dealing with anger or fear, flip to the back of your Bible’s concordance and locate those words to see which scriptures talk about those things.
If you can’t think of anything right away, thumb through the concordance in the back of your Bible and pick one of the words. Begin looking at all scriptures referenced with this word and read them. Ask the Holy Spirit to lead you, and He’ll lead you and reveal things to you.

When I first started studying the Word, I didn’t have very good relationships. I didn’t really understand what love was.

As I studied the subject of love, I learned that it’s more than a gooey feeling, It’s a decision on how you’re supposed to trust people. I didn’t know how to love people, or myself. By studying what the Bible says about love, I learned how to love. Then my life began to change.

Being able to apply what you study to your life, like I did on the subject of love, is just one picture of what studying the Bible looks like.

Hopefully you understand why you should study with some ideas on what to study. Here are four steps you can take to begin digging into God’s Word now:

Four Effective Steps to Studying the Bible

1. Purposely set aside time. I make an appointment with God in the mornings, but if that doesn’t work for you, find a time that does…even if it’s not every day. Whatever you can do, that’s what you need to do. Just start somewhere and you’ll see the fruit that this time brings to your life!

2. Make preparation for your Bible study. Have a place that you enjoy being—a room in your house where you can be alone. Somewhere you are comfortable and like to be.

3. Have all your materials available. You’ll want of course your Bible, but also get a good Bible dictionary, concordance, a pen and paper. That way, you don’t have to stop every few minutes to reference something or write something down.

4. Prepare your heart. Talk to God about things you may need to confess, and enter your study time peacefully and without anything that may block you from receiving revelation during your study.

Make the time in your life to study because there is power in it to change your life and become the person God wants you to be. Once you do, you’ll experience the peace and joy to enjoy every day of your life!

- Joyce Meyer -

Dokii azungumzia ulokole wake!

Dokii
Bwana Yesu asifiwe Dokii.

Dokii: Ameeen!

Swali: Siku za nyuma ilisemekana uliokoka na kuachana na matendo maovu na ukafanikiwa kutoa albamu moja ya nyimbo za injili lakini nasikia umepotoka, kulikoni?

Dokii: Nani kasema nimekengeuka. Mimi ni mlokole safi hata Mungu anajua hilo. Hata mimi nasikia watu wanasema nimeachana na wokovu lakini hawajui suala la wokovu ni la mtu binafsi na Mungu wake.

Swali: Unahisi kwa nini wanasema umeachana na wokovu?

Dokii: Nafikiri kwa sababu ya kuona nimerejea katika masuala ya sanaa ambayo ndiyo yalinifanya nijulikane mpaka leo hii. Watu wengine huwa wananishangaa kuona nimesuka aina fulani ya mtindo ambao huwa hawaupendi.

Swali: Inasemekana umekuwa ukienda kwenye majukwaa ya kumbi za burudani na kufanya mambo ambayo ni chukizo mbele za Mungu na kuonekana kama huna wokovu ndani yako. Je, ni kweli?

Dokii: Siyo kweli. Mimi huwa siwaelewi watu wanaojiita walokole kwa kufuatilia maisha ya mtu. Hata maandiko yanasema asiyefanya kazi na asile. Sasa mimi nikifanya kazi ya sanaa naonekana ni mtenda dhambi. Wangapi ambao wanafanya mambo ambayo ni machukizo mbele za Mungu na hawasemi chochote? Nimesoma sana Biblia sijaona sehemu inapomuelekeza mtu kazi ya kufanya bali imesema asiyefanya kazi na asile. Ninachojua mimi nafanya kazi ambayo ni halali hata Mungu anaitambua, wanaosema mimi nimekengeuka wananikosea heshima.

Swali: Kwa nini uliamua kuachana na uimbaji wa nyimbo za injili ukaanza kuimba nyimbo nyingine?

Dokii: Mimi bado ni mwimbaji wa nyimbo za injili na mpaka sasa ninaimba katika kwaya moja maeneo ya Mwananyamala, ukifika hapo ndiyo watakwambia kama kweli mimi nimeacha wokovu.

Swali: Unaimba katika kwaya gani?

Dokii: Ninaimba katika kwaya moja maeneo Upanga katika Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG).


Swali: Kwa nini uliachana na muziki wa Injili na kurejea upande wa pili?


Dokii: Muziki wa Injili unahitaji utulivu sana na pia unahitaji kuwa na mtaji wa kutosha ili ufanye promosheni. Nililazimika kukaa pembeni kwa sababu najua kama ningeamua kujikita zaidi huko, leo hii nisingekuwa hapa nilipo.

Swali: Kama ni hivyo kwa nini usingebaki katika ulokole huo na kucheza sinema za kilokole ili kuponya roho za watu wengi zinazoangamia?


Dokii: Sawa lakini wakati wa kufanya hivyo haujafika na ipo siku nitafanya hivyo.


Swali: Staili zako za unyoaji na mavazi yako ndivyo huwafanya watu washindwe kukuamini kama kweli umeokoka. Unalizungumziaje hili?


Dokii: Ni kweli kabisa, lakini kila nikisoma maandiko matakatifu sioni kama yanaelekeza jinsi ya uvaaji ama unyoaji. Nawashangaa wanaonisema juu ya uvaaji wangu.

Hayo ndo yalikuwa Mazungumzo kati ya Mwandishi wa Habari hii na Dokii.

- George Kayala -

Saturday, February 23, 2013

Umuhimu wa Kujua Neno la Mungu.

Evangelist Simon Mkanza
Mwinjilisti Simon Mkanza
Shaloom Mpendwa!

Upo umuhimu wa kujua neno la Mungu katika maisha ya Mkristo halisi. Biblia  inatuambia Yesu Kristo ndiye Neno la Mungu. Kwa maneno mengine Yesu ndiye Neno ambalo Mkristo anapaswa kuwa nalo (Yohana 1:1).
 

Kwa kusema hivyo kuna  umuhimu wa kumjua Yesu na kumshika, kwa maana yeye ndiye Neno la Mungu. Katika Biblia mtume Petro anasema mbele za Yesu kwamba, twende kwa nani na wewe ndio mwenye maneno ya uzima? Petro alijua upo umuhimu wa kumjua Yesu kama Neno maana ndani ya Neno kuna uzima

Biblia inasema neno la Kristo likae kwa wingi ndani yetu (Wakolosai 3:16).

Kwa nini basi neno la Kristo likae kwa wingi ndani yetu? Ni kwa sababu lina mambo yafuatayo ambayo ni muhimu katika maisha yetu ya Ukristo. Mambo hayo ni…

A) Neno la Mungu li Hai

B) Neno la Mungu lina nguvu (Mwanzo 1:6).

