Advertise Here

Thursday, November 15, 2012

Semina ya Neno la Mungu katika Kanisa la New Vine International Ministries.

 KANISA la New Vine International Ministries lililopo maeneo ya Nyegezi Jijini Mwanza Chini ya Mpakwa Mafuta wa Bwana Pastor Goodluck Kyara, wanakuletea Semina kubwa ya Neno la Mungu iliyopewa Jina la "Siku 8 za Ushindi na Mafanikio".

Somo kuu katika Semina hiyo linatoka katika Kitabu cha Warumi 8:29-30 likiwa na Kichwa kinachosema "Umezaliwa Kushinda".

Semina hiyo itaanza rasmi Novemba 18 mpaka Novemba 25, kuanzia Saa 9:00 Jioni - Saa 12:00 Jioni. Ukumbi ni pale pale Kanisani maeneo ya Nyegezi karibu kabisa na Sheli ya Mafuta ndani ya Tema Hotel.

Watumishi wa Mungu mbalimbali kutoka ndani na Nje ya Tanzania watahudumu. Baadhi yao ni Mchungaji Kiongozi wa New Vine International Ministries Pastor Goodluck Kyara, Apostle Prince Mulangila(South Africa) na Apostle Paul Njoroge kutoka Nchini Kenya.

Kwa Maelezo zaidi, Piga Simu Namba;
+255 754 435 951

Watu wote mnakaribishwa!