Advertise Here

Saturday, October 27, 2012

Semina Maalum ya Mabinti Jijini Mwanza.

KANISA la New Vine International kupitia New Vine International Ministries wanakuletea Semina Maalum kwa Ajili ya Mabinti iliyopewa Jina la Ladies Evening.

Semina hiyo itafanyika Jumapili ya Kesho yaani Octoba 28, 2012 kuanzia Saa 9:00 Alasiri - 1:00 Usiku katika Kanisa la New Vine International lililoko maeneo ya Nyegezi, ndani ya Tema Hotel(Ukumbi Mkubwa).

Wanenaji katika Semina hiyo ni Pastor Goodluck Kyara(Rais wa New Vine International Ministries) na Lucy Ikachoi(Mhasibu wa Constech Co. Ltd).

Hakuna Kiingilio, na Mabinti wote wa Jijini Mwanza Mnakaribishwa sana.

- Vaa Upendeze -