C) Neno la Mungu lina ukali kuliko upanga

D) Neno la Mungu linachoma hata kuzigawanya nafsi, roho viungo na mafuta yaliyomo ndani yake

E) Neno la Mungu li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.


Kwa Nini Neno la Mungu li Hai?

Neno la Mungu li hai kwa sababu  Mungu mwenyewe analithibitisha kwamba li hai maana

a) Linafanya mabadiliko (Isaya 55:10-11).

b) Linatupa kushinda dhambi (Zaburi 119:11).

c) Neno la Mungu  li hai kwa sababu linatupa mafanikio katik mwili. Petro anasema ”kwa neno lako tunatupa nyavu zetu.“  Hapa tunaona kuwa Neno la Mungu  pekee yake ndilo linaloweza kuleta majibu katika maisha yetu (Luka 5:3-6).

Uhai wa Neno la Mungu kwa mtu ndio unaoleta kushinda dhambi. Nao wakamshinda kwa neno la ushuhuda wao (Ufunuo 12:11).

Daudi aligundua au kwa maneno mengine alifahamu umuhimu wa neno la Mungu katika maisha, kama vile mtume Paulo anavyosema na Wakolosai kwa habari ya neno la Kristo kwamba likae kwa wingi ndani ya mioyo yetu.

Neno la Mungu lina nguvu na ndio maana  tunamshinda  shetani kwa neno la Mungu. Yesu kama kielelezo yeye mwenyewe ni neno ndani ya neno anamshinda shetani (Luka 4:1-12). 
 

Katika mistari hiyo tunaona Yesu anamwambia  shetani  ”imeandikwa“   Shetani nae anageuza usemi nae anamwambia Yesu ”imeandikwa kwamba atakuagizia malaika usije ukajikwaa mguu wako.“ Kwa kuwaYesu neno la Mungu limo ndani yake hamwambii tena shetani imeandikwa ila anamwambia imenenwa.
Kwa maneno mengine tukiwa na neno la Yesu ndani yetu hatuwezi kuyumbishwa. Kwanini? Kwa sababu tumeshaona jinsi ambavyo shetani  anajaribu kutumia neno la Mungu   kwa kusema ”imeandikwa.“  Na ni kweli imeandikwa ananukuu kutoka kitabu cha Zaburi 91 :1-12.

Hata kama shetani ananukuu maandiko haina sababu  yamimi kushindwa na shetani  maana Yesu tayari alikwisha mshinda. Yesu kumshinda shetani ina nipelekea mimi kusoma neno la Mungu kwa bidii sana. Kwa mfano, ni kweli kabisa imeandikwa mtakula vitu vya kufisha havitawadhuru lakini je, ninywe sumu sitakufa kwa sababu imeandikwa? Hapana, ukinywa hakika utakufa. Shetani hutumia mandiko kuwafunga wasiojua neno la KristoYesu. 
 

Katika Biblia tunasoma pia kwamba ”imeandikwa“ Wanandoa MKE na MUME wasinyimane. Kwa kutojua neno vijana wa kiume na wa kike wamedanganywa. Si hao tu hata walioko kwenye ndoa wametegwa kwa andiko hilo. Neno linasema katika Mithali 6:32 ”Aziniye na mwanamke hana akili kabisa“ na Mwanamke vivyo hivyo akizini na mwanaume hana akili kabisa. Watu wamepata hasara ya mambo mengi kwa kutojua neno la Mungu. Ili tuweze kumshinda shetani  ni lazima  neno la Yesu liwe ndani  yetu ndiposa tutamshinda shetani. Ayubu kwa neno la Mungu alishinda. (Ayubu 19:25-27, Waefeso 6:17).

Nataka nikwambie neno la Mungu ni msaada katika maisha yetu maana hutupa  majibu ya maisha yetu. Katika Luka 5:3-6 tunasoma jinsi Petro na wenzake walivyopata samaki wengi kwa kutii neno la Kristo. Kumbuka pia juu ya yule akida, alimwambia Yesu ”...sema neno tu na mtumwa wangu atapona“ (Luka 7:2-10). Yesu akisema neno lazima mabadiliko yatokee. 
 

Neno la Mungu lina ukali kuliko upanga. Kwa nini neno la Mungu  lina ukali kuliko upanga? Upanga unaweza kukukata na usipone. Lakini neno linakata na kuponya. Kwa neno hili wafalme wanatubu. Yona alitumia neno la Mungu likawa kali watu wakatubu. (Yona 3:1-10; Matendo ya Mitume 8:18-24).

Neno la Mungu linachoma hata kuzigawa nafsi na roho na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake (Matendo 7:51-54, Yohana 4:16 -18, 27-29). Mwanamke akaambiwa mambo yake; Neno likachambua kila tabia.

Neno la Mungu li jepesi kutambua mawazo na makusudi ya moyo.

Yesu kama Neno la Mungu anajua mambo ambayo watu wanawaza ndani ya mioyo yao (Luka 5:17-24, 6:6-8 ; Mathayo 16:1-4). Yapo makusudi ya moyo ambayo ni ya siri sana kwa mwanadamu lakini nataka nikuambie neno la  Mungu ni jepesi kutambua makusudi ya moyo. 
 

Mtume Petro aliyependa kujua neno la Mungu, naye pia Mungu alimjalia neema ya kuyajua makusudi ya moyo wa mwanadamu (Matendo 5:1-11). Elisha aliyajua makusudi ya moyo wa mfalme ya kuwatenda Israeli kwa siri ila Mungu alimpa neema ya kuyajua mawazo ya mfalme (2 Wafalme 6:8-12). 
 

Hili ni jambo la msingi katika maisha ya Mkristo yaani kulijua neno la Mungu. Neno la Mungu  tukiwa nalo na likitenda kazi ndani yetu lazima tufanikiwe (Yoshua 1:8)

Je unahitaji kuwa na imani katika neno la Mungu? Basi, ni neno la Mungu peke yake ambalo laweza kuumba imani, maana pasipo neno la Mungu hakuna imani (Waebrania 11:3 ; Warumi10:17). Ili uwe mwanafunzi wa Yesu ni lazima ulijue neno la Mungu na kulishika.(Yohana 8:31 ; Luka 2:19).
Kama neno halimo ndani yetu tunayoyafanya yanakuwa hayana Mungu, hata twaweza kusalitiana. Mtu anayelitamani neno la Yesu  huling’ang’ania na kulitenda maana kwake ni nguvu. (1Wakorintho 1:18). Si kwamba Neno la Mungu ni nguvu tu: bali huleta faida (Mathayo 13:23). Watu wengi tunapotea kwa kutokujua uwezo (nguvu) iliyomo katika neno la Mungu (Mathayo 22:29).

