Advertise Here

Wednesday, May 1, 2013

Word Explosion Summit yaanza rasmi Mwanza.

Mch. Emmanuel Mchutah
Ile Semina ya WORD EXPLOSION SUMMIT inayoingia siku ya pili leo, Jana ilifanyika katika Kanisa la TAG Nyamalango, Malimbe Mwanza na kuhudhuriwa na Watu wengi sana. Semina hiyo ambayo wanenaji ni Mchungaji Emamuel Mchutah na Janeth Mchutah, itafanyika kwa Siku 5, ambapo siku ya jumamosi itakuwa ndiyo siku ya mwisho ya Semina hiyo.

Siku ya Jana ilikuwa ni Siku ya Utangulizi tu, na Mafundisho rasmi yanaanza leo kuanzia Saa 11:45 Jioni mpaka Saa 2 Usiku. Kwa siku ya Jana, Vijana wengi walijitokeza kukabidhi Maisha yao kwa Yesu(Kuokoka).

Tazama video hii, inayoonyesha baadhi tu ya Watu walioamua kumpokea Yesu huku Mchungaji Emmanuel akiwaongoza sala ya toba