Advertise Here

Friday, March 2, 2012

Martha Mwaipaja asherehekea Send Off Party yake ndani ya Diamond Jubilee.

Martha akiwa na Mumewe mtarajiwa Mch. John

Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Martha Mwaipaja, jana usiku ilikuwa ni Sherehe ya Send Off Party yake, iliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee (VIP HALL).
Siku chache zijazo, yaani kesho kutwa, Martha atakuwa akifunga ndoa na Mch. John Said wa Kanisa la UDHIHIRISHO WA INJILI lililopo maeneo ya Kipunguni B, Ukonga jijini Dar es salaam.

Martha akiwa na waimbaji mbalimbali wa Nyimbo za Injili

Akizungumzia sherehe hiyo, Mch. John anasema “Ndoa yetu itafungwa Jumapili ijayo March 4, 2012 katika kanisa la Ukonga, na kufuatiwa na Shughuli itakayofanyika katika Ukumbi wa Sinza Delux kuanzia mida ya Saa 1 usiku.”

Kitchen party ya Martha Mwaipaja, ilifanyika Jumapili iliyopita February 26, 2012.

BLOG HII INAWATAKIA HARUSI NJEMA, NA MAISHA MEMA YENYE FURAHA TELE.