Advertise Here

Sunday, September 9, 2012

Kanisa la Anglikana lataka kuwa na Raisi.

Archbishop Rowan Williams
ASKOFU Mkuu wa kanisa la Anglikana, Rowan Williams, amefichua siri kuwa kanisa hilo linaandaa mpango wa kumteua rais wa kanisa, ambaye atabeba sehemu ya jukumu la kuongoza kanisa duniani.

Alisema mtu atayechukua nafasi hiyo ataweza kusafiri kwa urahisi, na hivyo kumuacha Askofu Mkuu kushughulika zaidi na kuongoza kanisa.

Doctor Williams, ambaye anastaafu mwezi Disemba baada ya uongozi wa miaka 10, alikiri kuwa hakuweza kufanya mengi kuzuia mgawanyiko kanisani juu ya swala la uhusiano wa jinsia moja.

BBC Swahili