Advertise Here

Saturday, March 16, 2013

Jenipher Mgendi kutoka na "Hongera Yesu".

Jenipher Mgendi
Mwimbaji Mkongwe wa Nyimbo za Injili Tanzania ambaye kwa Muda mrefu sasa amekuwa akijihusisha pia na utengenezaji wa Filamu Jenipher Mgendi, anatarajia kutoa album yake mpya Mwezi wa 5 Mwaka huu.

Akizungumza na Gospel News Media, Jenipher amesema kuwa album hiyo itakuwa na Jumla ya nyimbo 8 na Nyimbo zote ameimba peke yake pasipo kumshirikisha Mwimbaji yeyote.

Baadhi ya Nyimbo zitakazopatikana katika Albam hiyo ni kama Hongera Yesu(Wimbo uliobeba Jina la album), Msimamo, Asante Yesu, na nyinginezo. Kwa Mwezi huo wa 5, Album hiyo itatoka katika Mfumo wa audio peke yake.

Mtandao huu ulipotaka kujua sababu za Jenipher kuwa kimya kwa muda Mrefu, Jenipher amesema kuwa alikuwa akitengeneza Filamu 2 ambazo ni "Teke la Mama" pamoja na "Chai Moto".