Advertise Here

Wednesday, April 3, 2013

Mgogoro wa Uchinjaji nyama waibuka Tunduma Mbeya.

MGOGORO mkubwa umeibuka kuanzia asubuhi siku ya leo jijini Mbeya wilayani Tunduma ukihusisha suala la uchinjaji wa nyama kwa ajili ya kitoweo, baina ya wakristo na waislam kwenye machinjio ya ng'ombe wilayani Tunduma.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kilichopo eneo la tukio kimeeleza kuwa Vurugu hizo zimekuja baada ya tamko alilolitoa Mkuu wa mkoa wa Mbeya siku moja kabla ,mh.Abas Kandoro tamko lililoruhusu siku ya leo shughuli za uchinjaji wa nyama kwa ajili ya kitoweo katika machinjio mkoani hapo zifanywe na wakristo.

Sintofaham iliibuka siku ya leo ambapo Wakristo waliamkia kwenye machinjio wakiwa wamejiandaa kwa shughuli za uchinjaji rasmi,lakini kinyume na matarajio yao ghafla walipokelewa na Askari wa kutuliza Ghasia FFU wakiwa eneo la tukio kuzuia wakristo kuingia kwenye machinjio kwa kile kilichoelezwa kuwa wamepewa amri hiyo toka kwa mkuu wa wilaya ya Tunduma.

Baada ya zuio hilo ndipo Utaratibu wa siku zote ukafanyika ambapo waislam wakaendelea na shughuli ya uchinjaji chini ya ulinzi wa FFU na baada ya kumaliza kuchinja nyama zote ndipo FFU wakaondoka.

Kufuatia kitendo hicho wakristo walijawa na jazba na ndipo yalipoibuka maandamano makubwa barabarani yaliohusisha uchomaji wa matairi kupinga kitendo hicho kilichotokea siku ya leo.



 

SOURCE: Mjap Inc