Advertise Here

Friday, April 12, 2013

Mwimbaji wa Bongo Flavour Kenya Aokoka.

http://themonsterradio.com/wp-content/uploads/2012/10/size-81-440x248.jpgMwimbaji wa Muziki wa kizazi kipya Nchini Kenya Linet Munyali a.k.a Size 8, ametangaza rasmi ya kuwa Ameokoka na hivyo kuachana na Muziki wa Kizazi kipya.
 
Akiongea na Mtangazaji wa Clouds Fm Millard Ayo kupitia kipindi cha Amplifier cha leo April 12, Size 8 amesema, "Nimeamua kuokoka kwasababu Maisha yangu yalikuwa hayana Amani. Mara nyingi nilikuwa Mtu wa Huzuni na kuna kipindi nilikuwa nikitoka kufanya Show Usiku najikuta nalia mwenyewe".

"Pamoja na kwamba pesa ninayo lakini maisha yangu yalitawaliwa na Huzuni" aliongeza Size 8. Akitoa sababu ya yeye kutokuwa na Amani, Size 8 amesema kuwa, hali hiyo ilikuwa ikimtokea tu, na yeye pia hajui sababu ilikuwa ni nini.

Huyu atakuwa si Mwimbaji wa kwanza wa Muziki wa kizazi kipya Nchini Kenya kutangaza kuokoka. Mwimbaji mwingine aliyewahi kuokoka ni DNA aliyetamba sana na Wimbo wa Banjuka. Kwa Tanzania Mwimbaji Stara Thomas pia aliwahi kutangaza kuokoka lakini akaamua kurudi nyuma tena na kuimba Bongo Flavour tena.

Swali la Msingi la kujiuliza, ni; Je! Nini kinafanya Waimbaji hawa kurudi nyuma na kuimba tena Bongo Flavour? Ni jukumu la Kanisa sasa kuhakikisha kuwa watu kama hawa wanalelewa vizuri Kiroho ili waweze kudumu katika Wokovu.