Advertise Here

Tuesday, August 20, 2013

Hhc Alive Fm yaendelea na Ratiba yake ya Matamasha ndani ya Jiji la Mwanza.

Maganga James Gwensaga akiwa na Adela Mwampamba katika Tamasha lililofanyika Mkudi
Radio ya Kikristo ya Hhc Alive Fm(91.9Mhz) ya Jijini Mwanza, imeendelea na ratiba ya Matamasha yake ya kila jumapili katika maeneo mbalimbali ya Jijini Mwanza, ikiwa ni sehemu ya utangulizi wa Tamasha kubwa kabisa la FRIENDS FOREVER litakalofanyika Mwezi wa 10 Mwaka huu katika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.
Sehemu ya Umati uliohudhuria Tamasha la Kiseke
Akizungumza na Mtandao huu, Meneja wa kituo hicho Bw. Maganga James Gwensaga amesema kuwa Matamasha haya yatakuwa yakiendelea hadi mwezi wa 10 na hitimisho lake litakuwa ni Tamasha kubwa litakalofanyika CCM Kirumba.
Moja ya kwaya zilizohudumu katika Tamasha la Kiseke
Lengo la Matamasha hayo ni kuweka Wasikilizaji pamoja na jamii kuwa karibu zaidi na Timu nzima ya Hhc Alive Fm. Katika Matamasha hayo kwaya mbalimbali na waimbaji binafsi hupata fursa ya kuhudumu, huku timu nzima ya Watangazaji wa Hhc Alive Fm wakifanya Performance Jukwaani.
Adela Mwampamba na Japhet Busanji
Mpaka sasa Matamasha hayo yamefanyika Maeneo ya Mkudi na Kiseke.