Advertise Here

Sunday, November 4, 2012

Ibada ya leo katika Kanisa la Hosanna Christian Center Mission.

Samuel Sasali akiwa madhabahuni
 BAADA ya kumaliza Semina iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Mt. Augustino, Samuel Sasali leo akaenda kuhudumu katika Kanisa la Hosanna Christian Center Mission lililopo maeneo ya Kilimahewa Jijini Mwanza, chini ya Mtumishi wa Bwana Bishop Irene Nzwalla.
Sehemu ya Waumini
Waumini wakifuatilia Mafundisho
Kichwa cha Somo la leo kilikuwa ni "Kutembea katika Uwepo wa Mungu" na Somo hili lilitoka katika Kitanu cha 1 Samwel 4:1-8.
Ibada ikisonga mbele
Halleluyah..............!!!
Kabla ya Neno Hosanna Praise Team chni ya Music Director(MD) Adolph Robert Nzwalla ilihakikisha Uwepo wa Mungu unakuwa Kanisani pale.
MD na Mtangazaji wa Alive Fm Adolph Robert Nzwalla akishusha uwepo wa Bwana
Kushoto ni Mtangazaji wa Alive Fm, Joel Kaema
Hosanna Praise Team
Maombi pia yalipewa nafasi ya kutosha sana.
Mchungaji Kiongozi Bishop Irene Nzwalla
Maombi ya Fungu la Kumi
 Kisha Mchungaji Kiongozi wa Hosanna Christian Center Mission akamkaribisha Mtumishi wa Mungu Samuel Sasali kwa ajili ya kutoa Ujumbe wa leo.
Samuel Sasali na Bishop Irene
Hapa Injili Ikaanza
Moja ya vitu vilivyofundishwa leo, ni Namna ya kutembea na Uwepo wa Mungu, ambapo Mtumishi Samuel Sasali alitaja Mambo matatu ya Msingi;

1. Kusoma Neno la Mungu na kuliishi

2. Maombi

3. Jitabirie (Jinenee yaliyo Mema)
Bishop Irene akinukuu Mambo ya Msingi
Waacheni watoto wadogo waje kwangu, kwa maana..............
 Hapa Somo likakolea zaidi
Ameeeeeeeeeeeeeeeen!
Ruth Lyanga(Kushoto) na Monica(Kulia)
 Hapa Nanukuu, "Usiwe na Imani ya Chekechekea, lazma ifike Mahala uwe na Imani ya Chuo Kikuu". Akimaanisha watu tusiwe na Imani legelege.
Tumeelewana watu wa Mungu???
Kisha Mama akakazia Maarifa baada ya Neno
 Leo tunamaliza na hawa watoto ambao walionyesha uwezo wao katika Kumsifu Bwana.
Watoto wakimsifu Bwana

Mungu akubariki sana!