Advertise Here

Monday, December 31, 2012

Salamu za Mwaka Mpya 2013 kutoka "Gospel News Media".

 

Bwana Yesu Asifiwe!


Kipekee Nianze kwa Kumshukuru sana Mungu kwa kunipa pumzi ya Uhai ambayo bado inanipa nafasi ya kutuunganisha Mimi pamoja na Wewe. Nawashukuru pia wazazi wangu ambao wamekuwa Msaada mkubwa sana kwangu. Mwaka 2012 ulikuwa ni Mwaka wa Mafanikio sana kwangu ingawa si kwa asilimia mia, lakini kwa kiwango kikubwa nimefikia malengo niliyojiwekea kwa Mwaka wa 2012.
Blogger Sowane Emmanuel
 Nikiwa kama Mwanzilishi wa Blog hii ya kikristo ya Gospel News Media, napenda kutumia fursa hii kukushukuru wewe Msomaji wa Blog hii, lakini pia niwashukuru watu wote ambao kwa Namna moja au Nyingine wamefanikisha Malengo ya Blog hii kwa Mwaka 2012. Sina cha kuwalipa ila Mungu wa mbinguni naamini ni Mkuu sana na Kamwe hata wapungukia.
Historia ya Blog Hii
Blog hii ilianza Mwaka 2011, ikiwa na Jina la Halleluyah Gospel Outreach ikiwa na link ya www.esowane.blogspot.com (Haiko hewani kwa sasa). Mwaka 2012 mwezi wa 2, blog nyingine ya kikristo ilianzishwa ikiwa kama mbadala wa blog ya Halleluyah Gospel Outreach, na blog hii ilikuwa ni Hot Gospel News ikiwa na link ya www.hotgospelnews.wordpress.com (Bado ipo hewani mpaka sasa ingawa haitumiki tena). Miezi michache baadae, blog hiyo ilibadilishwa Jina kutoka Hot Gospel News na kuwa Gospel News Media ikiwa bado na link ile ile. Baada ya Miezi 6, yaani Agosti Mwaka huu, ndipo Blog hii ya Gospel News Media ikiwa na Link ya www.gospelnewsmedia.blogspot.com ilipoanzishwa rasmi. Mabadiliko yote hayo yalifanyika ili kuhakikisha kwamba ubora wa kutosha unapatikana.

Shukrani za Dhati
Napenda sana kumshukuru Brother Victor Nivox (Mmiliki wa Blog ya Kikristo ya Hosanna Inc) ambaye alinipa hamasa ya kutosha ya kuanzisha Blog ya Kikristo. Alitoa muda wake kwa kunifundisha, kunielekeza na kunikosoa pia pale alipoona sipo sawa. Mungu akubariki sana kwa Msaada wako Kaka Victor ambao umefanya leo nimefika hapa. Mimi ni Moja ya Matunda yako!
Victor Nivox
 Pia napenda sana kuwashukuru wamiliki wenzangu wote wa blog za kikristo kwa Ushirikiano na Msaada wao ambao wamenipa mpaka leo nimefika hapa. Napenda nitambue wa Mchango wa Patrick Samson Sanga(Patrick Sanga Ministry)  Mary Damian(Strictly Gospel), Samuel Sasali(Sam Papaa Blog), Ambwene Michael(Gospel Kitaa), James Temu(Uncle Jimmy Blog), Jacqueline Moshi(Real Life 4 Christian), Firmina Matee(Amenhalleluyah Blog), Baraka Samson(Mjap Inc), Faraja Naftal(Fmndeme Blog), Tunu Bashemela(Gospel Vision),  King Chavala(Chavala Blog), Rulea Sanga(Ruma Africa Blog), Erick Brighton(Pamoja kwa Umoja Blog) na wengine wengi.
Baadhi ya Wamiliki wa Blog za Kikristo Tanzania, baada ya kikao kilichofanyika Octoba Mwaka 2012 Jijini Dar es salaam
Mbali ya hawa, napenda pia kutambua Mchango wa watu wangu wa karibu ambao walikuwa Msaada mkubwa sana kwa kufanikisha malengo ya blog hii, baadhi ni kama Adolph Nzwalla, Barnabas Shija, Elia Migongo, Buberwa, Nyamiti Kayora, Maganga Gwensaga, Joel Kaema, Ruth Lyanga, Vick Bonge, Shija Chongolo, Mary Ramadhani, Members wote wa TAFES SAUT, Wafanyakazi wenzangu wote wa Alive Fm na Wengine wengi.

Malengo ya kuanzishwa kwa Blog Hii
Kutokana na Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia, Dunia sasa inakuwa si kijiji tena, bali ni Nyumba moja. Mabadiliko hayo yanaleta umuhimu kwa sisi tukiwa kama wakristo, kuweka sehemu maalum ambayo wakristo wengi watapata habari mbalimbali za kikristo na mafundisho ya Neno la Mungu kupitia Mtandao.

Tasmini ya Blog hii Kwa Mwaka 2012
Najua tumefanya mengi sana kwa Mwaka 2012, Mimi pamoja na Team yangu nzima. Pengine kuna ambayo tuliyafanya tukihisi ni mazuri, kumbe kwa namna moja ama nyingine ilikuwa ni kwazo kwako. Pale tulipokosea na kukukwaza tunaomba utusamehe sana, na tuanze Mwaka Mpya wa 2013 tukiwa na amani ndani ya Mioyo yetu.

Tunakuahidi uboreshaji wa utaratibu wetu wa utoaji wa habari, na mafundisho mbalimbali. Lakini pia tunakaribisha Maoni yako au Ushauri wako ili kuboresha Blog hii. Mchango wako wa Mawazo ni wa Muhimu sana katika kuboresha Blog hii.

Gospel News Media-Team inawatakia Heri ya Mwaka Mpya 2013. Tunawashukuru wote na Mungu awabariki sana!

Kwa Maoni/Ushauri, Wasiliana Nami;
Sowane Emmanuel
0712 113305
0754 030789
Email; sowane@ymail.com
 Facebook Page; Gospel News Media