Advertise Here

Thursday, November 22, 2012

Noel Didas ndani ya Ujio Mpya wa "Nuru ya rohoni".

Noel Didas Shirima
 Noel Didas Shirima anayejulikana sana kama Noel Didas, ni mwimbaji wa Nyimbo za Injili toka mkoani Arusha, Tanzania mwenye albam 2 mpaka hivi sasa.

Akizungumza nami kwa Njia ya Simu katika Kipindi cha Gospel Sound kupitia Hhc Alive Fm ya Jijini Mwanza kinachoruka kila Siku za Jumamosi kuanzia Saa 8 Mchana – Saa 10 Jioni, Noel amesema ameshakamilisha albam yake Mpya ya 3 aliyoipa jina la Nuru ya Rohoni itakayotoka hivi karibuni.
Sowane Emmanuel akiwa katika Studio za Hhc Alive Fm
 Kwa mujibu wa Maelezo ya Noel, albam hiyo ina nyimbo 10 ambazo zote amerekodia katika Studio ya Christ Studios ya Jijini Arusha chini ya Producer Mtangoo. Baadhi ya Nyimbo zilizomo kwenye albam hiyo ni kama Furika Roho Mtakatifu, Uzuri wa Yesu, Kuna Kuinuka Tena, Nimechagua maneno yako na Ninataka Kuingia Mjini kwa Mungu.

Mbali ya hilo, Noel amesema pia yuko mbioni kufanya Video ya Albam yake ya Pili yenye Jina la Uniinue Viwango Vingine atakayoifanya na Kampuni ya Gospel Media ya Jijini Arusha. Albam hiyo ya Pili ina Nyimbo kama Jina lako Mtakatifu, Kuna Wakati Nashindwa, Nimekutana na Mwanamume, na Yesu ni Rafiki. Audio Albam hii ya Uniinue Viwango Vingine aliirekodia Jijini Mbeya katika Studio za High Pitch Records chini ya Producer Fredy Kameta.
Cover la Album ya Uniinue Viwango Vingine
 Mwezi wa 5 mwakani (2013) Noel anatarajia kufanya Live Recording Video ya Nyimbo za Kusifu na Kuabudu Jijini Mwanza akishirikiana na Waimbaji mbalimbali akiwemo Solomon Mukubwa. Video hiyo itajumuisha Nyimbo za Kusifu na Kuabudu zilizomo kwenye Albam zake zote 3, na Nyimbo Mpya za Kusifu na Kuabudu atakazoziongezea.

Audio Albam yake ya Pili anaisambaza yeye mwenyewe. Kwa Ushauri, Maoni, au kama utahitaji Albam hiyo tafadhali Wasiliana na Noel Didas mwenyewe ili akupe maelekezo ya Jinsi gani utapata Albam hiyo.

Noel Didas Shirima
0655 115990
0765 115990

Muswada wa kuwaapisha wanawake kuwa makasisi wapingwa Uingereza.

Mkuu wa kanisa la Anglikana duniani Rowan Williams
Mkuu wa kanisa la Anglikana duniani, Rowan Williams

KANISA la Anglikana nchini Uingereza limetupilia mbali uwezekano wa kuwaapisha wanawake kuwa makasisi huku kiongozi wa kanisa hilo akionesha wazi kusikitishwa na hatua hiyo.

Uamuzi huo umechukuliwa baada ya kupiga kura katika uchaguzi uliofanyika juzi nchini Uingereza na kushuhudia makasisi waliopiga kura wakiupinga muswada huo kwa asilimia 76.7 ya kura.

Uamuzi huo huenda ukaleta madhara makubwa katika kanisa hilo ambapo kulikuwa na matumaini makubwa ya kuboresha na kufanya marekebisho katika taasisi za kanisa hilo la Anglikana.

Kiongozi wa kanisa hilo duniani, Rowan Williams ambaye anamaliza muhula wake Desemba ijayo, amebainisha masikitiko yake kuona muswada huo unashindwa kupasishwa baada ya kupambana kwa muda wa miaka 10.

Wednesday, November 21, 2012

Sanamu ya Papa John Paul yazinduliwa Upya baada ya kuzua tafrani hapo awali.

