Advertise Here

Tuesday, October 30, 2012

Video Shooting ya Album ya "U Mwema Rafiki" ya Noel Mlabwa, Felix Mshama, na Barnabas Shija.

Papaa Noel Mlabwa(Wa Kwanza Mbele), Felix Mshama(Nyuma Kushoto) na Barnabas Shija(Nyuma Kulia)
"U MWEMA Rafiki" ndiyo project inayoendelea hivi sasa chini ya Noel Mlabwa(Papaa), Felix Mshama, na Barnabas Shija. Project hii ni ya Utengenezaji wa Album ya Audio na Video kwa Pamoja.

Jana zilirekodiwa Video za Nyimbo nyingine 3, ambapo Blog hii ilishuhudia zoezi zima la ku'shoot Video hizo. Sasa Tazama Picha hizi ili kujua nini kiliendelea katika zoezi hilo liliochukua muda wa kama Masaa 9 hivi.
Kinye kazini akiwa anaisaka shot moja kali sana

Vijana hawa wote ni Mazao ya Tanzania Fellowsip of Evangerical Students(Tafes) ya Chuo Kikuu cha Mt. Agustino - Mwanza.
 
Video ya Kwanza ya U Mwema ilishatengezwa na Kampuni ya Kinye Media chini ya Video Producer Wynjones a.k.a Kinye, Kampuni ambayo inasimamia utengenezaji wa Video za Nyimbo zote zilizopo kwenye Audio album yao.
Video Producer Wynjones a.k.a Kinye
 Baadhi ya Nyimbo zitakazokuwepo kwenye Video Albam hiyo ni Rafiki, U Mwema, Mungu si Mwanadamu, Amani, Yatima, Utukufu na Cha Kutumaini.
 Kwa Maelezo yao wanasema mpaka kufikia Mwishoni mwa Mwezi Novemba, Audio na Video Albam zote zitakuwa tayari, na zitaanza kupatikana katika maeneo ambayo watayataja pindi Albam hizo zikikamilika.
Cameraman Julius Mahela akijaribu kupata Closeup Shot ya Felix
 Hii ndiyo Video ya wimbo wa U Mwema ya Noel, Felix na Barnabas iliyofanywa na Kinye Media