Advertise Here

Tuesday, May 7, 2013

Hongera Boniphace Magupa na Jessica Honore kwa kufunga ndoa.

Juzi ilikuwa ni Siku ya Furaha kwa Wanandoa hawa wapya Boniphace Magupa ambaye ni Mtangazaji wa kituo cha luninga cha Chanel 10 na Jessica Honore ambaye ni Mwimbaji wa Nyimbo za Injili.

Harusi hii ilifungwa katika Kanisa la Anglikani mkoani Shinyanga, na kufuatiwa na tafrija fupi nyumbani kwa akina Boniphace Magupa maeneo ya Ndala, Shinyanga kabla ya kuelekea Ukumbi wa NSSF kwa ajili ya kuwapongeza Maharusi hawa.

Shughuli hiyo ilihudhuriwa na watu mbalimbali kutoka mikoa mbalimbali Tanzania.
 Mtandao huu, unawatakia Maharusi hawa Maisha mema na yenye Furaha tele.