Yesu anasema, mtu anayelitenda neno la Mungu na kulishika huyo amepanda mbegu ambayo itazaa sana, maana ndani ya moyo wake imo mbegu ambayo ni neno la Mungu la uponyaji na mafanikio, msamaha, utu wema na mengi yanayofanana na hayo.

Yapaswa maisha yetu yawe yenye neno (mbegu) la  Mungu ili tuweze kuzaa mambo mazuri.

Wokovu wetu unaimarika kwenye neno la Mungu. Hilo neno la Mungu tunalipata wapi? Isaya 34:16. Upo umuhimu wa kuyachunguza maandiko ili kujua Mungu anasema nini (Matendo 17.10-11).  Je, tangu ulipowekwa msingi wa wokovu, neno limo ndani? (Hagai 2:18-19). Kila kitu kinaweza kupita lakini sio neno la Mungu (Isaya 40:8, Mathayo 24:35).

Ili neno litende kazi katika kinywa chako unapolitamka na kuamini ni lazima iwepo nguvu ya Roho Mtakatifu. Bila hii nguvu hamna kitakacho endelea. Utasema umeamini lakini hakutakuwa na matokeo. Mungu mwenyewe alipotamka neno liliambatana na nguvu ya Roho Mtakatifu (Mwanzo1:2-3).
Imeandikwa na Mwinjilisti  Simon Mkanza
0784 475622, 0786 477021

Friday, February 22, 2013

Facebook na Watumishi wa Mungu leo.

Kadinali Timothy Dolan azungumzia Kashfa za kimaadili kanisa katoliki.

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/7d84cef20b45c62c8b260e6d60216ea4_XL.jpg
Kadinali Timothy Dolan wa Kanisa Katoliki
 Kadinali Timothy Dolan ambaye ni mmoja wa maaskofu wanaotarajiwa kumrithi Papa Benedict wa XVI aliyejiuzulu hivi karibuni amesema kuwa kuanzia sasa watu wote wanaotarajiwa kuwa mapadri na maaskofu watakuwa wanachunguzwa tabia zao tokea utotoni.

Matamshi hayo yamekuja baada ya mchungaji mwingine mmoja wa mji wa Milwaukee ambao ni moja ya miji mikubwa ya jimbo la Wisconsin nchini Marekani kuwatumia vibaya kijinsia watoto wadogo. Kwa upande wake, Frank Lokoko, mtaalamu wa masuala ya sheria wa mji wa Milwaukee amesema kuwa, Kadinali Dolan alihojiwa kwa muda wa masaa matatu  na mawakili wa watoto waliotumiwa vibaya kijinsia na makasisi wa mji huo.

Amesema, Timothy Dolan alikuwa Askofu mkuu katika kipindi cha miaka ya 2002 hadi 2009 na ni mmoja wa makadinali 10 wanaowania nafasi ya kurithi kiti cha Papa Benedict wa XVI.

Ijapokuwa limekuwa ni jambo la kawaida kwa wakuu wa Kanisa Katoliki kufanya vitendo vichafu vya kijinsia huko Magharibi, lakini kuongezeka vitendo viovu vya ufisadi wa kimaadili na ubadhirifu wa fedha, vitendo ambavyo vimewahusisha hata viongozi wa ngazi za juu kabisa wa kanisa hilo, ni jambo ambalo limeyatumbukiza makanisa hayo ya Magharibi katika mgogoro mwingine mkubwa zaidi, tangu ule wa karne za kati wakati kanisa hilo lilipofanya mauaji makubwa ya watu kwa imani za kidini.

Watu wengi hivi sasa wamekuwa wakiyapa nguvu madai kuwa maaskofu wa kieneo na hata wa Vatican kwenyewe wanafanya kwa siri vitendo viovu vya udhalilishaji wa kijinsia na ni kwa sababu ndio maana maaskofu wa chini nao wakapata nguvu za kuwatumia vibaya hata watoto wadogo. Hali hiyo imejitokeza katika hali ambayo tangu miaka mingi nyuma, wachungaji walikuwa na heshima kubwa kati ya wananchi wa Magharibi.

Hata hivyo imani hiyo ya watu imepungua hasa baada ya kugunduliwa kashfa za kimaadili za wakuu wa Kanisa tena basi dhidi ya watoto wadogo. Takwimu zinaonesha kuwa watu wenye imani na Kanisa hasa kati ya wanawake, inazidi kupungua huko Magharibi huku idadi ya wanaokwenda kanisani nayo ikizidi kushuka chini.

Yamkini majibu ya sababu za kushuhudiwa hali hiyo yakawa yamo ndani ya matamshi ya Kadinali Martini ambaye hakuona tabu hata kidogo kutangaza malalamiko yake kuhusiana na utendaji mbaya wa Kanisa Katoliki. Kadinali Martini wa Milan, Italia, alikuwa askofu kwa muda wa miaka 20 na hata alitajwa kuwa ndiye Papa wa baadaye wa Kanisa Katoliki.

Alisema miaka michache kabla ya kufariki kwake dunia na katika mahojiano yake ya mwisho kwamba, Kanisa Katoliki liko nyuma kwa miaka 200. Alisema kama mabadiliko ya kimsingi hayatafanyika katika Kanisa Katoliki, basi kizazi kipya kitajitenga na kanisa hilo na kwamba mabadiliko hayo inabidi yaanze kwa Papa mwenyewe na kufuatiwa na maaskofu.

Thursday, February 21, 2013

Askofu Mokiwa aenguliwa Uaskofu Mkuu wa Kanisa Anglican.

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk Valentino Mokiwa ameshindwa kutetea nafasi yake ya uskofu mkuu wa kanisa hilo Tanzania baada ya kushindwa na Dk Jacobo Chimeledya (56) wa Jimbo la Mpwapwa.

Askofu Chimeledya ambaye anakuwa kiongozi wa sita kushika wadhifa huo nchini, aliibuka mshindi baada ya jina lake kupenya katika hatua tatu za kura.

Akitangaza matokeo hayo jana jioni, Katibu Mkuu wa Anglikana, Dk Dickson Chilongani alisema kanisa hilo halina utaratibu wa kutangaza kura zilizopigwa lakini akathibitisha kuwa Askofu Chimeledya ndiye mshindi.

