Advertise Here

Tuesday, August 20, 2013

Tukio moja, Kitabu kimoja, Maelezo na Habari ni tofauti. Tunafanyaje?

Habari wapendwa, tupeane maarifa katika  changamoto hii, ili tuwe na maelezo sahihi tuwapo kazini katika shamba la Bwana.


Najiuliza ivi je ni waandishi tofauti au ni yule katika Luka and Matendo? Na vipi sasa uwasilishaji  tofauti wa matukio yale yale-angalia pia Marco and Mathayo?Ni vema sana kukifahamu kitabu chetu (Biblia) ambacho ni bora kabisa kuliko vitabu vilivyowahi kuwako na kama vitakuwako vingine. Wakati mwingine Watu wa Mungu tunapokutana na changamoto ktk Kitabu chetu tukisomapo au hasa tukiuulizwa/kubanwa na wana dini,tunawahi kukemea pepo la upinzani na kufoka ili mtu huyo anyamaze milele au tunakua na hofu kua ni kukaribia kufanya makufuru kuchunguza/kufuatilia kila jambo ktk Neno!-mambo ambayo KiBiblia hayana msingi hata chembe, ni ya kibinadamu tu.

Kama/kwakua hiki ni Kitabu chetu cha ukweli na tunaamini kwa nguvu nyingi kua humo kuna maneno ya ukweli, kuliko kukimbia wajibu wa kulielewa Neno/Maandiko kwa kukemea pepo la kutoelewa ktkt ya watu( ana dini, majirani,wanafunzi tunaowafundisha, hadhira tunayohihubiri), ni faida na busara kufanya kila jitihada kukielewa Kitabu hiki kitamu mfano kukisoma na kukitakafari sana kila mara ili kupata kweli nyingine nyingi zilizomo kuweza ongelea mada/jambo/changamoto kadhaa, kusoma vyanzo vingine vya maarifa, kuuliza Viongozi wetu wa Kiroho au Mkristo mwenzio, kuomba/kumuuliza Roho Mtakatifu afunue/anunurishe ndani yetu pia  hata kuuliza watu wengine wa dini waliosomea tu Imani/Biblia kidarasani na njia nyingine bora na sahihi za kupata maarifa na ufahamu wa jambo.

Tukiulizwa haya yafuatayo ya kitabu chetu tukiaminicho sana, tunafanyaje? Tukemee pepo au tujibu kwa ujasiri na hakika kabisa? Tujadiliane kwa haya chini.

Mdo.1:1=Mwandishi Dr. Luka anatoa dokezo kwa Mpendwa Theofilo kuhusu kile   kitabu cha  ‘’kwanza’’ alichoandika kuhusu aliyoyafanya na kufundisha Yesu. Ni kitabu gani icho alichoandika kuhusu aliyoanza kufanya na kufundisha Yesu? soma hii ina connect..Luka.1:1-4 Anasema Luka kua ‘’nimeona vema kukuandikia mpendwa Theofilo upate kujua hakika ya mambo uliyofundishwa.....’’. Kwaiyo inaonekana kwamba aliyeandika kitabu cha Luka( see 1: 3) ndiye aliyeandika Matendo(check mstari 1:1) ambaye ni Mr. Luka aliyekua tabibu( bila shaka utagundua pia aina ya uandishi na namna alivyo-present coverage ya maisha ya Yesu ukilinganisha na injili nyingine kama ya Marko na Mathayo. Mfano- Luka ananza kwa kusema- nimependa ktk Kiingereza.. ‘‘Having perfect understanding of all things from the very first to write you an ORDERLY account'', tafsiri nyingine zinasema..''I, myself have carefully investigated everything from the beginning''.. ), Kwa iyo huyu daktari baada ya kufanya ''careful investigation ndipo akaandika in an orderly manner.. Sasa kwakua ukweli ndio huo, kumetokea nini hapa? Tunawekaje uwiano hapa?

Mdo.9:4-7 hasa mstari 7…waliokua pamoja na Paul ktk msafara pia ‘’WALIISIKIA ile  sauti’’, si Paul tu lakini ktk Mdo.22:1-10 hasa mstari 9..Paul anaposhuhudia/anajitetea mbele ya kundi la waliompiga vibaya kidogo wamuue,anasema….waliokua naye ktk msafara ‘HAWAKUSIKIA ile sauti’.Hapa Mwandishi ni mmoja, ndani ya kitabu kimoja na tukio  lilelile moja.

Pia Mathayo.27:24-28 hasa mstari 28 ..Wakamvua Yesu nguo na kumvika vazi JEKUNDU (scarlet robe) lakini Marco.15:15-17 hasa mstari 17..Wakamvika vazi la rangi ya ZAMBARAU (purple).Hapa waandishi ni wawili tofauti ila tukio lilelile.

Kama mtu wa Mungu tena mwana wa Mungu ambaye Biblia kwako ni Kitabu chenye maneno ya Baba, Bwana na Roho wetu, unasemaje juu ya hili?

Swali limeulizwa Na: Edwin Seleli