Sanamu Mpya ya Papa Yohane
 Katika kile kinachooonekana kuwa ni marekebesisho ya makosa yao, Roma wamezindua upya sanamu ya Papa Yohane (John) Paul tarehe 19 Novemba, baada ya ile ya awali kushambuliwa na kuharibiwa na watu kwa madai ya kuwa haifanani katu na baba huyo mtakatifu, bali kama dikteta Benitto Mussolini.

Msanii ambaye amefanya kazi ya kuirekebisha, Oliviero Rainaldi amesema kwamba ameridhishwa na matokeo ya alichokifanya, kwani ndicho alichokuwa nacho kwenye mawazo yake.

Hapo awali baada ya kuzinduliwa mnamo 2011 mwezi Mei, mkosoaji kutoka Vatican alisema kwamba sanamu hiyo inaonekana kama vile bomu ndo limetua, na si Papa wetu mpendwa kama inavyotakiwa.

Sanamu kushoto ikiwa imeharibiwa, na kulia ikiwa baada ya marekebisho
Sandro Barbagallo anaendelea kusema kuwa baada sanamu hiyo kukosewa, na kwamba ni watu wachache walioweza kumtambua kama Papa, basi ilibidi haraka iwezekanavyo meya wa jiji la Rome akutane na wasanii wataalamu wa uchongaji, maofisa utamaduni na wanazuoni ili kuweza kuokoa jahazi. Na hapo ndipo michoro ya Rainaldi ilipopitiwa upya na kufanyiwa kazi ipasavyo, jambo ambalo sasa limefanikiwa, kwani Papa amewekewa tabasamu, na pia anaonekana kuwa na shingo tofauti na hapo awali ambapo kichwa chake kilifananishwa na tufe (mpira wa bowling).

Hata hivyo katika uzinduzi huo wa mara ya pili, wananchi siku zote hawakosi ya kusema, na mjenzi wa barabara mwenye umri wa miaka 54 akafunguka.

"Sasa hivi inapendeza, naona wamefanya kazi nzuri, sio kama ilivyokuwa mwanzoni, naona wamerekebisha uso, sasa nona tabasamu na pia shingo ipo. Kazi ni nzuri".

Lakini msafiri mmoja akasema aliyefahamika kama Alberto Donella amekuwa tofauti na wenzake, yeye akisema.

"Sio yeye, sio yeye kabisa, alikuwa mwenye furaha - sio kitu kama hiki" Alberto alisema alipokuwa akipita kando ya hilo sanamu na kuongeza, "Kwangu mimi hiki naona kama ni jokofu tu".

- Gospel Kitaa -

Tuesday, November 20, 2012

Dk. Malasusa: Viongozi wa dini kuweni mfano.

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk. Alex Malasusa
VIONGOZI wa dini wametakiwa kuwa mfano katika maeneo wanayoyaongoza ili kuendelea kudumisha amani  kwa ajili ya ustawi wa nchi.

Rai hiyo ilitolewa juzi na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk. Alex Malasusa, alipokuwa akihubiri katika  ibada ya kumweka wakfu, Askofu wa Dayosisi ya Dodoma, Amon Kinyunyu.

Dk. Malasusa alisema Serikali imetoa uhuru wa kuabudu hivyo viongozi wasiposimamia amani iliyopo watahatarisha uhuru uliopo wa kuabudu.

 “Kwa sasa hivi tunaona vurugu zinazosababisha kufyatuliwa kwa mabomu ya machozi, hatupendi kuona risasi za moto zinatumika kwa kuwa wakati huo itakuwa ni vigumu kupata muda wa kuabudu,” alisema.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Rehema Nchimbi, ambaye aliiwakilisha serikali, alisema  viongozi wa dini wasibadilike, wahubiri amani na sio vurugu.

Dk. Rehema Nchimbi alisema serikali haina dini ila imetoa uhuru wa kila mwananchi kuabudu dini anayoitaka bila kuingiliwa uhuru wa mtu mwingine.

Aliwataka viongozi wa dini kumwogopa  Mungu aliyewaweka katika nafasi hizo na kuwasaidia katika kufanya mema.

Kwa upande wake, Askofu Kinyunyu aliwaomba waumuni wa Kanisa hilo kujikita katika kuendeleza mema yaliyoanzishwa na Askofu aliyemaliza muda wake, Festo Ngowo.

