Advertise Here

Tuesday, December 25, 2012

Ujumbe wa Krismasi toka kwa Mwl. Christopher Mwakasege.

Mwl. Christopher Mwakasege
 Mimi na mke wangu na familia yetu yote, yaani watoto na wajukuu, tunakutakia sikukuu njema ya krismasi.
Ujumbe nilionao kwako ni kutoka katika kitabu cha Mathayo 2:1-23. Ndani ya ujumbe huu napenda kukuambia mambo mawili makubwa.

Jambo la Kwanza
Yesu Kristo alipozaliwa Bethelehemu, si kila mtu alifurahi. Biblia inasema ya kuwa kuzaliwa kwa Yesu kuliposikika: " Mfalme Herode....alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye"(Mathayo 2:3). Kwa hiyo, hata wewe usishangae unapoona si kila mtu anafurahi juu ya kuokoka kwako. Si kila mtu atafurahi atakapoona Yesu anazaa kitu moyoni mwako. Na pia usitegemee kuona kila mtu anayekuona unadumu katika Kristo atakufurahia

Jambo la Pili
Kama vile Mungu alivyomsaidia na kumlinda Yesu alipozaliwa asiuwawe na wale waliochukia kuzaliwa kwake,uwe na uhakika Mungu huyu atakilinda kilicho cha Yesu katika maisha yako, kisiuwawe na wanaokichukia.

Naamini ujumbe huu utakutia moyo katika siku hii muhimu.