Advertise Here

Saturday, October 20, 2012

Hiki ndicho kilichofanyika Jana katika Campus Night ya Tafes Saut.

USIKU wa kuamkia leo, ulikuwa ni Usiku wa Praise & Worship ulioandaliwa na Tanzania Fellowship of Evangerical Students(TAFES) tawi la Chuo Kikuu cha Mt. Augustino kilichopo Jijini Mwanza wakishirikiana na Radio ya Kikristo ya Jijini Mwanza HHC Alive Fm inayosikika kupitia Masafa ya 91.9Mhz na Online kupitia www.hhcalivefm.org.

Kwaya na Band mbalimbali zilihudumu wakiwemo wenyeji Tafes Saut Praise & Worship Team, Revival Mission Band(Wana wa Uzao wa Daudi), Casfeta Tayomi, Kingdom Worship, Huima Saut, Tafes Choir, Kihayile Group na wengine wengi.

Shughuli ilianza mida kama ya Saa 3 Usiku, huku Mnenaji katika Ibada hii maalum akiwa ni bishop Eugine Murisa kutoka Kanisa la High Way of Holiness Cathedral lililopo maeneo ya Ilemela Kanisani, Njiaa Kuu ya Kuelekea Airport.

Sasa tuambatane pamoja katika kutazama picha hizi zifuatazo ili upate picha halisi ya jinsi Tamasha hilo lilivyokuwa.........
Kijana wa Yesu Felix Mshama
Blogger Baraka Samson (Mjap Inc Blog)
Noel Mlabwa kwenye Drums
Kijana Sephon kwenye Keyboard
Yesu Juuuuuuuu..............! (Tafes Praise Team)
Wapi Vick Bongeeeeeee! a.k.a Photogenic
Pipooooooooooooooooooo............!
Kweli kwa Yesu ni Raha tupu!
Kingdom Worship on Stage
Pastor Goodluck Kyala wa Kanisa la New Vine International Church akiombea Matoleo
Wana wa Uzao wa Daudi waite Revival Mission Band Wazee wa Roboko
Bishop Eugine Murisa akitoa Neno
Maombi pia yalikuwepo
Sala ya Toba ikiendelea
Hawa ni Huima Saut
Bugando Praise & Worship Team
Kukosea Step ilikuwa ni Kosa la Jinai
Wana wa Kihayile a.k.a Kihayile Group
 Daima Mungu atukuzwe kwa Ukuu wake!