Alisema Askofu Ngowo alianzisha ujenzi wa ofisi za Dayosisi hiyo, ujenzi wa shule ya sekondari na miradi mingine mbalimbali ya Kanisa hilo.

Askofu Kinyunyu alichaguliwa kushika nafasi hiyo baada ya Askofu Ngowo kuugua kwa zaidi ya miaka miwili.

 Kwa mujibu wa taratibu za KKKT, inapotokea askofu akaugua zaidi ya muda huo, askofu mwingine huchaguliwa kuchukua nafasi hiyo.

- Nipashe -

Monday, November 19, 2012

R.I.O.T Presents Men's Conference from 19-25/Nov/2012 in Dar es Salaam.


Righteous Invasion of Truth (R.I.O.T) gladly brings ‘Men of Valor’, its first men’s conference in Dar es Salaam. M.O.V. is an interactive platform, reaching out to men across different ethnic groups, socioeconomic and religious backgrounds to restore, transform, equip and edify the man holistically.

Men have a natural tendency of internalizing issues. When you ask a man what he is thinking when things are up to his neck, without a glance, he’ll instinctively say, “Nothing”. Men do cry, but their tears are only visible from the inside. That’s why God had to say, “It is not good for a man to be alone”. As much as studies show that women are twice as much susceptible to depression, surprisingly the male-to-female ratio for completed suicides is greater than 4:1

When in this state where the internalization of things has reached its limit, men tend to shift the blame for how they feel on the inside to outside things. We exhibit anger or irritability over everything. Men are more prone to using alcohol or drugs as an outlet. As if this isn’t enough, the male infant has a higher mortality rate than the female. Let alone the fact that the woman has a higher life expectancy rate.

To those that have overcome these obstacles, there is still no rest for them. The enemy has strategically planned to emasculate the ‘man’ figure from marriage, family and even the society at large. The ‘man’ as an authority figure is being undermined from his God-given position bestowed upon him from Genesis by God Himself.

How can men prevail this ongoing fierce battle?  If only we could learn the greatest ‘Art of War’ – PRAISE!  You might be the least in your father’s house or perhaps you are coming from the poorest family in your clan, but I clearly hear the Commander-in-Chief of the Army of The Lord saying this to you: “Jehovah is with you, Mighty Man of Valor”!

The Event will be conducted at Makumbusho Hall near Institute of Finance(IFM)
From 19th-25/Nov/2012
Time:5;30Pm - 8:30Pm

We welcome you all Men and Women!

Saturday, November 17, 2012

Video ya "U Mwema" ya Felix Mshama, Noel Mlabwa na Barnabas Shija.


Kuanzia kushoto ni Felix Mshama, Noel Mlabwa, na Barnabas Shija

KWA wahudhuriaji wa Event nyingi sana za Injili za Jijini Mwanza, hizi sura pamoja na majina yatakuwa sio mageni kwao. Hawa ni Vijana toka Jijini Mwanza ikiwa ni Mazao ya Tanzania Fellowship of Evangelical Students(TAFES) katika Chuo Kikuu cha Mt. Agustino cha Jijini Mwanza.

Safari yao ya Uimbaji ilianzia mbali kidogo, kila mmoja akiwa na historia yake, lakini kukutana kwao TAFES Saut, kuna tengeneza historia nyingine ya vijana hawa katika kumtumikia Mungu, na safari hii ni katika wimbo wao mpya wa "U Mwema".

Wakiwa katika studio za Makaya records za Jijini Mwanza, vijana hawa wanapata Idea ya kufanya wimbo kwa kutumia Acoustic Guitar, chombo kilichopigwa na Felix Mshama toka Mwanzo wa wimbo mpaka mwisho.

Tofauti na Utengenezaji wa Video tuliouzoea kwamba inaanza audio halafu ndo inafuata video, utengenezaji wa video hii ilianza Video kisha Audio ndo ikafuata kwa kutengenezwa katika Studio za Makaya Records.

Video Producer wa Wimbo huu akiwa ni Wynjones Kinye toka Kinye Media ndo aliyehakikisha Video hii ina ubora wa kutosha huku rangi ya video hii ikiwa ni ya tofauti na rangi za kawaida tulizozizoea kuziona kwenye video nyingine.

