Advertise Here

Saturday, March 8, 2014

Rais Uhuru Kenyatta avutiwa na Uimbaji wa Rufftone.

kenyaatta
Rais Uhuru Kenyatta
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ambaye siku chache zilizopita ameonesha nia yake ya wazi wazi ya kuutangaza zaidi Muziki wa Kenya, amekiri kuwa anapenda sana Mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini humo Rufftone.

Kupitia mahojiano yaliyofanywa na Easy Fm, Katibu wa Mawasiliano na msemaji wa Rais wa Kenya Manoah Esipisu amesema kuwa Rais Kenyatta anaupenda sana Muziki wa Kenya, na kuwa Rufftone ndiye Mwimbaji anayempenda zaidi.

Rufftone ni moja mojawapo kubwa sana Nchini Kenya kwenye tasnia ya Muziki wa Injili, ambaye anafanya vizuri sana kwa sasa kupitia Wimbo wake wa "Mungu Baba" ambao alipata fursa ya kuuimba wakati wa Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Kenya. Huku Kaka yake Daddy Owen akiendelea kufanya vizuri pia katika tasnia ya Muziki wa Injili Nchini Kenya.