Advertise Here

Sunday, October 21, 2012

Butimba Gospel Fellowship waja na Album ya "Halleluya".


Sowane Emmanuel akiwa anafanya Mahojiano na Wanakwaya wa Butimba Gospel Fellowship katika Kipindi cha Gospel Sound
HAWA ndiyo wanakwaya wa Butimba Gospel Fellowship kutoka Chuo cha Ualimu cha Butimba Teachers Training College kilichopo maeneo ya Butimba, Jijini Mwanza.

Mwalimu wa Kundi hili ni Bahati Kihayile kutoka Kihayile Group. Na kwasasa Kwaya hii ina Album Moja ijulikanayo kama Halleluyah ambayo bado haijaanza kusambazwa rasmi.
Wanakwaya wa Butimba Gospel Fellowship wakiwa Studio za HHC Alive Fm ya Jijini Mwanza. Wa kwanza Kushoto ni Bahati Kihayile(Mwalimu wa Kwaya)
Waliyasema hayo wakiwa katika Kipindi cha Gospel Sound kinachoruka kila Siku ya Jumamosi kuanzia Saa 8:00 - 10:00 Jioni, kupitia Radio ya Kikristo ya HHC Alive Fm(91.9Mhz) ya Jijini Mwanza.

Album hiyo ina Jumla ya Nyimbo 10, na baadhi ya Nyimbo hizo ni kama Injili, It is Good, Halleluya, Tujipe Moyo na Nitayainua. Malengo yao ni Kununua vifaa vya Muziki vitakavyowawezesha kuimba live katika Matamasha na Huduma Mbalimbali.