Advertise Here

Saturday, March 9, 2013

Uzinduzi wa Kitabu cha "Wokovu ni Uhakika wa Maisha ya Sasa na ya Baadaye".

 
SIKU ya Jumapili ya Tarehe 10 Mwezi wa 3 Mwaka huu, kutakuwa na Tukio la Uzinduzi wa Kitabu Kinachoitwa "WOKOVU NI UHAKIKA WA MAISHA YA SASA NA YA BAADAYE" kilichoandikwa na Mwandishi James Kalekwa ambaye ni Mkufunzi Msaidizi wa Idara ya Sosholojia katika chuo Kikuu cha Mt. Augustino.
Cover la Kitabu hicho
Shughuli hiyo itafanyika Katika Ukumbi wa Mikutano uliopo Isamo Hotel, Jijini Mwanza, na Wazungumzaji katika Uzinduzi huo ni Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la New Vine Christian Centre Mch. Goodluck Kyara - Mwanza, Samuel Sasali - Dar, na Mwandishi wa Kitabu hicho James Kalekwa -  Mwanza.
MD Adolph Robert Nzwalla - Hosanna Praise Team
Uzinduzi huo hauna Kiingilio, na Vikundi vya Kusifu na Kuabudu vitakuwepo chini ya MD Adolph Robert Nzwalla. Mc Pilipili ya Shughuli atakuwepo kupamba Uzinduzi huo.

WOTE MNAKARIBISHWA!