WASIFU WAO
Barnabas Shija
  • Aliwahi kuwa Praise leader wa Tafes mkoa wa Mwanza(2010/2011).
  • Ni mmoja wa waimbaji waliofanya Back up katika Event ya Jehovah Yu Hai tour katika Mkoa wa Mwanza.
  • Alishawahi kurekodi audio albam ambayo hakuitoa kutokana na Sababu za Ubora wa Kazi.
  • Kwasasa anahudumu katika Praise Team ya Kanisa la FPCT la kurasini Jijini Dar es salaam.
  • Graphic Designer (Banners na Posters)
  • Kitaaluma ni mhitimu wa BA. Mass Communication (2012), SAUT-Mwanza.
 
Felix Mshama
  • Mpiga Gitaa aina ya Acoustic na Bass.
  • Aliwahi kuwa Mwalimu wa kwaya ya Caanan Anglican ya mkoani Dodoma akiwa na umri wa Miaka 18.
  •  Kitaaluma ni Mwanasheria (LLB, Saut-Mwanza, 2012)

Noel Mlabwa
  •  Mwimbaji wa Gospel Band ya Kingdom worshipers ya jijini Mwanza.
  • Mpiga Drums mwenye mapenzi sana na mahadhi ya kikongo.
  • Mwanasheria mwanafunzi Mwaka wa 4, Saut-Mwanza.
Wasiliana Nao, Kwa Namba zifuatazo;
0717 642263
0716 093245
0719 995061

Sasa itazame Video hiyo iliyopewa jina la "U Mwema"

Mapadre wa Kanisa Katoliki Iringa wavamiwa na kujeruhiwa vibaya.

PAROKO wa Kanisa Katoliki Parokia ya Isimani, wilayani Iringa Angelo Burgeo (60) na msaidizi wake Herman Myalla (36) wamenusurika kufa baada ya kuvamiwa na majambazi waliokuwa na silaha za moto, mapanga na nondo.
Picture
Paroko Angelo Burgeo
 Mbali na kupigwa risasi katika ubavu wake wa kushoto na kujeruhiwa vibaya katika tukio hilo lililotokea majira ya 4.45 usiku wa kuamkia jana, Padri Burgeo alijeruhiwa vibaya nyuma ya kichwa chake baada ya kupigwa na nondo.

Akizungumza na wanahabari katika hospitali ya mkoa wa Iringa ambako viongozi wamelazwa kwa ajili ya matibabu, Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Faustine Gwanchele alisema Padri Myalla amejeruhiwa vibaya kichwani baada ya kupigwa kwa panga na nondo.
Picture
Msaidizi wa Paroko, Bw. Herman Myalla
 "Walifikishwa majira ya saa sita usiku wa kuamkia jana, na wakaanza kupatiwa matibabu wanayoendelea nayo mpaka sasa," alisema na kuongeza kwamba Padri Bergeo alianza kufanyiwa upasuaji jana ili kuondoa vipande vya risasi vilivyopo ndani ya mwili wake.

Tukio hilo limetokea ikiwa siku moja tu baada ya mlinzi wa Kanisa Katoliki Kihesa Iringa Mjini, Bathelomeo Nzigilwa (64) kujeruhiwa vibaya na majambazi waliovunja kanisa hilo na kufanikiwa kuiba mali mbalimbali zikiwemo fedha taslimu zaidi ya Sh 500,000.

 Dk Gwanchelle alisema hali ya Nzigilwa ni mbaya kwasababu majambazi waliomjeruhi walimvunja mfupa wa sehemu ya nyuma ya kichwa chake.

Friday, November 16, 2012

Kanisa Katoliki Parokia ya Kihosa lavamiva. Mlinzi ajeruhiwa vibaya.

Muonekano wa Nje wa Kanisa Katoliki Porokia ya Kihesa
WATU wasiofahamika usiku wa kuamkia Jana wamevamia Kanisa Katoliki Parokia ya Kihesa Jimbo la Iringa, Mkoani Iringa na kuiba baadhi ya mali huku mlinzi wa Kanisa hilo Bathlomeo Nzigilwa akijeruhiwa vibaya na kulazwa katika Hospitali ya Mkoa.
 
Akizungumzia tukio hilo Sista Lucy Grace Mgata amesema aligungua kuwa kunauvamizi majira ya  alfajiri alipofika kanisani hapo kwa ajili ya ibada ya Misa za kila siku zinazoanza saa 12:00 asubuhi.

