Advertise Here

Monday, May 27, 2013

Yaliyojiri kwenye Tafes Saut Live DVD Recording Jana, Pale JB Belmont Hotel - Mwanza.

JANA ndiyo ilikuwa siku ya kufanya LIVE DVD RECORDING ya kundi la Kusifu na Kuabudu toka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino-Mwanza. Shughuli hiyo iliyofanyika katika Hotel ya JB Belmont Hotel, ilianza mida ya Saa 9 Jioni na Kumalizika Mida ya Saa 3 Usiku chini ya Vocal & Music Director Samuel Yonah toka Dar es salaam.

DvD hiyo iliyopewa jina la Revival Flames Praise & Worship - Season 1 ukamilifu wake umefanikiwa chini ya Udhamini wa SIFA TANZANIA, CLARA SALOON na Radio ya Kikristo ya HHC ALIVE FM (91.9Mh) na Tukio hilo lilirushwa LIVE kupitia Radio Sayuni. Sasa tazama jinsi tukio hili lilivyofana....
 








Hiki ndo Kikosi cha Tafes Saut Kilichofanya Mashambulizi siku ya Jana
Sasa kama Jana hukupata fursa ya kusikiliza kilichokuwa kikiendelea pale JB belmont hotel kupitia Radio Sayuni iliyokuwa ikirusha Matangazo LIVE kutoka eneo la Tukio, hebu sikiliza wimbo huu ambao nilipata kuurekodi LIVE Siku ya Jana pale JB Bemont Hotel

Hiyo ni "Sample" tu, Original yenyewe inakuja. Jiandae kujipatia Nakala yako HALISI ya DVD ya Kwao Tafes Saut siku chache Zijazo.