Advertise Here

Sunday, September 1, 2013

Harusi ya Mwimbaji Emmy Kosgei na Mtume Anselm yafana.

Mtume Anseln Madubuko na Emmy Kosgei wakifunga ndoa
Jana ilikuwa ndiyo siku ya Harusi ya Mwimbaji mashuhuri wa nyimbo za Injli kutoka Nchini Kenya, Emmy Kosgei alipofunga ndoa na Mtume Anselm Madubuko raia wa Nigeria anayehudumu katika Kanisa la Revival Assembly Church lililopo Lagos, Nigeria.

Harusi yao ilifanyika katika hotel ya Safari Park na wamefunga ndoa huku Mtume Anselm Madubuko akiwa na umri wa Miaka 55 na Emmy Kosgei akiwa na umri wa Miaka 33.

Mke wa awali wa Mtume Anselm Madubuko alifariki mwezi wa 7. Jambo linalowashangaza wengi ni kuwahi kwake kuoa baada ya mke wake kufariki. Katika kuondoa utata huo, Mtume Anselm Madubuko amesema: “It is how I have chosen to do it. I have decided to move on. I found out that 10 years and even 20 years will not be enough to forget my late wife. The time anybody remarries has nothing to do with your former partner.”

Akiongelea namna walivyokutana na Emmy Kosgei alisema: “I met her in one of my trips abroad. We were both invited as guest ministers in an event. I was to minister as a preacher, while she as a music minister. When she ministered, I said to myself this girl has a good spirit. Later, I invited her as a guest artiste to perform in Azusa. People loved her and her music. I never knew things would turn out this way.”

Naye Emmy Kosgei alipohojiwa kuhusu uamuzi wake wa kuolewa na Mtume Anselm Madubuko alisema: “He loves me as I am and understands what I do. I wish people would mind their own business and let us be. He approached me and asked for my hand in marriage. He is the only man who had the confidence to approach me.”

Zifuatazo ni Picha za Harusi yao iliyofanyika Jumamosi ya Jana
High Table



 



Mtandao huu unawatakia Maisha Mema na yenye Baraka tele.