Advertise Here

Tuesday, April 23, 2013

Mwalimu na Mwimbaji John Shabani atunukiwa Shahada.

Mwl. John Shabani akipokea Cheti chake
Mchungaji mtarajiwa John Shabani (kushoto) amekabidhiwa shahada yake na Askofu Kitonga (Kiongozi wa Makanisa ya Redeemed duniani), baada ya kuhitimu Mafunzo katika chuo cha kimataifa cha huduma (International School of Ministry - ISOM) chenye makao makuu New York Marekani.

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa Mwalimu huyo wa muziki wa injili Afrika mashariki bwana John Shabani, baada ya kuhitimu mafunzo yake hayo kwenye chuo hicho cha kimataifa. John ambaye amekuwa na ndoto za kujiendeleza sana katika elimu mbalimbali, amekuwa miongoni mwa wanafunzi waliofanya vizuri katika chuo hicho.
Mchungaji huyo mtarajiwa anategemea kujiunga na chuo kimoja huko marekani ili kuendelea zaidi na masomo yake, pia amewahasa waimbaji wenzake wa injili kuwa na mpango wa kujiendeleza ki-elimu.

Mahafali hayo yamefanyika jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ki-dini na serikali. Makao makuu ya chuo yaliwakilishwa na Dr. Lee kutoka Marekani.

CHANZO: Tanzania Daily Eye