Advertise Here

Monday, February 18, 2013

Watu Watatu washikiliwa na Jeshi la Polisi kwa Mahojiano Juu ya Kifo cha Padri Evarist Mushi.

mushi
Marehemu Padri Evarist Mushi enzi za Uhai Wake
Padri Evarist Mushi wa Kanisa Katoliki, Parokia ya St. Joseph, Shangani, Unguja ameuwawa Jana mnamo saa moja asubuhi katika eneo la Beit-El-Ras karibu na kanisa la Katoliki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mohamed Aboud imeeleza kuwa kutokana na tokeo hilo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeliagiza Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwatambua wale wote waliohusika na tukio hilo kwa ajili ya kuwachukulia hatua zinazofaa kwa mujibu wa sheria.

Aboud amesema kuwa wakati uchunguzi huo unaendelea, Serikali inawaomba wananchi wote kuwa watulivu na kuliachia Jeshi hilo la Polisi kutekeleza wajibu wake.

Aidha Serikali imetoa mkono wa pole kwa familia na wanafamilia wa marehemu pamoja na waumini wa kanisa hilo kuwa wastahamilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Wakati huo huo Raisi Jakaya Kikwete amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya kuuawa kwa Padri Evarist Mushi wa Parokia ya Minara Miwili ya Kanisa Katoliki mjini Zanzibar, mauaji yaliyotokea Zanzibar.

Rais Kikwete ametoa pole za rambirambi kwa Baba Askofu Augustino Shayo wa Jimbo Katoliki, Zanzibar, Maaskofu wote nchini na waumini wote wa Parokia ya Minara Miwili kwa msiba huo mkubwa uliowakuta.

Rais kikwete amemwambia Baba Askofu Shayo. ”Napenda kuwahakikishia kuwa tupo pamoja katika kuomboleza kifo cha Mpendwa Marehemu Padri Evarist Mushin a kuwa msiba huu ni wa kwetu sote.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Nimeligiza Jeshi la Polisi nchini kukusanya nguvu zake zote na maarifa yake yote kuhakikisha kuwa uchunguzi wa kina na wa haraka sana unafanyika ili kubaini mhusika ama wahusika na kuwakamata ili kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria.”

“Aidha, nimewaagiza Jeshi la Polisi washirikiane na vyombo vingine vya Usalama nchini na mashirika ya upepelezi ya nchi rafiki katika kufanya uchunguzi wa mauaji haya.”
Amesisitiza Rais Kikwete: “Nataka ukweli wake ujulikane ili kama kuna jambo lolote zaidi liweze kushughulikiwa na kukata mzizi wa fitina.”

Vile vile, Rais Kikwete amewataka waumini wa Kanisa katoliki na wananchi wote kuwa watulivu wakati Serikali inashughulikia suala hili na kuwa hakuna mtu wala watu ama kikundi cha watu kitachoruhusiwa kuvuruga amani ya nchi yetu.

WATU WATATU WASHIKILIWA NA POLISI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjnfyYrTkIHYZBrbeswwAAznTUERbZYwcmm9JXuy9m5xI7DYDm9OGdqczB7EbO6fqSutexpIhyphenhyphenF7Me66puAKZpXyKLi89iar4YGqyO9KfWZ8l_JNMgn_uHx5aKMT0qSao_5Zvduazll3o25/s1600/_DSC3465.JPG 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPoWQqtVodAGRn26XHWVtebs7hrs_ojXmboADVkWxv0wQugoFa4L_BJbqm2MeJPvbWXjezO7gYZW2uUoc04Nt64Rw-TshFPCzZ-yt5REw-PuRuSm0EOT5JkGcpKednr0FeDOu5ohM-tMEI/s1600/_DSC3469.JPG