Dk Chilongani alisema kuchaguliwa kwa Askofu Chimeledya ni utaratibu wa kanisa hilo ambalo hufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano.

Uchaguzi huo ulianza kwa ibada iliyoongozwa na Askofu wa Dayosisi ya Dodoma, Godfrey Mhogolo na baada ya hapo, Msajili wa kanisa hilo, Profesa Palamagamba Kabudi alitangaza utaratibu wa uchaguzi.

Chilongani alisema wajumbe 129 walihudhuria mkutano huo kati ya wajumbe 140 waliotarajiwa.

“Kwa kawaida katika uchaguzi, askofu yeyote mwenye umri chini ya miaka 60 huwa anaweza kuwa mgombea na katika uchaguzi huo, maaskofu 21 walikuwa na sifa za kugombea,” alisema.

Dk Chilongani alisema Askofu Chimeledya alizaliwa mwaka 1957 na alisoma stashahada ya theolojia katika Chuo cha St. Philipo kilichopo Kongwa, Dodoma.

“Baadaye alikwenda Kenya na kuchukua shahada ya masomo ya dini katika Chuo cha St. Paul kabla ya kwenda kusomea shahada ya uzamili katika theolojia Marekani,” alisema.

Askofu Chimeledya aliteuliwa kuwa Askofu Mwandamizi wa Jimbo la Mpwapwa chini Askofu Simon Chiwanga mwaka 2007.

Baada ya Askofu Chiwanga kustaafu Dk Chimeledya aliteuliwa kuwa askofu wa dayosisi hiyo. Alisema askofu huyo mpya atawekwa wakfu mwishoni mwa Mei mwaka huu katika ibada itakayofanyika katika Kanisa Kuu la mjini Dodoma.

- Mwananchi -

Kanisa la TAG Songea latishiwa kuchomwa Moto.

 KANISA la Tanzania Asemblies of God (TAG) mtaa wa Msufini Songea mjini mkoani Ruvuma limetishiwa kuchomwa moto kutokana na maandishi yaliyoandikwa kwenye ukuta wa jengo la kanisa hilo yanayosomeka ‘CHOMA’.

Mchungaji wa Kanisa hilo, Alimosa Mwasangapole alisema ameshitushwa na maandishi hayo kutokana na mfulululizo wa matukio mbalimbali hasa kuchomwa moto makanisa na kuuawa kwa baadhi ya watumishi wa Mungu nchini.

Mwasangapole alisema baada ya kuona maneno hayo alikwenda kutoa taarifa polisi ambao wamemuahidi kulifuatilia suala hilo.

Naye Oliver Richard kutoka Iringa anaripoti kuwa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa, Dk. Owdenberg Mdegela amezungumzia uhalifu unaoendelea nchini dhidi ya matukio yanayoambatana na mauaji ya viongozi wa dini na uharibifu wa nyumba za ibada.

Dk. Mdegela alisema kwamba uhalifu huo upo nyuma ya vikundi kadhaa vilivyopatiwa mafunzo maalumu nje ya nchi kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo ambao umelenga kuwaangamiza maaskofu na mapadre.

Alisema amewaandikia waraka wanachama wote wa Jumuiya ya Makanisa ya Kikristo Tanzania (CCT) kuanza mara moja mfungo wa saa 24 kuanzia jana.

Hatua hiyo kwa ajili ya kuwasaidia makachero kutoka ndani na nje ya nchi kuwabaini wanaotekeleza mkakati huo dhalimu.

”Vikundi hivyo vinataka kuichafua serikali, kuuvunja Muungano na kuifanya Zanzibar kuwa nchi ya dini.

Serikali ichukue au isichukue hatua sisi tunakwenda madhabahuni na ndiyo maana nimeitisha maombi kwa makanisa yote ambayo ni wanachama wa CCT.

“Ingawa matamko haya hayawezi kumaliza tatizo, tutasugua goti kudhihirisha nguvu ya maombi,” alisema na kuongeza:

”Naagiza kuwe na ulinzi kuanzia geti la mbele la nyuma na kwenye kengele ili wakitokea watu hao, walinzi wapige kengele na kupambana nao”.

- Mtanzania -

Facebook na Watumishi wa Mungu leo.

Dar yaibuka kidedea Tamasha la Pasaka.

HATIMAYE Jiji la Dar es Salaam limeshinda katika mchakato wa kuchagua mkoa wa kwanza kati ya saba ambayo Tamasha la Pasaka mwaka huu litafanyika.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama, ilisema kamati yake iliendesha kura za maoni kwa mashabiki wao, wa eneo lipi tamasha hilo lifanyike.


“Tulifanya kura za maoni kwa njia ya simu za mkononi, pia tulikuwa na vipindi maalumu kwenye baadhi ya redio kwa mashabiki kutoa maoni yao.


“Mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya, Dodoma na Mwanza ilikuwa ikichuana vikali katika kupata mahali ambapo tamasha litafanyika, maana tulikuwa bado hatujatangaza.


“Lakini leo tumechagua Dar es Salaam, ambapo zaidi ya mashabiki 15,000 walichagua tamasha lifanyike Dar es Salaam, mashabiki 13,000 walitaka lifanyike Mbeya, mashabiki 7,000 walitaka Mwanza na mashabiki 3,000 walitaka Dodoma,” alisema Msama.

Alieleza kuwa hivi sasa wanatazama mkoa upi lifanyike Jumatatu ya Pasaka na siku zingine zitakazofuata.


“Siku yenyewe ya Pasaka tushapata kwamba ni Dar es Salaam, sasa tunajipanga kwa siku zingine, maana mwaka huu tunataka mikoa saba tufanye tamasha letu,” alisema Msama na kuongeza kuwa kwa Dar es Salaam litakuwa Machi 31.


Pia alisema bado wanaendelea na mazungumzo na wasanii mbalimbali kwa ajili ya kushiriki tamasha la mwaka huu.

- Elizabeth John -

Waziri Aboud azomewa kwenye Mazishi ya Padri Evarist Mushi.


SIMANZI na vilio vilitawala mazishi ya Padri Evarist Mushi yaliyofanyika Kitope Zanzibar jana huku Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud akipata wakati mgumu baada ya kuzomewa na waombolezaji kutokana na kukerwa na hotuba yake.

Padri Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi, Jumapili iliyopita wakati akijiandaa kwenda kuongoza misa katika Kanisa la Mt. Joseph Minara Miwili mjini hapa.


