Advertise Here

Thursday, November 22, 2012

Noel Didas ndani ya Ujio Mpya wa "Nuru ya rohoni".

Noel Didas Shirima
 Noel Didas Shirima anayejulikana sana kama Noel Didas, ni mwimbaji wa Nyimbo za Injili toka mkoani Arusha, Tanzania mwenye albam 2 mpaka hivi sasa.

Akizungumza nami kwa Njia ya Simu katika Kipindi cha Gospel Sound kupitia Hhc Alive Fm ya Jijini Mwanza kinachoruka kila Siku za Jumamosi kuanzia Saa 8 Mchana – Saa 10 Jioni, Noel amesema ameshakamilisha albam yake Mpya ya 3 aliyoipa jina la Nuru ya Rohoni itakayotoka hivi karibuni.
Sowane Emmanuel akiwa katika Studio za Hhc Alive Fm
 Kwa mujibu wa Maelezo ya Noel, albam hiyo ina nyimbo 10 ambazo zote amerekodia katika Studio ya Christ Studios ya Jijini Arusha chini ya Producer Mtangoo. Baadhi ya Nyimbo zilizomo kwenye albam hiyo ni kama Furika Roho Mtakatifu, Uzuri wa Yesu, Kuna Kuinuka Tena, Nimechagua maneno yako na Ninataka Kuingia Mjini kwa Mungu.

Mbali ya hilo, Noel amesema pia yuko mbioni kufanya Video ya Albam yake ya Pili yenye Jina la Uniinue Viwango Vingine atakayoifanya na Kampuni ya Gospel Media ya Jijini Arusha. Albam hiyo ya Pili ina Nyimbo kama Jina lako Mtakatifu, Kuna Wakati Nashindwa, Nimekutana na Mwanamume, na Yesu ni Rafiki. Audio Albam hii ya Uniinue Viwango Vingine aliirekodia Jijini Mbeya katika Studio za High Pitch Records chini ya Producer Fredy Kameta.
Cover la Album ya Uniinue Viwango Vingine
 Mwezi wa 5 mwakani (2013) Noel anatarajia kufanya Live Recording Video ya Nyimbo za Kusifu na Kuabudu Jijini Mwanza akishirikiana na Waimbaji mbalimbali akiwemo Solomon Mukubwa. Video hiyo itajumuisha Nyimbo za Kusifu na Kuabudu zilizomo kwenye Albam zake zote 3, na Nyimbo Mpya za Kusifu na Kuabudu atakazoziongezea.

Audio Albam yake ya Pili anaisambaza yeye mwenyewe. Kwa Ushauri, Maoni, au kama utahitaji Albam hiyo tafadhali Wasiliana na Noel Didas mwenyewe ili akupe maelekezo ya Jinsi gani utapata Albam hiyo.

Noel Didas Shirima
0655 115990
0765 115990