“Mimi nilifika hapa kanisani saa 11:40 alfajiri, na nilipofungua mlango wa kanisa kwa ajili ya misa nilishangaa mlango ukiwa wazi na kumuona  mlinzi amekaa kwenye kiti huku kichwa chake kikiwa kimeinamishwa chini na kufunikwa kofia, nilijua amelala kumbe alikuwa ameumizwa na hajitambui," Alisema Sista Mgata. 
Ndani ya Ofisi baada ya Uharibifu
Amesema  alipomsogelea mlinzi huyo aliona damu inatiririka chini na mwili wake ukiwa umelowa kwa damu na hapo ndipo alipokwenda kugonga nyumba ya padre kutoa taarifa.

Pamoja na kuvunjwa kwa Kanisa hilo ofisi ya parokia nayo ilivunjwa huku vitabu, na kumbukumbu mbalimbali zikiwa zimechanwa na kuwa mavazi ya ibada na vifaa mbalimbali vya ibada vimeharibiwa vibaya,  Taberenakulo ndogo nayo ikiharibiwa, msalaba kuvunjwa pamoja na Hostia Takatifu zikimwagwa kila mahali.

Damu zilizovuja baada ya mlinzi kupigwa
Sista Mgata  amesema hela za watumishi wa Artare walizokuwa wakichangishana pamoja na fedha za chama cha kitume cha utume wa Fatima zimechukuliwa japo bado hazijajulikana ni kiasi gani.

“Pia wamechukua hela ambazo watumishi wa artare walikuwa wakichangishana kwa ajili ya matumizi ya umoja wao, na fedha za chama cha kitume cha utume wa Fatima nazo wamechukua ingawa sijajuwa ilikuwa ni kiasi gani mpaka wao wenyewe waje waeleze kulikuwa na shilingi ngapi," Alisema sista Mgata.
Muuguzi mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa Rustica Tung'ombe akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya mlinzi aliyeumizwa na kufukishwa hospitalini hapo leo
 Kwa upande wake Katekista Agustino Luhama mhudumu wa ofisi ya Parokia alisema hela anazozikumbuka kwa harakaharaka ambazo zimechukuliwa na wavamizi hao ni zaidi ya shilingi laki tano.

“Hela ninazozikumbuka kwa harakaharaka ambazo zimechukuliwa ni zaidi ya shilingi laki tano lakini zingine sijapata idadi kwa sababu nilikuwa sijazijumlisha na zingine nilizipokea jana kutoka kwa waamini mbalimbali” alisema Kat. Luhama.

Padre Aloyce Mdemu ambaye pia ni Makamu wa Askofu wa jimbo hilo alisema bado ni mapema kujua thamani ya uharibifu uliofanyika kwa kuwa bado wanaendelea na uchunguzi wa vifaa vingine na maeneo mengine ambayo huenda hayajagundulika.
Mlinzi aliyejeruhiwa akiwa hospitali
“Ni kweli tukio hili limetokea na kutushtua sana hata kuumizwa nuzura kuuawa mlinzi wetu lakini bado ni pame sana kujua thamani ya uharibifu wa vitu vyote vilivyoharibiwa kwa sababu tunaendelea na uchunguzi wa vitu vingine na maeneo mengine ambayo huenda nayo yameharibiwa na hayajajulikana. Tutakapokuwa tumekamilisha, taarifa zitatolewa” alisema Pd. Mdemu.

Hata hivyo Muuguzi mfawidhi wa hospitali ya Mkoa wa Iringa Rustica Tung’ombe alikiri kumpokea majeruhi ambaye ni mlinzi wa kanisa hilo na kusema kuwa hali yake ni mbaya japo kuwa anaendelea kupatiwa matibabu.

“Tumempokea majeruhi Bathlomeo Nzigilwa mlinzi wa Kanisa ambaye ni mkazi wa kwa Semtema akiwa na hali mbaya, na bado hajapata ufahamu, ila anaendelea na matibabu,” alisema Tung’ombe.

Thursday, November 15, 2012

Semina ya Neno la Mungu katika Kanisa la New Vine International Ministries.

 KANISA la New Vine International Ministries lililopo maeneo ya Nyegezi Jijini Mwanza Chini ya Mpakwa Mafuta wa Bwana Pastor Goodluck Kyara, wanakuletea Semina kubwa ya Neno la Mungu iliyopewa Jina la "Siku 8 za Ushindi na Mafanikio".