Ibada ya mazishi iliyoongozwa na Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo ilianza saa nne asubuhi katika Kanisa la Mt. Joseph Minara Miwili na kuhudhuriwa pia na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.

Baada ya misa hiyo iliyomalizika saa 6.30 mchana, msafara wa mazishi ulielekea Kitope yalipo makaburi ya viongozi wa Kanisa Katoliki. Baada ya kufika makaburini, ibada ya mazishi ilianza saa 7.30 mchana na mwili wa Padri uliwekwa kaburini saa moja baadaye.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa.

Waziri Kuzomewa
Waziri Aboud alizomewa kutokana na kauli yake aliyotoa katika salamu za Serikali kuwa kifo cha Padri Mushi ni kazi ya Mungu, ambayo haina makosa.

“Serikali imepokea msiba huu kwa huzuni na masikitiko makubwa. Maumivu ya familia ya marehemu ni maumivu ya Serikali. Padri Mushi ametuachia pengo kubwa lakini kazi ya Mungu haina makosa,” alisema Waziri Aboud kauli ambayo ilipokewa kwa waomboleza kuguna wengine wakizomea hali iliyowafanya baadhi ya viongozi kuwatuliza.


Mmoja wa waombolezaji alisikika akisema: “Kazi ya Mungu ndiyo imewatuma hao wahalifu kuua kwa risasi?”

Mwakilishi wa familia, Francis Mushi alijibu kauli ya waziri huyo alipopewa nafasi ya kutoa salamu kwa kusema: “Tumeupokea msiba huu kwa masikitiko makubwa hasa kwa kuwa Padri hakuugua… Alikuwa kiungo kikubwa katika familia yetu.” Maneno ambayo yaliibua simanzi na vilio kutoka kwa waombolezaji wengi.

Hata Askofu wa Jimbo Katoliki Zanzibar, Augustino Shao aliyekuwa amekaa karibu na Rais Dk Shein alipopewa nafasi naye alisema waziwazi: “Naomba kusema kuwa, kauli hii ya mapenzi ya Mungu haipo… Hili ni suala la uovu na tusikubali kushindwa na uovu.” Kauli hiyo ilionekana kuungwa mkono na waumini.

Ibada hiyo ilihitimishwa kwa sala iliyoongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga, Antony Banzi.
 
- Mwananchi -

Namna ya Kuongeza Imani unapokuwa kwenye Jaribu.

2
Mpenzi msomaji Shalom,


Biblia katika kitabu cha Mathayo 17:18 inasema‘..Ni kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana amini nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

Hii ni habari ya yule kijana aliyekuwa na pepo bubu na kiziwi, mzazi wake akamleta kwa wanafunzi wa Yesu wamwombee. Biblia inatueleza kwamba wanafunzi walijaribu kumtoa yule pepo wasiweze, wakati huo Yesu alikuwa amepanda Mlimani kwenda kuomba.

Yesu aliporudi alielezwa kilichotokea, akawakemea wanafunzi wake na kisha akamuombea yule kijana akapona. Baadaye wanafunzi wa Yesu wakamuuliza, kwa nini sisi hatukuweza kumtoa yule pepo. Ndipo Yesu akawajibu akasema ‘Ni kwa sababu ya upungufu wa imani yenu… Neno upungufu lina ya isiyo – tosheleza, yaani imani yao ilikuwa ina upungufu na kwa hiyo wasingeweza kumtoa yule pepo.

Jambo ninalotaka tuliangalie ni kwamba kwa kuwa tatizo lilikuwa ni upungufu wa imani yao, ina maana walitakiwa kuongeza imani yao wakati wanaendelea kukemea. Sasa swali muhimu ni je wangeongezaje imani yao wakati wako kwenye jaribu/vitani?.

Naam licha ya swali hili kuna maswali mengine ambayo ni muhimu kuyatafakari ili tuweze kuwa na ufahamu mzuri wa imani. Je upungufu huu wa imani kwa wanafunzi walikuwa nao kabla hawajaanza kukemea yule pepo au ulikuja wakati wanaendelea kuomba. Naam Yesu anatuonyesha kwamba kosa la hawa wandugu wenzetu lilikuwa upungufu wa imani yao?

 Ni kwa namna gani walikuwa na upungufu wa imani?
Biblia katika Waebrania 11:1 inaeleza kwamba ‘imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo yasiyoonekana’. Kwa hiyo endapo Yesu alisema ni kwa sababu ya upungufu wa imani yao ina maana ndani yao walipungukiwa uhakika wa kile walichokitarajia, ambacho ni kufunguliwa/kuponywa kwa kijana mwenye pepo. Naam upungufu wao wa imani ulitokana na  mashaka juu ya uhakika wa yule kijana kufunguliwa.

Nini kilipelekea wao kuingiza hofu/mashaka?
  • Kukosekana kwa dalili za kijana kufunguliwa – Ni imani yangu kwamba wanafunzi walipoanza kukemea walikuwa na uhakika kwamba Yule kijana atafunguliwa. Naam kadri walivyoendelea kuomba na kuona kwamba hakuna mabadiliko ya aina yoyote kwa mgonjwa yule ndipo hofu/mashaka yakawaingia mioyoni mwao.  

  • Maneno ya kusikia – Ikumbukwe kwamba chanzo cha imani yoyote ni kusikia (Warumi 10:17)?  Kumbuka wakati wanendelea kuomba kulikuwa kuna kundi kubwa la watu ambao walikuwa wanamsubiri Yesu pamoja nao. Hivyo huenda wakati wanafunzi wanaaendelea kuomba walisikia watu wakisema, wanafunzi wa Yohana wenyewe walishindwa kumuombea, wao wataweza, wamejaribu watumishi wa kila aina wameshindwa, huyu hawezekani anasubiri kifo, naam haya yote yakapunguza uhakika ndani yao kwamba kwa jina la Yesu yule kijana anaweza kupona.
  • Maneno yao wenyewe – Biblia haituelezi namna/approach waliyoitumia kuomba/kukemea. Huenda walianza kuomba mmoja mmoja/ au waliomba wachache na mwishowe ndipo wakaomba kama kundi. Kwenye kundi lolote kuna mengi, huenda walipokemea kwa muda kadhaa na bila kijana kuonyesha dalili za kupona baadhi ya wanafunzi wakaingiwa na hofu na wakawaambukiza na wengine na hivyo kushindwa kumtoa pepo. Hebu jaribu kufikiri mtu kama Yuda Iskariote alikuwa anafanya nini wakati wenzake wanakemea?
Nini cha kufanya?
Hofu/mashaka ni silaha kubwa sana ambayo Shetani huitumia kuwafanya watu washindwe kupata majibu ya maombi/miujiza yao kutoka kwa Mungu. Shetani anafahamu kwamba imeandikwa ‘Mwenye haki wangu ataishi kwa imani, naye akisstasita roho yangu haina furaha naye’ (Wabrania 10:38).

