Advertise Here

Sunday, September 9, 2012

Mchungaji aliyebadili Dini kuwa mkristo, aachiwa huru baada ya kifungo cha Miaka 3 gerezani.


MCHUNGAJI wa Kanisa moja Nchini Iran Mch. Youcef aliyekuwa kifungoni kwa zaidi ya miaka mitatu kwa kukabiliwa na kosa la kuuasi uislam na kubadili dini kuwa mkristo, sasa ameachiwa huru. Mchungaji huyo alipata hukumu ya kunyongwa ili kuwatisha watu wengine wasibadili dini kuwa wakristo.

Sehemu mbalimbali Duniani kulikuwa na maombi ya mnyororo ya kufunga kwa wakristo ili kumuomba Mungu awezeshe kuachiwa huru kwa Mchungaji huyo na hilo Mungu amefanya leo kwani Mchungaji Youcef ameachiwa huru na kuungana na familia yake.

Glory to God!