Somo kuu katika Semina hiyo linatoka katika Kitabu cha Warumi 8:29-30 likiwa na Kichwa kinachosema "Umezaliwa Kushinda".

Semina hiyo itaanza rasmi Novemba 18 mpaka Novemba 25, kuanzia Saa 9:00 Jioni - Saa 12:00 Jioni. Ukumbi ni pale pale Kanisani maeneo ya Nyegezi karibu kabisa na Sheli ya Mafuta ndani ya Tema Hotel.

Watumishi wa Mungu mbalimbali kutoka ndani na Nje ya Tanzania watahudumu. Baadhi yao ni Mchungaji Kiongozi wa New Vine International Ministries Pastor Goodluck Kyara, Apostle Prince Mulangila(South Africa) na Apostle Paul Njoroge kutoka Nchini Kenya.

Kwa Maelezo zaidi, Piga Simu Namba;
+255 754 435 951

Watu wote mnakaribishwa!

Monday, November 12, 2012

Kilichofanyika Jana katika Tafes Jointmass Mkoa wa Mwanza, ndani ya Bugando University.

BAADA ya kutoka Chuo cha Ualimu Butimba(Butimba TTC) wiki chache zilizopita, Jana shughuli nzima ya Jointmass ilihamia Chuo Kikuu cha Bugando ambapo Wanafunzi toka Matawi yote ya Tafes Mwanza walikutana pale.
With his Presence
Vikundi mbalimbali vya Uimbaji vya Praise and Worship vilihudumu, pamoja na waimbaji binafsi pia walipata nafasi ya kuhudumu.
Sema na Moyo wako.................... (Ruth Lyanga)
Moja ya Vitu vilivyopewa nafasi kwa Siku ya Jana, ni "TAFES AWARENESS", Mada iliyowakilishwa na Tafes Staff(Former Reginal Coordinator) Dada Upendo Mwangoka. Kati ya Mengi aliyoyazungumza, pia alieleza historia ya Tafes na Kazi zake pia.
Dada Upendo Mwangoka
Kwa Upande wa Chakula cha Kiroho, Neno lilifundishwa na Mwl. Gilbert Ezekiel likiwa na Kichwa cha Somo kisemacho; "Nguvu iliyoko katika Ufahamu" na tukapitia Mistari ifuatayo; Yoh 8:31-32, Yoh 1:11, Mithali 8:9 na Waefeso 3:20.
Mwl. Gilbert Ezekiel
Wanafunzi wakifuatilia somo kwa Makini
Kusifu na Kuabudu pia kulipewa nafasi ya kutosha sana ili kushusha Uwepo wa Mungu mahali pale.
Tafes Praise Team
 Upande wa pili mambo yakawa hivi.........
Pipooooooooooooooo................!!!
Mpaka chini, Mpaka chini..................!(Ester Denisy)
Sephone Sospeter(Kwenye Keyboard) na Mutu ya watu Felix Mshama(Kwenye Guitar)
 Maombi pia yalikuwepo wa watu mbalimbali waliokuwa na Uhitaji.
Baadhi ya watu waliofanyiwa Maombi
Mungu na akupe Neema ya kutambua Nguvu iliyoko katika Ufahamu.

Sunday, November 11, 2012

Askofu Anglikana ataka wacheza kamari watoe Sadaka.

Askofu Justin Welby

ASKOFU Justin Welby, aliyeteuliwa kuwa Askofu Mkuu wa kanisa la Anglikana, yaani Askofu wa Canterbury, amependekeza kwenye mtandao wa Twitter kwamba mtu yeyote aliyeshinda kwenye kamari kwa kubahatisha kuwa yeye ndiye atateuliwa, anafaa kutoa fedha hizo kama sadaka kwa kanisa.

Mwanzo wa juma hili makampuni ya kamari yalitangaza kuwa yamesimamisha kamari juu ya nani atakuwa kiongozi mpya wa kanisa la Anglikana, kwa sababu wengi walifikiri kuwa ni Askofu Welby, ambayo inaonesha baadhi ya maafisa wakijua kuwa jina hilo ndilo lilopendekezwa.