Hivyo ili kuharibu/kuondoa imani ya mtu kwa Mungu, silaha anayotumia ni kuingiza mashaka moyoni mwake dhidi ya ahadi za Mungu/neno la Mungu kwenye maisha yake. Yesu aliwaambia hivi wanafunzi wake ‘… amini nawaambia yeyote atakayeuambia mlima huu ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake’ (Marko 11:22).
  
Mpenzi msomaji kamwe usimruhusu Shetani kwa kutumia silaha hii ya mashaka azuie baraka zako na wale wanaokuhusu maishani mwako. Haijalishi jaribu limesimama mbele yako kwa kiwango gani usiondoe imani yako juu ya kile ambacho Yesu amekisema kwenye neno lake juu yako. Naam Mungu wetu si mtu hata aseme uongo, ahadi zake ni amina na kweli. 

Naam katikati ya jaribu/changamoto wewe ongeza imani yako kwa kupambana na roho ya mashaka/hofu, naam tumia Biblia ili ikuongoze kukupa mistari ambayo itakuongezea uhakika wa kufanikiwa katika lile ulifanyalo.
 
Zaidi kuwa makini na maneno ya kusikia kwa habari ya imani yako. Wanafunzi wa Yesu walipaswa kutokujali maneno ya kusikia kutoka kwa watu, au kwa wenzao walioingia mashaka, naam walipswa kudumu kuamini kwamba kijana atapona naam ingekuwa hivyo. Je si unakumbuka habari za Petro alivyoambiwa na Yesu atembee juu ya maji. Awali alianza vema na akatembea hatua kadhaa juu ya maji.

Biblia inasema dhoruba ilipompiga akaona shaka na kuanza kuzama. Kwa nini alizama? si kwa sababu Yesu hakuwepo, bali ni kwa sababu aliona shaka.

Naam kitu kilichopungua kwenye imani ya wanafunzi, ni uhakika kwamba yule kijana atapona. Na kilichopelekea upungufu wao wa imani, si   kutokumwamini/kumjua Yesu, bali ni kuruhusu hofu ichukue nafasi ya imani/uhakika waliokuwa nao kwamba yule mgonjwa atapona. Naam kwa mara nyingine tena ‘usirihusu hofu iharibu muujiza/future yako’.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nawe daima!

Imeandikwa na Mwl. Patrick Sanga
0715 816800, 0755 81680

Wednesday, February 20, 2013

Facebook na Watumishi wa Mungu leo.

Mbadala wa Joyous Celebration Hawa Hapa.

Safari ya Mwisho ya Padri Evarist Mushi.

Jeneza lenye Mwili wa marehemu Padri Evarist Mushi aliyeuwawa kwa kupigwa risasi huko Zanzibar.

Mabadiliko ya Tamasha la Jessica Honore.

Jessica Honore
 Muda Mfupi uliopita Jesca Honore kupitia ukurasa wake wa facebook ametoa taarifa ya mabadiliko ya tamasha lake alilotarajia kulifanya pale Serena Hotel.

Jesca amesema "ARIFA YA MABADILIKO:ZIMA UKIMYA NA JESSICA HONORE, ITAKUJIA NDANI YA CITY CHRISTIAN CENTER, TAREHE 24 MARCH, BADALA YA SERENA HOTEL 10 MARCH. KUMRADHI KWA MABADILIKO HAYA, NIKATIKA HALI YA KUBORESHA!! DONT MISS THE CONCERT DATE 24 MARCH AT CCC UPANGA. LOVE U ALL!! slogn(The jessica Music/change the atmospher)"

USIKOSEEEEEEEE!!!

Usikose Hii pale Atriums Hotel na Glorious Celebration.

Picha 4 zikionyesha Taswira halisi ya Kanisa lililochomwa Moto huko Zanzibar.

 

http://2.bp.blogspot.com/-TkQ56lYuQgY/USOv5NGCwMI/AAAAAAAAb08/iFPH4sZxZns/s1600/KANISA1.bmp

http://2.bp.blogspot.com/-AFV0c1soIXw/USOuuCv2BFI/AAAAAAAAb0o/ZSOFw7_fhPI/s1600/KANISA2.bmp 

http://1.bp.blogspot.com/-ZY2T0sSy1FQ/USOv786dVnI/AAAAAAAAb1E/Wq3lQ7ye-MM/s1600/KANISA3.bmp

Tuesday, February 19, 2013

Vitu vyenye thamani ya Millioni 3.5 vyaharibika kwenye Kanisa lililochomwa Moto huko Zanzibar.

LEO asubuhi vyombo vingi vya habari vimeripoti Juu ya Uchomwaji wa Kanisa la The Pool of Siloam la huko Zanzibar kwa kutupiwa vitu vilivyosababisha moto huo.

Jioni hii tumezungumza na Mchungaji wa Kanisa wa Kanisa hilo ambaye amethibitisha kuwa vitu vyenye Thamani ya Shilingi Milioni 3 na nusu vimeharibika vibaya na vyote vilikuwa upande wa Madhabahuni.

Aidha Mlinzi wa Kanisa hilo amesema kuwa, mida ya Saa 9 usiku aliona watu watatu wakipita karibu na Kanisa hilo na kutupia vitu viwili ndani ya Kanisa hilo upande wa madhabahuni na baada ya yeye kuona hivyo alikimbilia Upande wa pili na muda mfupi baadaye aliona moto ukianza kuwaka upande wa madhabahuni hivyo kuamua kumpigia Simu Mchungaji wa kanisa hilo.

Kwa Mujibu wa Maelezo ya Mchungaji huyo, tukio hili ni la pili kulikumba Kanisa hilo kwani lilishawahi kukumbwa na tukio lingine kama hilo.

Kwa Maelezo Zaidi, Sikiliza Kipindi cha Alive Fm Matukio leo Saa 2 Kamili Usiku kupitia Masafa ya 91.9Mhz kwa Wakazi wa Kanda ya Ziwa. Kama Uko Nje ya Mwanza, Sikiliza Hhc Alive Fm Online Kupitia; www.hhcalivefm.org

Namna ya Kumtumia Roho Mtakatifu kama Msaidizi kupitia kazi zake.

Yohana 14:16-18 … Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni, wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu”.

