Advertise Here

Monday, September 2, 2013

Simanzi yatawala Mapokezi ya Mwili wa Marehemu Askofu Dr. Mosses Kulola Mwanza.

Ndege iliyobeba mwili wa Marehemu ikiwasili Uwanja wa ndege wa Mwanza
Jana mida ya Saa 7:09 Mchana, mwili wa Marehemu Dr. Mosses Kulola uliwasili uwanja wa ndege wa Mwanza na kupokelewa na watu mbalimbali akiwepo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. Engeneer Evarist Ndikilo, Maaskofu mbalimbali, Wachungaji, na waumini wa Makanisa mbalimbali Mwanza pasipo kujali Imani za dini zao.

Mwili huo baada ya kupokelewa ulipelekwa moja kwa moja nyumbani kwa Marehemu Askofu Dr. Mosses Kulola ambapo simanzi ilizidi na ni kama msiba ulianza upya kwani kila kona ilikuwa ni vilio tu.

Mwili wa Askofu Dr. Mosses Kulola utaagwa kesho katika Uwanja wa CCM Kirumba kuanzia mida ya Saa 4:00 Asubuhi hadi Saa 12:00 Jioni ili kuwapa nafasi nzuri na ya kutosha wakazi wa Mwanza na Mikoa Jirani kupata fursa ya kuuaga mwili wa Marehemu.

Hizi ni baadhi tu ya Picha za Mapokezi ya Jana, kuanzia Airport kuelekea nyumbani kwa Marehemu
Umati wa watu wakisubiri mwili wa Marehemu
Gari lililobeba Mwili wa Marehemu
Mtoto wa Marehemu Mch. Daniel Kulola (wa kwanza kushoto) akiwa na viongozi mbalimbali
Mch. Daniel Kulola (kushoto) na Mwl. Jacob (kulia)
Mke wa Marehemu akishuka kutoka kwenye ndege
Polisi nao walikuwepo wa kutosha kuhakikisha usalama unakuwepo
Emmanuel Mbasha
Watu wakiwa wamejipanga barabarani
Msafara wa Magari ukielekea nyumbani kwa Marehemu
Kwasasa mwili wa Marehemu umewekwa katika hospitali ya Bugando na kesho utakuwa ukiagwa katika Uwanja wa CCM Kirumba.


- Picha Zote na Baraka Samson -