Advertise Here

Tuesday, October 23, 2012

T.B Joshua atabiri kutokea kwa Mafuriko Nchini Nigeria.

T.B Joshua
MTUME T.B Joshua kutoka Kanisa la Synagogue Church of All Nations(SCOAN) la Nchini Nigeria, ametabiri kutokea kwa mvua kali zitakazosababisha Mafuriko nchini humo.

Akizungumza katika Ibada ya Jumapili iliyopita na kurushwa live na Kituo cha luninga cha Emmanuel Tv kinachomilikiwa na Kanisa hilo, T.B Joshua alisema "It is always sensitive to talk about our country. Before you know it, they will say that is another thing. May God forgive us."

Amesema kuwa mvua hizo zitasababisha mafuriko makubwa sana ambayo yataleta uharibifu katika baadhi ya maeneo ya Nigeria. Baadhi ya watu watapoteza Nyumba zao na wengine watakufa kutokana na Mafuriko hayo.

Amewaomba wananchi wa Nigeria kuomba sana kwa ajili ya Jambo hilo ili Mungu aepushe Mafuriko hayo kwani Viongozi wa Nchi hiyo wanapuuzia Jambo hilo.

Tazama Video hii kuona alichokizungumza T.B Joshua katika Ibada hiyo...