Katika somo hili nataka kuandika juu ya kazi za Roho Mtakatifu na kukuonyesha namna unavyoweza kumtumia Roho Mtakataifu kama Msaidizi kupitia kazi zake. Labda niseme kwa lugha hii, kama unataka kuona msaada wa Roho Mtakatifu kwenye maisha yako, ni lazima kwanza uzijue kazi zake, maana kazi zake ndizo zinazotuonyuesha maeneo ya msaada wake, kazi zake ndizo zinazofafanua kwa namna gani Roho Mtakatifu ni Msaidizi.

Roho Mtakatifu ni nani?
Roho Mtakatifu ni Mungu, mwenye nguvu zote, maarifa yote, anayepatikana kila mahali. Yeye anayo nafsi na ameamua kuishi ndani ya mwili wa mwanadamu. Kusudi kubwa la ujio wake ni kuwa Msaidizi wa mwanadamu kwenye ulimwengu huu wa mwili, ili kumsaidia kuishi katika mapenzi ya Mungu.

Roho Mtakatifu amemamua kuishi ndani ya mwili wa mtu kwa sababu, Mungu hana namna ya kutawala kwenye ulimwengu wa kimwili bila kuwa na mwili wa damu na nyama, kwa kuwa yeye ni Roho (Yohana 4:24). Hivyo hana budi kuingia kwenye mwili wa mtu na kufanya makao yake hapo, ili kutawala na kumuongoza mwanadamu katika mapenzi yake. (Yohana 14:23, Yohana 14:18, Ufunuo 3:20, 1Wakorinto 3:16-17, 6:19).

Kinachotusaidia kujua kwamba Roho Mtakatifu ana nafsi, ni tabia zake, maana kwenye kila nafsi kuna hisia, nia, kumbukumbu, akili nk. Baadhi ya sifa na tabia za Roho Mtakatifu ni; anapatikana kila mahali (Omnipresence), Zaburi 139:7, ana maarifa/anajua yote (Omniscient, Intelligence), 1 Wakorinto 2:10-11, ni mwenye nguvu zote/wa umilele (Omnipotent), Mwanzo 1:2, ni Mtakatifu, Luka 11:13, ana hisia (Waefeso 4:30, Mwanzo 6:3) – Wala msimuhuzunishe Roho wa Mungu…, Roho yangu haitashindana na Mwanadamu milele, ana nia (will), 1Wakorinto 12:11 – Hutenda kazi kama apendavyo.

Kazi za Roho Mtakatifu
  • Kufundisha, Mwalimu (Yohana 14:26) … Atawafundisha yote…
  • Kuongoza, Kiongozi (Warumi 8:14, Yohana 16:13) – Atawaongoza awatie kwenye kweli yote, wote wanaoongozwa na Roho hao ndio … Mfano (Matendo ya Mitume 13:4, Acts 8:29)
  • Ni mfunuaji wa mambo/mafumbo/siri za Mungu (1Wakorinto 2:10) – Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote. Usipoteze muda kumtaka Mungu akufunulie siri zake, wewe mwambi Roho Mtakatifu hiyo ndiyo kazi yake.
  • Muombezi (Warumi 8:26) – Roho hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
  • Mtoa/mpasha habari za mambo yajayo (Yohana 16:13f) – Na mambo yajayo atawapasha habari yake.
  • Ni msemaji wa mambo ya Mungu/Yesu (Yohana 15:26, 2 Petro 1:21) – Yeye atanishuhudia (he will speak about me), Wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
  • Ni mtetezi/msemaji wa mambo yetu (Marko 13:11) – Kwa maana si ninyi msemao, bali ni Roho Mtakatifu.
  • Ni mkumbushaji wa yale uliyojifunza au uliyoagizwa na Mungu (Yohana 14:26)… Atawakumbusha yote niliyowaambia.
  • Kutia/kuwapa nguvu watu wake nguvu/uwezo (Matendo1:8) – Lakini mtapokea nguvu akisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu…
  • Kuuhakikisha (convict, make aware, sadikisha) ulimwengu kwa habari ya dhambi, haki na hukumu (Yohana 16:8) e.g unajuaje kwamba kuna hukumu? Warumi 8:16
Naam kazi hizi za Roho Mtakatifu zinatufikisha mahali pa kujua kwamba jukumu lake kubwa ni kuwa Msaidizi wa mwanadamu. Kufanyika msaada wa mwanadamu katika mambo hayo hapo juu pale mwanadamu atakapohitaji msaada huo. Hivyo ni jukumu lako kumpa nafasi kwa kuboresha mahusiano yako na yeye ili akusaidie. Hata hivyo Roho Mtakatifu kuitwa Msaidizi haina maana kwamba ndio umvunjie heshima, bali fahamu kwamba, Roho Mtakatifu ni Msaidizi kwa namna ambayo bila yeye mimi na wewe hatuwezi kutenda neno lolote.

Kazi hizi zinatupa kujua kwamba Roho Mtakatifu yupo tayari kutusaidia katika kila eneo la maisha yetu. Ni jukumu letu kumpa nafasi hiyo na kutambua kwamba bila msaada wake sisi hatuwezi lolote. Watu wengi leo hawaoni msaada wa Mungu kwao kwa sababu ya kutokumpa Roho Mtakatifu nafasi ya kuwasaidia katika maisha yao na pia kwa kutokujua maeneo ya kumtumia Roho Mtakatifu kama Msaidizi.

Je, unahitaji msaada wa Roho Mtakatifu eneo gani la maisha yako?, ni ndoa, kazi, madeni, huduma, kanisa, utawala nk mpe nafasi akusaidie, akufundishe na kukuongoza katika kweli yote. Kumbuka yeye ni Mungu ambaye ni Mwalimu na Kiongozi pasina yeye mimi na wewe hatuwezi neno lolote. Unataka kumjua Mungu, kuwa na maombi yenye matokeo mazuri na kufanikiwa katika maisha yako kiroho na kimwili pia mwambie Roho Mtakatifu akusaidie.

Msaada wa Roho Mtakatifu hauna mipaka maadam unahitaji msaada katika yale ambayo ni mapenzi ya Mungu. Hivyo haijalishi unapita katika jambo gani mpe nafasi Roho Mtakatifu akusaidie. Na ili uweze kuthamini msaada wa Roho Mtakatifu jifunze siku zote kufikiri kwa dhana kwamba bila msaada wake wewe huwezi lolote, na kwa sababu hiyo utaona umuhimu wa yeye kukusaidia katika maisha yako.

