Advertise Here

Saturday, December 29, 2012

Kongamano la Kuingia Mwaka 2013 laanza rasmi leo Jijini Dar.

Mch. Florian Katunzi katika Moja ya Huduma zake
KONGAMANO la Siku 4 linalofanyika katika viwanja vya Maonesho vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere zamani Sabasaba leo limeanza rasmi huku waimbaji mbalimbali pamoja na Watumishi mbalimbali wakihudumu.
Martha Mwaipaja akihudumu
 Kongamano hilo ambalo ni Maalum kwa ajili ya kuukaribisha Mwaka 2013 na Kumshukuru Mungu kwa kutupigania kwa Mwaka wote wa 2012, litafanyika kwa Siku 4 mfululizo kuanzia leo.
 
Upendo Nkone akihudumu katika Kongamano hilo siku ya leo
Kwa siku ya leo, waimbaji mbalimbali kama Upendo Nkone na Martha Mwaipaja walihudumu huku Watumishi wa Mungu kama Mch. Florian Katunzi wakitoa Mafundisho Maalumu kwa ajili ya kuuanza vizuri Mwaka 2013.
Watoto nao hawakuachwa nyuma
Mbali ya hilo, familia mbalimbali zitapata nafasi ya kuombewa ili Mungu afanye kitu katika Maisha ya familia hizo kwa Mwaka 2013. Matangazo haya pia yatakuwa yakirushwa hewani moja kwa moja kupitia Wapo Radio Fm(98.1Mhz).

Watu Wote Mnakaribishwa!!!