Advertise Here

Monday, January 13, 2014

Safu ya James Kalekwa: Ongeza Maana/Thamani kwenye maisha yako kwa kuwa na malengo na kuyaelekea. - Part 2

James Kalekwa
Kisa mkasa (Scenario) #2
Mchezo wa mpira wa miguu bila magoli

Kama wewe ni mpenzi, mshabiki au mfuatiliaji wa mchezo wa mpira wa miguu basi uanelewa fika juu ya muundo wa viwanja vya mchezo huo… Moja ya vitu muhimu sana kwenye ujenzi wa kiwanja ni milingoti minne mikubwa isimamayo pande mbili tofauti (zinazokabiliana) za uwanja. Bila shaka umekwisha baini ya kwamba ninazungumza kuhusu magoli.


Hebu fikiri, mchezo wa mpira wa miguu pasipo magoli uwanjani… Je, inawezekana kuwa na mchezo huo? Hata ule mpira wa “mchangani” huwa na magoli, hata kama ni ya mawe au vijiti…

Hauwezi kuwa mpira wa miguu bila magoli. Hebu jiulize wachezaji wangekuwa wanakimbiakimbia uwanjani, wanapiga chenga, wanapeana pasi, wanakaba/wanazuia mashambulizi… ili iweje sasa???

Kuna umuhimu gani wa kuwa na mchezo wa mpira wa miguu pasipo magoli? Lengo kuu la mpira wa miguu ni magoli. Ukiyatoa malengo hayo, umeondoa maana, umeondoa thamani iambatanayo na mchezo huo.


Kabla hatujachukua hatua kubwa sana katika kujifunza haya, ninaomba tujenge uelewa wa pamoja juu ya maswala kadhaa ambayo yana uhusiano wa moja kwa moja na maswala mazima ya malengo.


Kusudi – ni sababu kuu ya kuwepo kwako. Hii hujibu swali la “Kwanini ninaishi?” mfano: Ninaishi ili kuudhihirisha utukufu wa Mungu kwenye kizazi changu.


Maono – ni taswira/picha kubwa uionayo juu ya mwisho wa maisha yako. Ni mkusanyiko wa mwisho wa maisha yako. Hii hujibu swali la “ninakwenda wapi?” mfano: … Kumtukuza Mungu kwa kufanya ugunduzi, uvumbuzi na utatuzi chanya wa mahitaji ya kizazi changu.



Dhamira – ni namna gani utafanya ili kuyafikia maono hayo kivitendo. Hii hujibu swali la “Namna gani nitatekeleza?” Mfano: … Kufungua taasisi ya utafiti wa uwezo wa mwanadamu na uelimishaji wa vijana.

N.B Unaweza kuwa na dhamira zaidi ya moja… Hakuna ukomo ilimradi tu dhamira zinafanikisha ufikiaji wa maono yako.



Malengo/Mipango – ni kuweka namna/njia za kivitendo na zinazopimika ili kufanikisha dhamira yako/zako Mfano: … Kufanya usajili wa taasisi yangu ifikapo March 28 ili kuanza utendaji rasmi.



Mkakati – ni mchanganuo wa hatua kwa hatua na uratibu wa rasilimali ili kufanikisha malengo yako. Hii hujibu maswali mengi “Nifanye nini, nifanye wapi, wakati gani?...” Mfano:


Mkakati wa usajili wa taasisi:

#
Jukumu
Yatakayohitajika
Kinachotarajiwa
Muhusika
Lini
Hali ya utendaji

Kuandika katiba ya taasisi.

Katiba ya taasisi
Frida
1-23 January, 2014
Inaendelea

Kualika wajumbe waanzilishi na kuwashirikisha wazo

Kikao/mkutano wa kwanza
James
28 January, 2014
Bado

Kufanya shughuli za usajili wa taasisi

Cheti cha usajili
Charisa & Joshua
19 February, 2014
















Kutoka kwenye mkakati huu unaweza kutengeneza bajeti (maelezo juu ya uratibu wa rasilimali fedha).


Lengo la kuainisha, walau kwa ufupi tu, tofauti ya mambo hayo ni ili uwe na uhakika na kitu gani unakiendea na unapaswa kufanya. Ni muhimu sana ufahamu ya kwamba kusudi ndilo huwa sababu ya maono; maono huzaa dhamira (utume) na dhamira ndiyo huleta malengo ambayo huzaa mikakati tayari kwa utekelezaji. Ili kurahisisha uelewa juu ya mambo haya, tazama na kujifunza kwenye Taswira ifuatayo:


Somo litaendelea Jumatatu Ijayo.....

 Mafundisho haya yameandaliwa na James Kalekwa
Mwanataaluma, Mwandishi wa vitabu na Mwalimu wa Neno la Mungu
+255 714 762 669
+255 754 917 764