Advertise Here

Tuesday, October 29, 2013

Emmy Kosgei ashinda Tuzo ya BEFFTA.

Emmy Kosgei akiwa na Annie
Mwimbaji maarufu wa Nyimbo za injili toka Nchini Kenya Emmy Kosgei Ijumaa iliyopita alipata Tuzo ya "Best International Gospel Act", Tuzo iliyotolewa na BEFFTA (Black Entertainment Film Fashion Television and Arts) iliyofanyika huko U.K.
Emmy Kosgei
Emmy Kosgei akiwa anaingia Ukumbini hapo
Emmy Kosgei ambaye amefunga ndoa kipindi kifupi kilichopita na Mtume Anselm Madubuko wa Nigeria, alikuwa Russia kihuduma baada ya Kutoka Honeymoon ya Ndoa yao, na Mwaka huu kwake umekuwa ni Mwaka wa Baraka sana.
Emmy Kosgei akipokea Tuzo yake
Kupitia ukurasa wake wa Facebook Emmy Kosgei kaandika Maneno haya It is here ladies n gentlemen... The BEFFTA AWARD 2013. 'Best International Gospel Act ‘! Home safely! This is ur award. .. Thanks for voting n support. , we give all the glory to God!!! He has done it for us again … May God bless u n have a blessed week ahead...lov yall!

Pia katika Orodha ya Washindi yupo Anne Kasiime kutoka Uganda aliyeshinda Tuzo ya "Best Comedian".