Advertise Here

Tuesday, March 26, 2013

Sifa Group Foundation yahitaji Milioni 16 kusaidia Watoto yatima.

Mkurugenzi wa Sifa Group Foundation, Sifa John
Sifa Group Foundation ni taasisi iliosajiliwa kisheria, inajishugulisha na maswala ya kusaidia watoto yatima na watoto wa mazingira magumu. Pia kituo hiki husaidia vijana wasio na ajira ili wapate cha kufanya na wasiwe tegemezi.
Mkurugenzi wa Sifa Group Foundation, Sifa John akiwa Ofisini kwake
Kituo hiki kilichopo Bunju B, Mtaa wa Sun Nsiro - Jijini Dar es salaam na kilichoanzishwa na Mwimbaji wa Nyimbo za Injili toka Nchini Tanzania Sifa John, mpaka sasa kimekwisha saidia vijana kumi na tatu(13) kwa kuwapa mafunzo ya ushonaji na sasa wamejiajiri wenyewe. Vijana wengine saba(7) wamejua computer, na vijana wa tano(5) wanajishughulisha na miradi ya chips na vinywaji.
Darasa la Cherehani linalomilikiwa na Sifa Group Foundation
Pia kituo hiki kina jumla ya watoto 105 ambao ni yatima na wale wanaotoka kwenye mazingira magumu. Vijana hawa wanasaidiwa katika swala zima la elimu, chakula na mavazi. Na kwa wale ambao hawajawahi kusoma kabisa, kituo kimewatafuta walimu na kimeanzisha madarasa ambayo vijana hao wanapewa elimu.
Baadhi ya Watoto wanaohudumiwa na Sifa Group Foundation wakipokea zawadi ya Nguo kutoka kwa Mkurugenzi wa kituo hicho Sifa John
Watoto 17 kati ya hao huishi hapo hapo kituoni na wengine hurudi majumbani kwao jioni. Mkurugenzi wa kituo hicho Sifa John anasema, "Pamoja na kuruhusu watoto hawa warudi Majumbani kwao, roho yangu huniuma sana kwa sababu najua mahali wanakoenda kulala palivyo pabaya, ila sina jinsi sababu sijapata nyumba kubwa ya kuwatosha, lakini niko katika kutafuta jinsi ya kununua kiwanja ambacho kipo tayari na kinahitaji pesa taslimu Sh. Milioni kumi na Sita, ili tuweze kujenga shule pamoja na hosteli kwaajili ya kulala watoto hawa".
Hivi ndivyo Sifa Group Foundation inavyohakikisha kuwa Watoto wanaoishi kwenye Mazingira Magumu wanapata Elimu.
"Pia maombi yangu kwa mtu yeyote yule mwenye roho ya Huruma juu ya Watoto hawa, atowe msaada wowote alionao ili tuweze kupata mahali pa kuwaweka watoto hao 115, na waweze kusoma na kuishi maisha mazuri kama wanayoishi watu wengine" Aliongeza Sifa John.
Mkurugenzi wa Sifa Foundation, Sifa John(Wa Pili Kulia) akiwa na Baadhi ya watu walinaojitolea Misaada mbalimbali katika kituop hicho
Kwa msaada wowote, Tumia namba hizi;
Tigo Pesa: 0652 562347
M-Pesa: 0766 91 37 80.
 Account No: 010 - 00 175 951 (Benki ya Posta)
email: sifagroupfoundation13@yahoo.com

Mungu akubariki sana wewe utakayeguswa kwaajili ya jambo hili.