Advertise Here

Tuesday, September 11, 2012

Mchungaji Vinac Mwakitalu; Matatizo ya Serikali ya Tanzania, Chanzo ni Kanisa.

Mchungaji Vinac Mwakitalu
 
WAKRISTO wametakiwa kujua kwamba matatizo makubwa katika serikali ya Tanzania yanatokana na wao kutokuwa waaminifu mbele za Mungu katika kufanya Ibada ya Utoaji.
 
Akihubiri katika Ibada ya Jumapili Mchungaji na Mwalimu Vinac Amnon Mwakitalu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilomba Christian Centre Mbeya amesema serikali nyingi ulimwenguni ikiwemo Tanzania zimejikuta katika changamoto mbalimbali kutokana na kanisa kutokuwa waamini katika utoaji wa mafungu ya 10 na sadaka mbalimbali. 

Mchungaji Mwakitalu ameongeza kusema Mungu ndiye anayejua kipimo halisi cha utoaji kwa mtu wa Mungu na kwamba kwa kufanya hivyo hakuna anayeweza kumdanganya Mungu. Pia Mchungaji Mwakitalu amesema wengi wamefikiri kuwa kufunga na kuomba sana ndio miujiza itafanyika huku wakisahau utoaji wa Mafungu ya 10 na sadaka mbalimbali. 

Aidha Mchungaji Mwakitalu alibainisha Baraka za mwamini anayekuwa mwamini katika utoaji wa sadaka na mafungu ya 10 kuwa Mungu atafungua madirisha ya mbinguni na Baraka zake zitamiminika kwa mja wake.