Askofu Welby atachukua nafasi ya Rowan Williams mwaka ujao kuwa kiongozi wa wamumini wa Kianglikana dunia nzima.

- BBC Swahili -

Saturday, November 10, 2012

Jotta A, Mwimbaji Mtoto wa Nyimbo za Injili toka Nchini Brazil.


ALIZALIWA Mnamo mwaka 1997 Nchini Brazil. Akiwa na Umri wa kama miaka minne hivi ndipo talent yake ikaanza kuonekana.

Jina lake ni Jotta A, mwimbaji wa Nyimbo za Injili toka Brazil. Kwasasa ana umri wa Miaka 15 tu lakini kile anachokifanya ni zaidi ya Umri wake.

Tumia muda wako kutazama video hii ambayo Jotta A ameimba na Mwimbaji nguli wa Muziki wa Injili Donnie MCclurkin alipokuwa Nchini Brazil.

Kama kungekuwa na Maajabu 7 ya Dunia katika Muziki wa Injili basi Jina la Jotta A lisingekosa kwenye Orodha. Hebu Tazama pia Video hii hapa

Friday, November 9, 2012

Mwili wa Marehemu Askofu Aloysius Balina.

Mwili wa Marehemu Askofu Aloysius Balina ukiwa ndani ya Jeneza
Jeneza lililokuwa na Mwili wa Marehemu Askofu Aloysius Balina
- Picha zote na Elia Migongo =

Wednesday, November 7, 2012

Msiba wa Mhashamu Askofu Aloysius Balina wa Mkoani Shinyanga.

Askofu Balina enzi za Uhai wake
ASKOFU wa Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga, Mhashamu Aloysius Balina, amefariki dunia jana katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Antony Makunde, imesema kuwa Askofu Balina alifariki jana mida ya Saa 5 Asubuhi, kutokana na maradhi ya saratani ya ini yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.

Padre Makunde alisema kuwa, mapema mwaka huu, Askofu Balina alipelekwa Ujerumani kwa matibabu, na akarejea nchini akiwa mwenye afya njema.

Hata hivyo, miezi michache alianza tena kusumbuliwa na ugonjwa huo, na afya yake ilizidi kudorora ambapo mwezi uliopita, alilazwa katika Hospitali ya Bugando kabla ya kufikwa na umauti jana.

Askofu Balina alizaliwa Juni 21,1945, Ntuzu, Bariadi mkoani Shinyanga. Baada ya kuhitimu masomo yake mbalimbali, alipewa daraja la upadri Mei 26, 1971.

Kutokana na utumishi wake mwema, Baba Mtakatifu Yohane Paulo II alimteua kuwa askofu wa Jimbo la Geita mwaka 1985. Septemba 1997, aliteuliwa kuwa askofu wa Jimbo la Shinyanga ambako alilitumikia hadi jana alipoitwa na Mungu.

Wakati wa uhai wake, Askofu Balina alishikilia nafasi kadhaa ndani ya Baraza la Maaskofu ambako kwa miaka mingi alikuwa mwenyekiti wa idara ya afya ya baraza hilo, na Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Bugando.

Askofu Balina ni mmoja wa maaskofu wachache wa Kikatoliki ambaye alitazama maisha ya waamini wake na watu wote wa majimbo ya Geita na Shinyanga, katika mahitaji yote ya kiroho na kimwili.

Aidha, ni mmoja wa viongozi wa dini aliyesimamia kikamilifu kuinua Hospitali ya Bugando na hasa juhudi zake zilizosukuma kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Afya Bugando.

Kadhalika, alifanya kazi kubwa akishirikiana na maaskofu wenzake, kuhakikisha kuwa kinaanzishwa Chuo Kikuu cha Mt. Augustine, na hatimaye kufikia mafanikio makubwa.

Salamu za Rambirambi toka kwa Rais Jakaya Kikwete kwa Kanisa Katoliki Tanzania.
Askofu Balina(Kushoto) enzi za Uhai wake akiwa na Rais Jakaya Kikwete
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete jana Jumanne, Novemba 6, 2012, amelitumia Kanisa Katoliki Tanzania salamu za rambirambi kuomboleza kifo cha Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga, Mhashamu Baba Askofu Aloysius Balina aliyefariki dunia majira ya saa tano asubuhi leo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Bugando, Mwanza.
 
