Advertise Here

Tuesday, September 11, 2012

Pastor Daniel Moses Kulola anakukaribisha kwenye OYES CONFERENCE - Mwanza.

Pastor Daniel Moses Kulola

MCHUNGAJI Daniel Moses Kulola wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya la Jijini Mwanza, anakukaribisha katika Kongamano la Kimataifa la OYES yaani "OPEN YOUR EYES AND SEE", Kongamano litakalofanyika katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Jipya la Saba Saba.

Mhudumu wa Kimataifa Mch. John Bigirimana kutoka Norway atahudumu. Kongamano hilo linatarajia kuanza Jumatano hii kuanzia Saa 8:30 Mchana mpaka Saa 12:30 Jioni, na Kongamano hili litaisha Siku ya Jumapili.

Kila siku ya Kongamano kutakuwa na shifti 2. Kwaya Mbalimbali na Waimbaji binafsi pia watakuwepo ili kuhudumu katika kongamano hilo. Ukipata taarifa hii, mtaarifu na Mwenzako.

NYOTE MNAKARIBISHWA!