Advertise Here

Sunday, October 28, 2012

Mwanza Gospel Team yawachakaza Vijana wa Gilgal kwa Ushindi wa Goli 2-1.

Kikosi cha Mwanza Gospel Team
 JANA katika Viwanja vya Kanisa la Baptist Jijini Mwanza, ulifanyika mpambano mkali wa kupimana nguvu kati ya Mwanza Gospel Team na Vijana wa Kanisa la Gilgal.
Kikosi cha Vijana wa Kanisa la Gilgal
Vijana wa Kanisa la Gilgal ndio waliokuwa wa Kwanza kuzifumania nyavu za Mwanza Gospel Team katika dakika ya 27 ya kipindi cha Kwanza. Matokeo yalibaki hivyo mpaka kuisha kwa Kipindi cha Kwanza.
Mechi ikiendelea
Kipindi cha Pili kilikuwa cha tofauti kidogo kwani Mwanza Gospel Team walifanikiwa kupata goli la kusawazisha katika dakika ya 68. Hii ni baada ya Kocha kufanya mabadiliko katika safu ya ushambuliaji.
Benchi la Ufundi la Mwanza Gospel Team
 Dakika ya 73 Mwanza Gospel Team ilifanikiwa kupata Goli lake la Pili na kufanya Matokeo yawe Goli 2 kwa 1.

Mashambulizi yakizidi kwenye Ngome ya Vijana wa Kanisa la Gilgal
Mashabiki nao hawakuachwa nyuma, walikuwa makini sana kufuatilia mpira mwanzo hadi mwisho.
Mashabiki
 Na kila goli lilipokuwa likiingia nyavuni, Mashabiki nao morali ikawa inapanda.
Mashabiki wakishangilia
 Ilipokuwa ikitokea foward kukosa goli, mambo yalikuwa hivi.....
Mashabiki wa Gilgal wakishangaa baada ya foward yao kukosa goli la wazi kabisa
Huyu ni moja ya Beki machachari sana wa Mwanza Gospel Team
Yusuph Magupa baada ya kutoka Uwanjani
 Zuli a.k.a Mwarabu, ndiye kocha aliyehakikisha Mwanza Gospel Team inapata Ushindi. Team hii inaundwa na Watangazaji wa Radio za Kikristo za Jijini Mwanza pamoja na Waimbaji wa Nyimbo za Injili wa Jijini Mwanza.
Kocha wa Mwanza Gospel Team, Zuli a.k.a Mwarabu
 President Maganga James Gwesaga toka Living Water Fm(103.3Mhz), ndiye Team Captain wa Mwanza Gospel Team. Baadhi ya wachezaji wengine kutoka Radio za Kikristo za Jijini Mwanza ni kama Joshua Dede na Jackson(Kwa Neema Fm), Fabian Fanuel(Living Water Fm), Adolph Nzwalla, Sowane Emmanuel, na Erasto Juma(HHC Alive Fm).
Maganga James Gwensaga
Mpaka mwisho wa Mechi unafika, Mwanza Gospel Team waliibuka kidedea kwa kuwafunga Vijana wa Kanisa la Gilgal Magoli 2 kwa 1.