Katika salamu zake za rambirambi kwa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Mshahamu Baba Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Rais Kikwete amesema: “Nimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha Mhashamu Baba Askofu Aloysius Balina ambaye nimeambiwa ameaga dunia asubuhi ya leo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Buganda, Mwanza, kwa ugonjwa wa kansa.”
 
Amesema Rais Kikwete katika salamu zake hizo: “Mhashamu Baba Askofu Balina alikuwa kiongozi hodari na mwadilifu ambaye siyo tu alichangia kipekee katika mwenendo mzuri wa kiroho wa waumini wa Kanisa Katoliki bali pia katika maendeleo ya Watanzania wote kwa jumla.”
 
“Kifo chake kimetuondolea kiongozi mwema ambaye tutazikosa busara zake na uongozi wake. Lakini napenda kukuhakishia Mshahamu Baba Askofu kuwa sisi ndani ya Serikali tutaendelea kutambua na kuthamini mchango wa Askofu Balina alioutoa kwa nchi yetu katika maisha yake,” amesema Rais Kikwete na kuongeza:
 
“Baba Askofu, nakuomba upokee salamu za rambirambi za Serikali ninayoiongoza na zangu binafsi kufuatia msiba huu mkubwa. Aidha, kupitia kwako, naomba uwafikishie salamu zangu viongozi na waumini wote wa Kanisa Katoliki kwa kuondokewa na kiongozi na muumini mwenzao. Naungana nanyi kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, aiweka pema peponi roho ya Marehemu. Amen.”

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
6 Novemba, 2012

Sunday, November 4, 2012

Ibada ya leo katika Kanisa la Hosanna Christian Center Mission.

Samuel Sasali akiwa madhabahuni
 BAADA ya kumaliza Semina iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Mt. Augustino, Samuel Sasali leo akaenda kuhudumu katika Kanisa la Hosanna Christian Center Mission lililopo maeneo ya Kilimahewa Jijini Mwanza, chini ya Mtumishi wa Bwana Bishop Irene Nzwalla.
Sehemu ya Waumini
Waumini wakifuatilia Mafundisho
Kichwa cha Somo la leo kilikuwa ni "Kutembea katika Uwepo wa Mungu" na Somo hili lilitoka katika Kitanu cha 1 Samwel 4:1-8.
Ibada ikisonga mbele
Halleluyah..............!!!
Kabla ya Neno Hosanna Praise Team chni ya Music Director(MD) Adolph Robert Nzwalla ilihakikisha Uwepo wa Mungu unakuwa Kanisani pale.
MD na Mtangazaji wa Alive Fm Adolph Robert Nzwalla akishusha uwepo wa Bwana
Kushoto ni Mtangazaji wa Alive Fm, Joel Kaema
Hosanna Praise Team
Maombi pia yalipewa nafasi ya kutosha sana.
Mchungaji Kiongozi Bishop Irene Nzwalla
Maombi ya Fungu la Kumi
 Kisha Mchungaji Kiongozi wa Hosanna Christian Center Mission akamkaribisha Mtumishi wa Mungu Samuel Sasali kwa ajili ya kutoa Ujumbe wa leo.
Samuel Sasali na Bishop Irene
Hapa Injili Ikaanza
Moja ya vitu vilivyofundishwa leo, ni Namna ya kutembea na Uwepo wa Mungu, ambapo Mtumishi Samuel Sasali alitaja Mambo matatu ya Msingi;

1. Kusoma Neno la Mungu na kuliishi

2. Maombi

3. Jitabirie (Jinenee yaliyo Mema)
Bishop Irene akinukuu Mambo ya Msingi
Waacheni watoto wadogo waje kwangu, kwa maana..............
 Hapa Somo likakolea zaidi
Ameeeeeeeeeeeeeeeen!
Ruth Lyanga(Kushoto) na Monica(Kulia)
 Hapa Nanukuu, "Usiwe na Imani ya Chekechekea, lazma ifike Mahala uwe na Imani ya Chuo Kikuu". Akimaanisha watu tusiwe na Imani legelege.
Tumeelewana watu wa Mungu???
Kisha Mama akakazia Maarifa baada ya Neno
 Leo tunamaliza na hawa watoto ambao walionyesha uwezo wao katika Kumsifu Bwana.
Watoto wakimsifu Bwana

Mungu akubariki sana!