Advertise Here

Friday, October 18, 2013

Changia Ujenzi wa Kaburi la Askofu Dr. Mosses Kulola.

Marehemu Askofu Dr. Mosses Kulola enzi za Uhai wake.
Ikiwa imepita Miezi kadhaa baada ya Kufariki kwa Shujaa wa Injili Askofu Dr. Mosses Kulola, Ujenzi wa Kaburi lake lililopo Kanisa la EAGT Bugando - Mwanza Umeanza ili kuhifadhi Kaburi hilo katika hali nzuri.
Ujenzi wa Kaburi ulipofikia
Kupitia Ukurasa wake wa Facebook, Mtoto wa Askofu Mosses Kulola ambaye ni Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya - Mwanza, Mch. Daniel Kulola amesema Ujenzi huo Umeshaanza lakini kwa sasa wamesisima ili kuvuta nguvu kwanza ya kumalizia Ujenzi huo.

Sehemu iliyobaki ni Ripu, Matofali ya Kuziba mahali walipopanga, vigae vizuri, Cement, Rangi, n.k. Kama utaguswa na Ujenzi wa Kaburi hili, na utapenda kuchangia chochote kwa ajili ya Ujenzi wa Kaburi hili, Waweza kutumia Mpesa Namba: 0767 749040 na Kwa walio mbali waweza kutumia Huduma ya Western Union na Maelezo ya siri ya Muamala huo ukatuma kwenda kwenye Email:
Muonekano wa Kaburi kwa ndani
Karibu tushiriki Pamoja katika Kujenga Kaburi la Shujaa wa Imani Tanzania mpendwa wetu Askofu Mosses Kulola.