Advertise Here

Monday, January 7, 2013

Hosanna Christian Centre yafanya Tamasha Kubwa la Kumshukuru Mungu kwa Kuiona 2013.

Revival Mission Band wakihudumu
SIKU ya Jana katika Kanisa la Hosanna Christian Centre lililoko maeneo ya Kilimahewa Jijini Mwanza chini Mtumishi wa Mungu, Bishop irene Nzwalla, kulifanyika Tamasha kubwa la Kusifu na Kuabudu likiwa na Lengo la Kumshukuru Mungu kwa Kuiona 2013, kwani ni Neema ya Kipekee sana.
MD Adolph Robert Nzwalla chini ya Uwepo wa Mungu
Twakuabudu Bwana.................
Uweponi Mwake
Vikundi mbalimbali pamoja na Band mbalimbali za Muziki wa Injili zilishiriki huku Hosanna Praise Team chini ya Music Director(MD) na Mtangazaji wa radio ya kikristo ya Alive Fm, Adolph Robert Nzwalla wakiongoza Sifa na Kuabudu.
Sehemu ya Hosanna Praise Team
Uliniweka Tumboni Mwa Mama yangu ili Nitumike kama Chombo........
Dada huyu aliimba Siku ya Jumapili akiwa ni Mjamzito wa Miezi 9, na Siku ya leo amejifungua salama mtoto wa Kiume. Ni Jambo la Kumshukuru sana Mungu!
Baadhi ya Band za Muziki wa Injili zilizoshiriki ni kama Revival Mission Band pamoja na Exellence Band zote zikiwa ni za Jijini Mwanza. Pamoja na Pastor David Yared.
Pastor David Yared akihudumu
Katikati, ni Mzee wa Juu ya Mataifa Almaarufu Joel Kaema(Mtangazaji Alive Fm)
Papaa Noel Mlabwa Kutoka katika Kundi la "Brothers" la Jijini Mwanza
 Mbali ya Tamasha hilo pia Jana ilikuwa ni siku Maalum ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi katika Kanisa hilo. Jiwe hilo liliwekwa na Mchungaji kiongozi wa kanisa hilo Bishop Irene Nzwalla.
Bishop Irene Nzwalla
Moja ya Vichwa vyenye Vocal Kali sana Jijini Mwanza
Sephone Sospeter kama kawaida yake