Advertise Here

Thursday, October 31, 2013

Mwimbaji Namatayi Chipanga wa Zimbabwe achaguliwa Kushiriki Tuzo za "Women in Enterprise".

New and celebrated music couple, Charles and Namatayi Chipanga, are back in the limelight
Namatayi akiwa na Mumewe Charles Chipanga
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili kutoka Zimbabwe Namatayi Chipanga amechaguliwa kushiriki katika Tuzo za Heshima za “Women in Enterprise Awards" za Nchini Zimbabwe, Tuzo zitakazotolewa kesho huku Mgeni Rasmi katika Tuzo hizo akiwa ni Mwanamke Mfanyabiashara kutoka Afrika Mashariki Gloria Serobe.

Mwenyekiti wa Dawati la Wanawake la "Zimbabwe National Chamber of Commerce" Divine Ndlukula amesema Tuzo hizo zina lengo la kuwatunuku Wanawake waliofanikiwa katika Shughuli zao.

Namatayi alizaliwa Livingstone, Zambia na ameolewa na Mwimbaji Charles Chipanga. Licha ya Upekee wa Sauti yake, pia Namatayi ni Mwimbaji mwenye Mafanikio Makubwa sana Nchini Zimbabwe katika Tasnia ya Muziki wa Injili Nchini Zimbabwe.

Tazama moja ya Kazi za Namatayi akiwa anaimba LIVE Wimbo wa "Gore Rangu" yeye pamoja na Mumewe Charles Chipanga