Usisubiri mambo yako yaharibike au usiachague mambo unayofikiri magumu ndio umshirikishe akusaidie, yeye anataka kuwa Bwana wa maisha yako, akusaidie kwa kila kitu hata mambo madogo kabisa kwenye maisha yako. Kina-muumiza Mungu kuona watoto wake chini ya jua wanahangaika katika maisha yao, wakati yeye amemleta Roho Mtakatifu ili awasaidie katika maisha hayo. Tumia vizuri fursa ya Roho Mtakatifu sasa maadam anapatikana, kuna wakati hatapatikana.

Neeme ya Kristo iwe Nawe!

Imeandikwa na Mwl. Patrick Sanga
0715 816800, 0755 81680

Kifo cha Padri Evarist Mushi, Jukwaa la kikristo Mbeya latoa Tamko.

JUKWAA la Kikristo Tanzania (TCF) katika Mkoa wa Mbeya, limetoa tamko la kuitahadharisha Serikali na kuitaka ichukue hatua za haraka za kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wote waliohusika na mauaji ya Padri, Evarist Mushi.

Akisoma tamko hilo mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliohudhuriwa na maaskofu, mapadri na wachungaji, Katibu wa Jukwaa hilo, Askofu Damianus Kongoro, alisema kuna mambo yanayotendeka waziwazi yakiwa na athari kubwa kwa amani na ustawi wa nchi na wananchi kwa jumla.

Alisema mambo hayo ni pamoja na uchochezi, kashfa, matusi na uchokozi wa wazi unaofanywa na baadhi ya watu wasiopenda amani lakini hakuna hatua za makusudi zinazochukuliwa na Serikali kuwashughulikia.

Askofu Kongoro alisema kuuawa kwa wachungaji, mapadri na maaskofu kuanza kutoa matokeo mabaya.

Alisema hatua zinazochukuliwa na Serikali haziridhishi wala kukidhi matakwa ya wananchi wapenda amani na badala yake, Serikali inakaa kimya au inachukua hatua ambazo kimsingi, hazitatui tatizo.


- Mwananchi -

Kanisa lachomwa Moto Zanzibar.

Taarifa za kuaminika Zilizorushwa na Radio Wapo katika kipindi chake cha Patapata leo asubuhi, ni kwamba watu wasiojulikana wamevamia kanisa moja linalojulikana kama SHALOM huko Zanzibar na kulirushia kitu kama bomu kilicholipuka moto japo majirani waliamka na kuuzima moto huo kabla haujaleta madhara makubwa.

Tukio hilo limetokea leo Alfajiri ya leo na Hakuna chombo cha dola kilichowahi kufika eneo hilo la tukio. Tukio hili limetokea ikiwa ni Siku chache tu baada ya Kuuliwa Padri Evarist Mushi kwa kupigwa Risasi huko huko Zanzibar.
Kwa Mujibu wa Kamishna wa Polisi wa Mjini Zanzibar Musa Ali Musa, kuna baadhi ya Vitu vya Kanisa hilo vimeungua.

Monday, February 18, 2013

Watu Watatu washikiliwa na Jeshi la Polisi kwa Mahojiano Juu ya Kifo cha Padri Evarist Mushi.

mushi
Marehemu Padri Evarist Mushi enzi za Uhai Wake
Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki, Parokia ya St. Joseph, Shangani, Unguja ameuwawa Jana mnamo saa moja asubuhi katika eneo la Beit-El-Ras karibu na kanisa la Katoliki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mohamed Aboud imeeleza kuwa kutokana na tokeo hilo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeliagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwatambua wale wote waliohusika na tukio hilo kwa ajili ya kuwachukulia hatua zinazofaa kwa mujibu wa sheria.

Aboud amesema kuwa wakati uchunguzi huo unaendelea, Serikali inawaomba wananchi wote kuwa watulivu na kuliachia Jeshi hilo la Polisi kutekeleza wajibu wake.

Aidha Serikali imetoa mkono wa pole kwa familia na wanafamilia wa marehemu pamoja na waumini wa kanisa hilo kuwa wastahamilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Wakati huo huo Raisi Jakaya Kikwete amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya kuuawa kwa Padri Evarist Mushi wa Parokia ya Minara Miwili ya Kanisa Katoliki mjini Zanzibar, mauaji yaliyotokea Zanzibar.

Rais Kikwete ametoa pole za rambirambi kwa Baba Askofu Augustino Shayo wa Jimbo Katoliki, Zanzibar, Maaskofu wote nchini na waumini wote wa Parokia ya Minara Miwili kwa msiba huo mkubwa uliowakuta.

Rais kikwete amemwambia Baba Askofu Shayo. ”Napenda kuwahakikishia kuwa tupo pamoja katika kuomboleza kifo cha Mpendwa Marehemu Padri Evarist Mushin a kuwa msiba huu ni wa kwetu sote.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Nimeligiza Jeshi la Polisi nchini kukusanya nguvu zake zote na maarifa yake yote kuhakikisha kuwa uchunguzi wa kina na wa haraka sana unafanyika ili kubaini mhusika ama wahusika na kuwakamata ili kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria.”

“Aidha, nimewaagiza Jeshi la Polisi washirikiane na vyombo vingine vya Usalama nchini na mashirika ya upepelezi ya nchi rafiki katika kufanya uchunguzi wa mauaji haya.”
Amesisitiza Rais Kikwete: “Nataka ukweli wake ujulikane ili kama kuna jambo lolote zaidi liweze kushughulikiwa na kukata mzizi wa fitina.”

Vile vile, Rais Kikwete amewataka waumini wa Kanisa katoliki na wananchi wote kuwa watulivu wakati Serikali inashughulikia suala hili na kuwa hakuna mtu wala watu ama kikundi cha watu kitachoruhusiwa kuvuruga amani ya nchi yetu.

WATU WATATU WASHIKILIWA NA POLISI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjnfyYrTkIHYZBrbeswwAAznTUERbZYwcmm9JXuy9m5xI7DYDm9OGdqczB7EbO6fqSutexpIhyphenhyphenF7Me66puAKZpXyKLi89iar4YGqyO9KfWZ8l_JNMgn_uHx5aKMT0qSao_5Zvduazll3o25/s1600/_DSC3465.JPG 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPoWQqtVodAGRn26XHWVtebs7hrs_ojXmboADVkWxv0wQugoFa4L_BJbqm2MeJPvbWXjezO7gYZW2uUoc04Nt64Rw-TshFPCzZ-yt5REw-PuRuSm0EOT5JkGcpKednr0FeDOu5ohM-tMEI/s1600/_DSC3469.JPG