Advertise Here

Tuesday, February 19, 2013

Kanisa lachomwa Moto Zanzibar.

Taarifa za kuaminika Zilizorushwa na Radio Wapo katika kipindi chake cha Patapata leo asubuhi, ni kwamba watu wasiojulikana wamevamia kanisa moja linalojulikana kama SHALOM huko Zanzibar na kulirushia kitu kama bomu kilicholipuka moto japo majirani waliamka na kuuzima moto huo kabla haujaleta madhara makubwa.

Tukio hilo limetokea leo Alfajiri ya leo na Hakuna chombo cha dola kilichowahi kufika eneo hilo la tukio. Tukio hili limetokea ikiwa ni Siku chache tu baada ya Kuuliwa Padri Evarist Mushi kwa kupigwa Risasi huko huko Zanzibar.
Kwa Mujibu wa Kamishna wa Polisi wa Mjini Zanzibar Musa Ali Musa, kuna baadhi ya Vitu vya Kanisa hilo vimeungua.