Advertise Here

Friday, March 8, 2013

Kutana na Goodluck Gozbert a.k.a Goody.

Goodluck Gozbert a.k.a Goody ni Mwimbaji wa Nyimbo za Injili toka Mkoani Mwanza, Tanzania ambako ndiko alikozaliwa. Goodluck alizaliwa April 12, Mwaka 1991 katika hospitali ya Bugando, Mwanza. Akiwa ni Mtoto pekee wa Bw. Gozbert Rweyemamu pamoja Janeth Gozbert, Goodluck alilelewa na Mama yake pekee baada ya Baba yake mzazi kufariki huku Goodluck akiwa na Umri wa Mwaka 1.
 
Goody anasema alianza kazi za uimbaji Mwaka 2005 akiwa na Tumaini Choir (K.K.K.T- Imani Mwanza). Baada ya Miaka 3 yaani 2008, Goody alianza kuimba nyimbo zake pekeyake huku akiwa bado ni miongoni mwa waimbaji wa Kwaya ya Tumaini (K.K.K.T- Imani Mwanza).
 
Goody alitoa Album yake ya Kwanza Agosti 19, 2008 aliyoifanya katika Studio ya Ujumbe Records chini ya Meneja wake Abraham Nyantori. Katika Utengenezaji wa Album hiyo, Goody alifanya kazi na Maproducer mbalimbali wa Jijini Mwanza kama Selemani Muyomba, na Charles Sokoro.
 
Mwaka 2012 Goody alianza kurekodi Album yake ya 2 aliyoipa Jina la NIMEUONA, ambalo ni Jina la Moja ya Nyimbo zinazopatikana katika Album hiyo. Katika Album hiyo kuna Nyimbo kama vile Nimelipiwa Deni, Nimeuona na Wa Moyo(Wimbo unaopendwa sana na Watu wengi na ni Wimbo Unaofanya vizuri sana katika vituo mbalimbali vya Nyimbo za Injili Kanda ya Ziwa).
 
Mbali ya Uimbaji Goody anauwezo mzuri wa kupiga Kinanda, Drums, Guitar, na Trumpet, Vyombo alivyojifundisha yeye Mwenyewe akiwa kanisa la K.K.K.T- Imani chini ya Tumaini Choir. Goody pia ni Mwandishi wa Nyimbo,  Mtayarishaji wa Nyimbo(Audio Producer), Mwandishi wa Script, Muongozaji wa Filamu na Pia ni Muigizaji. Baadhi ya Nyimbo katika Album yake ya 2 amezitengeneza yeye Mwenyewe kuanzia Utunzi, Utengenezaji wa Beat pamoja na Kufanya Mixing.
Tazama Video hii ya Goodluck Gozbert, Jina la Wimbo ni Nimelipiwa Deni

Mawasiliano ya Goodluck Gozbert
0762486168