Advertise Here

Sunday, March 31, 2013

Ibada ya Pasaka katika Kanisa la New Vine Christian Centre.

LEO katika Kanisa la New Vine Christian Centre, kulikuwa na Ibada ya Pasaka iliyofanyika Kanisani hapo kuanzia Saa 3:00 Asubuhi hadi Saa 5:45 Asubuhi.
Pastor Goodluck akiwa Madhabahuni
Hizi ni picha za baadhi ya matukio yaliyokuwa yakiendelea Kanisani hapo siku ya leo.
Baadhi ya Waimbaji wa NVCC Praise Team
Mtumishi Jema kama kawaida yake kwenye Keybord
Tenzi za Rohoni pia zilitumika kuleta Uwepo wa Mungu
Mmiliki wa Chombo cha Habari cha Mjap Inc, Baraka Samson akiwa Madhabahuni
Bila huyu Jamaa Setting ya Vyombo haijakamilika. Steve akiwa kwenye Mixer
Neno la Mungu lilitolewa na Mtumishi wa Mungu Eliud Mwasenga likiwa Kichwa Kinachosema, "Kuishi Maisha Mapya ndani ya Kristo".
Mtumishi wa Mungu, Eliud Mwasenga
Kanisa la New Vine Christian Centre lililoko Tema Hotel - ukumbi Mkubwa, Nyegezi Jijini Mwanza, chini ya Mtumishi wa Mungu Pastor Goodluck Kyara, huwa linakuwa na Ibada kila Jumapili kuanzia Saa 3:00 Asubuhi - Saa 5:45 Asubuhi.
Baadhi ya Watu waliohudhuria Ibada leo
Sikiliza sehemu ya Mahubiri ya Jumapili ya leo ya Pasaka yaliyotolewa na Mtumishi wa Mungu Eliud Mwasenga


Je! Ungependa kupata CD za Mahubiri haya ili ukue zaidi kiroho? Piga Simu sasa Namba; 0754 435951.

Sasa Tazama Sehemu tu ya Wimbo wa Kuabudu ulioimbwa na New Vine Christian Centre - Praise Team, katika Ibada ya leo ya Pasaka