Advertise Here

Thursday, March 7, 2013

Huyu ndiye Adolph Robert Nzwalla.

Adolph Robert Nzwalla ni Kijana wa Kwanza kwenye Familia ya Marehemu Bishop Robert Nzwalla na Bishop Irene Nzwalla  kutoka katika kanisa la Hosanna Christian Centre lililopo Ghana, jijini Mwanza. Addo kama ajulikanavyo na wengi , anao wadogo zake wapatao wanne ambao ni Priscilla na Gladyce hawa ni mapacha na mdogo wao wa Mwisho anaitwa Joseph Robert Nzwalla.
Adolph Robert Nzwalla akipiga Keyboard wakati wa Ziara ya John Lisu jijini Mwanza
Adolph Nzwalla ni Mtangazaji  wa redio ya kikristo ijulikanayo kama  HHC Alive Fm yenye makazi yake maeneo ya Kirumba jijini Mwanza inayorusha matangazo yake kupitia  masafa ya 91.9 Fm. Tofauti na utangazaji Addo pia ni Music Director wa Hosanna Praise team ya Jijini Mwanza. Kwa muda mrefu sasa amekuwa akijishughulisha na muziki wa injili akiwa kama muimbaji, mpigaji na mshauri kwa makundi na matukio mbalimbali yafanyikayo jijini Mwanza na kanda ya ziwa kwa ujumla.
Slim B
Adolph Nzwalla alianza rasmi kujishughulisha na muziki akiwa  mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Nyanza na baada ya hapo alijiunga na shule ya sekondari Mwanza(Mwanza Sec). Baada ya kumaliza elimu yake ya Sekondari, Addo alipata nafasi ya Kwenda kusoma Nchini Marekani katika Chuo cha Word of Life School of Ministry ambacho kiko katika Jimbo la Delaware na baada ya kumaliza masomo alirejea Nyumbani na kuunda kundi la Hosanna Praise Team ambalo ndilo anafanya nalo kazi hivi sasa Kama Music Director na Worship Leader wa kundi hilo.
 
Mwaka 2009 Addo alikuwa ni mmoja wa majaji  katika shindalo la Kusaka Vipaji kwa kanda ya Ziwa lijulikanalo kama “Zaburi Gospel Star Search” ambalo lilikuwa likirushwa na kituo cha Television cha Star Tv cha jijini Mwanza. Mwaka juzi Addo alikuwa miongoni mwa watumishi walio-organise ujio wa New Life Band katika jiji la Mwanza. Katika ujio huo kulifanyika Tamasha kubwa la kihistoria katika viwanja vya Furahisha lililohudhuriwa na maelfu ya wakazi wa Mwanza pamoja na mama Diana Mwakasege kutoka Arusha.
Adolph Nzwalla akirun show ya Cross Rythm ndani ya Hhc Alive Fm
Addo anauwezo mkubwa wa kupiga Gitaa la solo, Keyboard, drumz na tumba, lakini kwa muda mwingi huonekana akipiga keyboard. Katika Huduma hii ya Uimbaji amefanya Huduma na Waimbaji wakubwa kama Jackson Benty, John Lisu, Miriam Lukindo, Pastor David Yared pamoja na waimbaji wengi wa sifa na kuabudu. Katika jiji la Mwanza Addo amekua akiandaa na wakati mwingine kushirikishwa katika kuandaa matamasha mbalimbali ya kusifu na kuabudu.
Adolph Nzwalla akiongoza worship pamoja na mtumishi Ihano Nestory wakati wa ThanksGiving Concert
  Tazama Video hii ambapo Addo alikuwa aki'lead Wimbo wa Ahsante Yesu.