Advertise Here

Wednesday, March 13, 2013

Kanisa Katoliki ulimwenguni lapata Papa Mpya.

 
Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Papa Jorge Mario Bergoglio ambaye ni kanidali kutoka nchini Argentina ametangazwa rasmi kuwa Papa wa Kanisa Katoliki.

Papa Francis (Jorge Mario) ana umri wa miaka 76 na amekubali kuitumikia nafasi hiyo. Na ikumbukwe pia Papa Francis Jorge Mario ameweka historia ndani ya Jiji la Vatican na Dunia kwa Ujumla Mara baada ya Kuwa Papa wa Kwanza kutoka katika Bara la Marekani ya Kusini.

 
Alizaliwa Mjini Buenos Aires huko Argentina mwaka1936.
Papa Francis 1 ni mtu wa kwanza katika kipindi cha miaka elfu moja (1,000) kwa mtu kutoka nje ya bara la Ulaya kutawazwa kuwa papa wa Kanisa Katoliki.

Papa Francis 1 ni mwana wa Mtaliano aliyekuwa akifanya kazi katika shirika la gari Moshi kabla ya kuhamia nchini Argentina miaka ya zamani.

Kama kadinali wa Jimbo la Buenos Aires ,Kadinali Bergoglio amekuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya Argentina.
Hata hivyo Kadinali Bergoglio anapendwa sana na wafuasi wa kanisa hilo huko Argentina na hasa watu maskini.

Kadinali Jorge Bergoglio kwa karibu miaka yake yote kama Kasisi amehudumu nyumbani kwao Argentina. Kadinali huyo wa Jimbo la Buenos Aires inasemekana aliibuka nambari mbili wakati Papa Benedict alipochaguliwa mwaka 2005.

Anaaminika kuwa na ujuzi mkubwa ambao wengi wanasema utamsaidia sana katika uongozi wake. Katika maisha yake ya huduma kwa Kanisa Katoliki huko Amerika Kusini ambapo Kanisa Katoliki lina waumini wengi zaidi duniani, Kadinali Bergoglio ameibuka kuwa mtu anayependa sana udhabiti wa kisiasa katika nchi zilizo katika bara la Amerika Kusini.
 
Bergoglio anasifiwa kwa kuleta mageuzi makubwa katika Kanisa la Argentina huku katika eneo hilo la Amerika Kusini Kanisa bado linashikilia itikadi za kale.