Advertise Here

Sunday, October 27, 2013

Yaliyojiri kwenye Usiku wa Uamsho pale CCM Kirumba.

Usiku wa Ijumaa kuamkia Jumamosi ulikuwa ni Usiku wa Uamsho yaani Revival Night. Usiku huo wa Kusifu, Kuabudu, Maombi na Maombezi ulifanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, Usiku uliondaliwa na Tafes Mkoa wa Mwanza kwa Kushirikiana na Radio ya Kikristo ya Hhc Alive Fm(91.9Mhz) ya Jijini Mwanza.

Ulikuwa ni Usiku wa Baraka sana kwani mbali ya maombi mbalimbali pia kulikuwa na Maombi maalum Juu ya Taifa letu la Tanzania, huku watumishi wa Mungu mbalimbali wakifundisha Neno la Mungu akiwemo Askofu Eugene Murisa wa Kanisa la Highway of Holiness Cathedral la Ilemela Mwanza, huku Ma'Mc wa Event hiyo wakiwa ni Sowane Emmanuel na Albert Francis.

Vikundi Mbalimbali vya waimbaji na waimbaji binafsi walihudumu huku Jackson Benty kutoka Arusha akihudhuria pamoja na kuhudumu katika Mkesha huo wa Kipekee kufanyika chini ya Tafes Mkoa wa Mwanza.

Sasa Mambo yenyewe yalikuwa hivi
Tafes Praise Team ya Mkoa


Revival Mission Band
Kihayile group
Tafes Saut Dadaz
Askofu Eugene Murisa
Ma'Mc Sowane Emmanuel(Kushoto) na Albert Francis(Kulia)
Askofu Murisa akihubiri
Askofu Murisa akiombea watu waliofika Uwanjani hapo
Jackson Benty akihudumu
Mr. Madaha(M/Kiti Tafes Mkoa wa Mwanza)
Viongozi Kamati ya Maandalizi
- Utukufu urudi kwake yeye aliye Mkuu kupita wote -